Abdalah Abdulrahman
JF-Expert Member
- Aug 29, 2019
- 222
- 201
Kawaida ya mfumo wa kidemokrasia ni kuheshimu na kuyapa nafasi mawazo ya wananchi hata yakiwa ni ya watu wachache. Ni katika msingi huu Tanzania mwaka 1992 iliingia katika mfumo wa siasa za vyama vingi japo maoni ya wananchi wengi yalipinga mfumo huu.
Ni wachache wanafahamu kuwa Tanzania tofauti na nchi zingine iliingia katika mfumo huu kwa umakini na tahadhari kubwa ikiwa na lengo la kulinda uhuru wake na kuwalinda wananchi wake.Hii ndio sababu kubwa ya madhara hasi ya demorasia kwa nchi yetu kuwa madogo ukilinganisha na madhara ya mfumo huu katika nchi zingine duniani.Ni wazi kuwa viongozi wetu walifuata msemo wa ”Akili za kuambiwa…..”
Ni wzi kuwa mfumo wa kidemokrasia nchini umepitia changamoto nyingi na umekua ukiimarika kuanzia awamu ya Pili ya Raisi Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,awamu ya tatu ya Raisi Mstaafu Benjamin Mkapa,awamu ya nne ya Raisi Mstaafu Jakaya Kikwete na awamu hii ya tano ya Raisi John Magufuli.
Kawaida ya mifumo hii ambayo huletwa na nchi zilizoendelea ina kuwa na malengo ya wazi na yale yaliyo fichikana ambayo ni yanafaida na hasara kwa nchi,ndio maana yapo mazuri na mabaya ya mfumo wa vyama vingi ambayo kila mmoja wetu anaweza kuya ainisha.Yapo pia yale ambayo yamefichikana na yanahitaji akili kubwa kuweza kuya ainisha kwani madhara yake hayaonekani haraka au hayatabiriki.
Kwa mfano,maadui wa Tanzania ambao hawatakii mema watanzania wanaweza kuja na hoja ya kuwepo kwa Tume huru katika kipindi hiki kifupi kuelekea uchaguzi mkuu October 2020 kwa lengo la kukatisha wapinzani tamaa kushiriki katika uchaguzi ujao ili wananchi wasipate viongozi wanaowataka,au kuleta machafuko ili taasisi ambazo zinashughulika na wakimbizi zipate kazi ya kufanya na kuturejesha nyuma kimaendeleo.
Mitego kama hii kwa serikali inahitaji akili kubwa kuweza kujua makusudio ya viongozi hawa ukizingatia hatua ambazo Tanzania imepiga katika maendeleo.
Sote tunafahamu kuwa Tume ya Uchaguzi Tanzania imeundwa kwa mujibu wa katiba ya Tanzania ambayo inaelezea wazi juu ya uhuru wa Tume hii.Sio Raisi wa Jamhuri ya Muungano au Raisi wa Zanzibar anaweza kuingilia majukumu na maamuzi ya Tume hii. Hivyo basi nina imani kuwa Tume ya Uchaguzi iliyopo ni tume huru na yenye watendaji waadilifu na wazalendo ambao watatenda haki kwa maslai ya Taifa.
Pili, muundo wa tume ambao baadhi ya wapinzani wanaulaalamikia kwamba wasimamizi wa uchaguzi wanakuwa wakurugenzi wa halmashauri za miji, manispaa na wilaya ni hoja pofu kwani ni viongozi hawa wenye uadilifu mkubwa wamefanya kazi kubwa ya kizalendo kuleta maendeleo makubwa ambayo kila mtazania anayafurahia.
Ni vigumu kwa serikali makini kuweza kuweka watu ambao sio wazalendo ambao wamekuwa wakitumika na wanaendelea kutumika na maadui wa Tanzania.Ipo mifano anuai ya viongozi wa upinzani na ushiki wao katika kuhujumu ndege zetu,madini yetu na kadhalika.
Tunataka Tume Adilifu na zalendo kwa mustakabali mwema wa Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania
Ni wachache wanafahamu kuwa Tanzania tofauti na nchi zingine iliingia katika mfumo huu kwa umakini na tahadhari kubwa ikiwa na lengo la kulinda uhuru wake na kuwalinda wananchi wake.Hii ndio sababu kubwa ya madhara hasi ya demorasia kwa nchi yetu kuwa madogo ukilinganisha na madhara ya mfumo huu katika nchi zingine duniani.Ni wazi kuwa viongozi wetu walifuata msemo wa ”Akili za kuambiwa…..”
Ni wzi kuwa mfumo wa kidemokrasia nchini umepitia changamoto nyingi na umekua ukiimarika kuanzia awamu ya Pili ya Raisi Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,awamu ya tatu ya Raisi Mstaafu Benjamin Mkapa,awamu ya nne ya Raisi Mstaafu Jakaya Kikwete na awamu hii ya tano ya Raisi John Magufuli.
Kawaida ya mifumo hii ambayo huletwa na nchi zilizoendelea ina kuwa na malengo ya wazi na yale yaliyo fichikana ambayo ni yanafaida na hasara kwa nchi,ndio maana yapo mazuri na mabaya ya mfumo wa vyama vingi ambayo kila mmoja wetu anaweza kuya ainisha.Yapo pia yale ambayo yamefichikana na yanahitaji akili kubwa kuweza kuya ainisha kwani madhara yake hayaonekani haraka au hayatabiriki.
Kwa mfano,maadui wa Tanzania ambao hawatakii mema watanzania wanaweza kuja na hoja ya kuwepo kwa Tume huru katika kipindi hiki kifupi kuelekea uchaguzi mkuu October 2020 kwa lengo la kukatisha wapinzani tamaa kushiriki katika uchaguzi ujao ili wananchi wasipate viongozi wanaowataka,au kuleta machafuko ili taasisi ambazo zinashughulika na wakimbizi zipate kazi ya kufanya na kuturejesha nyuma kimaendeleo.
Mitego kama hii kwa serikali inahitaji akili kubwa kuweza kujua makusudio ya viongozi hawa ukizingatia hatua ambazo Tanzania imepiga katika maendeleo.
Sote tunafahamu kuwa Tume ya Uchaguzi Tanzania imeundwa kwa mujibu wa katiba ya Tanzania ambayo inaelezea wazi juu ya uhuru wa Tume hii.Sio Raisi wa Jamhuri ya Muungano au Raisi wa Zanzibar anaweza kuingilia majukumu na maamuzi ya Tume hii. Hivyo basi nina imani kuwa Tume ya Uchaguzi iliyopo ni tume huru na yenye watendaji waadilifu na wazalendo ambao watatenda haki kwa maslai ya Taifa.
Pili, muundo wa tume ambao baadhi ya wapinzani wanaulaalamikia kwamba wasimamizi wa uchaguzi wanakuwa wakurugenzi wa halmashauri za miji, manispaa na wilaya ni hoja pofu kwani ni viongozi hawa wenye uadilifu mkubwa wamefanya kazi kubwa ya kizalendo kuleta maendeleo makubwa ambayo kila mtazania anayafurahia.
Ni vigumu kwa serikali makini kuweza kuweka watu ambao sio wazalendo ambao wamekuwa wakitumika na wanaendelea kutumika na maadui wa Tanzania.Ipo mifano anuai ya viongozi wa upinzani na ushiki wao katika kuhujumu ndege zetu,madini yetu na kadhalika.
Tunataka Tume Adilifu na zalendo kwa mustakabali mwema wa Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania