Uchaguzi 2020 Je, Tume itapoteza nini ikiruhusu watu wote ambao waliomba kugombea kwa vyama tofauti wagombee bila kujali masharti?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,435
5,404
Ndugu zangu,

Kuna mambo kadhaa ambayo yanaendelea katika uchaguzi huu ambayo naona ni hatari sana kwa mustakabali wa demokrasia yetu. Wagombea wengi sana wameenguliwa na tume kwa vigezo mbalimbali ikiwamo swala la idadi ya wadhamini, kukosea kujaza fomu katika maeneo machache na sababu nyingine nyingi ambazo kimsingi hazina mantiki hasa ukizingatia kwamba kazi ya tume sio kuwachaguliwa wananchi viongozi kwa kutumia vigezo vyao bali kazi yao ni kusimamia uchaguzi.

Binafsi naona tatizo kubwa sana ambalo tume inalileta ambalo athari yake hatutaiona sasa hivi bali tutaiona baada ya uchaguzi huu. Kama tume haitachukua hatua madhubuti mambo mengi sana ambayo hatuyataki yatokee yanaweza kutokea katika nchi hii.

Maoni yangu kwa tume ni haya:
Kwanza, tume itambue kwamba kipindi cha uchaguzi ndo kipindi ambacho wananchi wanaweza kuwa na mijadala ya wazi kuhusu mustakabali wa nchi yao bila kujali kiwango chao cha elimu n.k. Hivyo basi kuwanyima wagombea kushiriki katika uchaguzi ni sawa na kuwanyima fursa ya kuwa sehemu ya mjada huu muhimu. Je, tume inafanya haya kwa maslahi ya nani?Inataka kuharibu uchaguzi kwa maslahi ya nani? Kwani tume inawalipia hao watu gharama za kampeni?Kuna gharama zozote tume inazipunguza kwa kuwakata?

Tume iache hili suala liende kwa mujibu wa haki za raia na wale wote waliotia nia kugombea bila kujali kama walifikisha vigezo au la waruhusiwe kugombea kama kweli wanathamani amani ya nchi yetu.

Haya ni maoni yangu binafsi na tunaweza kuyajadili kwa pamoja na kukubaliana au kutokubaliana.

Asante
 
Utamruhusu mgombea ambaye hata kujaza jina lake agombee ndio awe mwakilishi wa Wananchi?

Chadema mnataka kutuharibia Nchi, mfuateni robertison wa Amsterdam mkaishi kule atawapa uhuru

Wewe mfuate Gwajima kule kwenye kanisa lake ukapate kuliwa vutu
 
Wanataka kina Nape, Majaliwa na Makamba waongezee nguvu kumnadi Magufuli.
 
Brother kila kinakwenda kwa Sheria na utaratibu, hata nyumbani kwako una Sheria na utaratibu uliojiwekea. Tafadhali usizame kwenye siasa ukasahau taratibu.
 
Utamruhusu mgombea ambaye hata kujaza jina lake agombee ndio awe mwakilishi wa Wananchi?

Chadema mnataka kutuharibia Nchi, mfuateni robertison wa Amsterdam mkaishi kule atawapa uhuru
Mkuu,unaelewa unachosema?Huyo ndo m,uwakilishi wa wananchi kama hajui kuandika jina lake kwa mujibu wa taratibu zenu bado anawakilisha wananchi.Unaweza usielewe kama wanafaa kuwa viongozi kwa sababu hawako CCM ila watakapoanza kukuonesha kile wanachojua ndo utaelewa kile ninachokisema.
 
Brother kila kinakwenda kwa Sheria na utaratibu, hata nyumbani kwako una Sheria na utaratibu uliojiwekea. Tafadhali usizame kwenye siasa ukasahau taratibu.
Mkuu utaratibu upi?Unajua kilichofanyika au unahisi kwamba wagombea wa upinzani wpte hawajui utaratibu na wagombea wa CCM wote wanajua utaratibu?

Mimi nakueleza kile ninchokifahamu,ninachokiamini na ninachokisema.kama unafikiri kwamba nimezama kwenye SIASA na sijui utaratibu basi utasubiri sana siku nitakukuonesha utaratibu ni upi.
 
Sasa mtu hawezi hata kujaza fomu, ataweza kweli kutunga sheria? Hebu kuweni siliasi kidogo
Mkuu,unaelewa unachosema?Wabunge wa CCM wengi hawajui kusoma na hawajakosea kwenye fomu zao ila upinzani hadi watu wenye degree wamekosea kujaza fomu.Unaona kwamba hakuna tatizo hapo?Funguka mkuu.
 
Brother kila kinakwenda kwa Sheria na utaratibu, hata nyumbani kwako una Sheria na utaratibu uliojiwekea. Tafadhali usizame kwenye siasa ukasahau taratibu.
Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kuichagua tena hii Serikali ya WATEKA NYARA, mamia kwa maelfu wanakusanyika huko kupata BURUDANI YA WASANII tu. Kusitishwa kwa matamasha kwaajili ya COVID-19 kuliwaacha watu wengi katika lindi la upweke.
 
Utamruhusu mgombea ambaye hata kujaza jina lake agombee ndio awe mwakilishi wa Wananchi?

Chadema mnataka kutuharibia Nchi, mfuateni robertison wa Amsterdam mkaishi kule atawapa uhuru
Kwa maagizo toja juu wameenguliwa wale wa Upinzani walioonekana ni tishio kwa ushindi wa watia nia wa CCM ili watendaji wa Time nao wasipoteze ajira zao. Kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mbinu hizihizi zilitumika kuengua wapinzani lakini baada ya vyama vya Upinzani kususia Uchaguzi walirudishwa wote lakini kwa kuwa walikuwa wamesusa wale wa CCM wakapita bila kupingwa. Kwenye hili Upinzani wanataka wagombea wao warudishwe na wamesema hawatasusia Uchaguzi, maagizo toka juu yako palepale na njaa ya wafanyakazi wa Tume iko palepale na wagombea wa CCM lazima washinde kwa kishindo. Ndo maana CCM hawataki kusikia Tume Huru.
 
Ndugu zangu,

Kuna mambo kadhaa ambayo yanaendelea katika uchaguzi huu ambayo naona ni hatari sana kwa mustakabali wa demokrasia yetu. Wagombea wengi sana wameenguliwa na tume kwa vigezo mbalimbali ikiwamo swala la idadi ya wadhamini, kukosea kujaza fomu katika maeneo machache na sababu nyingine nyingi ambazo kimsingi hazina mantiki hasa ukizingatia kwamba kazi ya tume sio kuwachaguliwa wananchi viongozi kwa kutumia vigezo vyao bali kazi yao ni kusimamia uchaguzi.

Binafsi naona tatizo kubwa sana ambalo tume inalileta ambalo athari yake hatutaiona sasa hivi bali tutaiona baada ya uchaguzi huu. Kama tume haitachukua hatua madhubuti mambo mengi sana ambayo hatuyataki yatokee yanaweza kutokea katika nchi hii.

Maoni yangu kwa tume ni haya:
Kwanza, tume itambue kwamba kipindi cha uchaguzi ndo kipindi ambacho wananchi wanaweza kuwa na mijadala ya wazi kuhusu mustakabali wa nchi yao bila kujali kiwango chao cha elimu n.k. Hivyo basi kuwanyima wagombea kushiriki katika uchaguzi ni sawa na kuwanyima fursa ya kuwa sehemu ya mjada huu muhimu. Je, tume inafanya haya kwa maslahi ya nani?Inataka kuharibu uchaguzi kwa maslahi ya nani? Kwani tume inawalipia hao watu gharama za kampeni?Kuna gharama zozote tume inazipunguza kwa kuwakata?

Tume iache hili suala liende kwa mujibu wa haki za raia na wale wote waliotia nia kugombea bila kujali kama walifikisha vigezo au la waruhusiwe kugombea kama kweli wanathamani amani ya nchi yetu.

Haya ni maoni yangu binafsi na tunaweza kuyajadili kwa pamoja na kukubaliana au kutokubaliana.

Asante
Jambo la ajabu ni kwamba ni wagombea wa upinza tu ndio walioenguliwa na kwa ujumla wanakaribia 1,500.
 
Ndugu zangu,

Kuna mambo kadhaa ambayo yanaendelea katika uchaguzi huu ambayo naona ni hatari sana kwa mustakabali wa demokrasia yetu. Wagombea wengi sana wameenguliwa na tume kwa vigezo mbalimbali ikiwamo swala la idadi ya wadhamini, kukosea kujaza fomu katika maeneo machache na sababu nyingine nyingi ambazo kimsingi hazina mantiki hasa ukizingatia kwamba kazi ya tume sio kuwachaguliwa wananchi viongozi kwa kutumia vigezo vyao bali kazi yao ni kusimamia uchaguzi.

Binafsi naona tatizo kubwa sana ambalo tume inalileta ambalo athari yake hatutaiona sasa hivi bali tutaiona baada ya uchaguzi huu. Kama tume haitachukua hatua madhubuti mambo mengi sana ambayo hatuyataki yatokee yanaweza kutokea katika nchi hii.

Maoni yangu kwa tume ni haya:
Kwanza, tume itambue kwamba kipindi cha uchaguzi ndo kipindi ambacho wananchi wanaweza kuwa na mijadala ya wazi kuhusu mustakabali wa nchi yao bila kujali kiwango chao cha elimu n.k. Hivyo basi kuwanyima wagombea kushiriki katika uchaguzi ni sawa na kuwanyima fursa ya kuwa sehemu ya mjada huu muhimu. Je, tume inafanya haya kwa maslahi ya nani?Inataka kuharibu uchaguzi kwa maslahi ya nani? Kwani tume inawalipia hao watu gharama za kampeni?Kuna gharama zozote tume inazipunguza kwa kuwakata?

Tume iache hili suala liende kwa mujibu wa haki za raia na wale wote waliotia nia kugombea bila kujali kama walifikisha vigezo au la waruhusiwe kugombea kama kweli wanathamani amani ya nchi yetu.

Haya ni maoni yangu binafsi na tunaweza kuyajadili kwa pamoja na kukubaliana au kutokubaliana.

Asante
Itakuwa imekiuka maagizo ya ndugu magufuli
 
Hofu Ni angalau ccm isipoteze majimbo yote angalau mengine wapite bila kupingwa kwa kubebwa na tume,wanaokosea kujaza formu Ni wapinzani tu
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom