Je Tax Exemptions ni kwa ajili ya Taifa au baadhi ya viongozi

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
7,610
3,152
Kwa muda nime kuwa nafikiria kuhusu suala la tax exemption na mambo yanavyo kwenda nchini, kama tulivyo elezwa hivi karibuni kuhusu makampuni makubwa kutolipa kodi , kama VODa ambapo rostam yupo Elinino Yumo wengine kama Msekwa alipata kuwa mwenyekiti wa Bodi,Watoto wa baadhi ya viongozi wapo, Cocacola, Hotel za Kitalii na kwenye Sekta ya madini.
suala la kujiuliza na ukihusisha mahusiano ya hayo makampuni, tunaona ni kwamba ni hatua au njama za maksudi ya baadhi ya viongozi kujipatia mitaji kwa mgongo wa wa tanzania wote kwa ujumla wetu. na bahati mbaya kuna baadhi ya wabunge wanapitisha hii miswada bila kujua madhara yake na ni kwa faida ya nani.
Naomba tujadili hili kwa faida ya nchi yetu, na kama hii mada inafaa kuwekwa katika fungu lolote naomba kwa muda iache hapa kwa faida yetu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom