Je! tatizo ni nini? Na nani chanzo cha tatizo hili?

Daudi1

JF-Expert Member
Dec 14, 2013
8,758
8,630
Habari wanajamvi, bila kupoteza muda niingie kwenye maada husika

Siku za hivi karibuni vijana Baadhi ya wanawake wamejivua utu wao na kuanza kujihusisha kimapenzi na vijana wadogo wengine kwa umri walitakiwa kuwa watoto wao(Naongelea serengeti boys na sugar mumys), sababu zipo nyingi za wao kufanya hivyo ikiwemo kutoridhishwa na waume zao wengine wanataka faraja kwa hao vijana wakidai kuwa ni wapweke labda baada ya kuondokewa na waume zao lakini wangine wanataka kujigeuza vichwa vya nyumba.

Na kwa sababu mara nyingi wanawake wenye hulka hizo za kupenda serengeti boys kiuchumi wanajiweza hivyo vijana hufanya kila jitihada ili waweze kuwaridhisha wa kina mama hao ili wasipoteze ajira yao hivyo wamejikuta wakitumia madawa mbali mbali ili kuongeza nguvu za kiume na kuongeza maumbile yao ya kiume ili waweze kunata na beat. Imefika kipindi wanawake wanaomba talaka au wanaleta vimbwanga kwa waume zao ili wapewe talaka ili wafanye yao na serenget boys kwa raha bila bugdha yoyote hapa nina mfano hai kuna mama mtu mzima ambaye alikuwa ni mke wa pili kwa mzee mmoja jirani na ninapoish ameomba talaka, wakt huo huo mchepuko wake ni kijana mdogo sana jamaniii!!!

Hoja zangu za msingi:
1. Imekuaje wanawake mmejivua utu kwa sababu ya tamaa za mwili tuu kwa sababu siamini kama kuna mapenzi hapo, umemzidi mwanaume miaka kumi maana yake umemzidi kila kitu kiakili, kiuchumi tatzo ni nini hasa?

2. Je chanzo ni wanaume kutotimiza haja za miili yenu? je hawa vijana ambao wanatumia madawa ili kuridhisha nafsi zenu hamuoni miaka ya mbeleni huko binti zenu hawatakuwa na wanaume wenye nguvu za kutosha na itakuwa chanzo kikubwa usagaji miaka ya baadaye?

3. Au ndo huu utandawazi unafanya yake watu hawajali lolote, Mungu wamemuacha nyuma?

Naomba tujikite katika maada, tusishambuliane sisi kwa sisi tukatoka nje ya maada, tujitahidi kuheshimu mawazo ya mtu. Asante
Nawasilisha hoja

 
Mkuu wapo kweli wenye tatizo la kutoridhika ktk tendo la ndoa kutokana na matatizo mbali mbali ya waume zao kama sukari nk. Lakini wapo wengeni wanafuata mkumbo tu, na wengine ni tamaa za ngono za damu changa.
 
Mkuu wapo kweli wenye tatizo la kutoridhika ktk tendo la ndoa kutokana na matatizo mbali mbali ya waume zao kama sukari nk. Lakini wapo wengeni wanafuata mkumbo tu, na wengine ni tamaa za ngono za damu changa.
inawezekana kweli kwa mwanaume aliye na kisukari ni ngumu kumridhisha mkewe je hiyo ni tiket ya kusaka serenget boys hakuna wanaume wenye umri mkubwa wenye uwezo wa kumridhisha?
 
inawezekana kweli kwa mwanaume aliye na kisukari ni ngumu kumridhisha mkewe je hiyo ni tiket ya kusaka serenget boys hakuna wanaume wenye umri mkubwa wenye uwezo wa kumridhisha?

Mkuu tatizo siyo umri tu bali uaminifu hakuna ktk ndoa nyingi, pia mume anafanya tendo la ndoa na mke wake kwa heshima, mke akitoka nje kwa serengeti boyz anakutana shughuri pevu, basi anakuwa akija nyumbani anatimoza wajibu tu mchezo mzima anatoka nje.
 
mmmh wanawake wengine hawaridhiki tu wengine waume zao hawawaridhishi japo walitakiwa kukaa chini wasolve tatizo na sio kuchepuka uaminifu siku hizi umekua haupo baina ya wanandoa.
 
Kwenye kuchepuka siungi mkono to be honesty
Lakini kwenye kuwa na mahusiano halali naunga mkono
Haiwezekani kibabu cha miaka 80 kioe binti wa miaka 27 kwa jamii iwe halali
Lakini sisi watoto wa kiume tukitoka na wamama saizi ya mama zetu iwe issue
Thats not fair

NB: Mimi nikipata jimama likanipenda na nikalipenda aaah sisikilizi watu wanasema nini mimi nagidua tuu YOLO
 
Kwenye kuchepuka siungi mkono to be honesty
Lakini kwenye kuwa na mahusiano halali naunga mkono
Haiwezekani kibabu cha miaka 80 kioe binti wa miaka 27 kwa jamii iwe halali
Lakini sisi watoto wa kiume tukitoka na wamama saizi ya mama zetu iwe issue
Thats not fair

NB: Mimi nikipata jimama likanipenda na nikalipenda aaah sisikilizi watu wanasema nini mimi nagidua tuu YOLO

nikishakumbuka YOLO huwa nafanya ninachojisikia nani atanisema kama sivunji sheria ?
 
Na nyie wanaume c muoe wanawake saizi yenu hata ukiwa na iyo sukar ata stay,mnaoa wadada huku upo 60's
 
Kwenye kuchepuka siungi mkono to be honesty
Lakini kwenye kuwa na mahusiano halali naunga mkono
Haiwezekani kibabu cha miaka 80 kioe binti wa miaka 27 kwa jamii iwe halali
Lakini sisi watoto wa kiume tukitoka na wamama saizi ya mama zetu iwe issue
Thats not fair

NB: Mimi nikipata jimama likanipenda na nikalipenda aaah sisikilizi watu wanasema nini mimi nagidua tuu YOLO

Huhuhuhuiuuuuuu ati YOLO??? Ni shida
 
Kwenye kuchepuka siungi mkono to be honesty
Lakini kwenye kuwa na mahusiano halali naunga mkono
Haiwezekani kibabu cha miaka 80 kioe binti wa miaka 27 kwa jamii iwe halali
Lakini sisi watoto wa kiume tukitoka na wamama saizi ya mama zetu iwe issue
Thats not fair

NB: Mimi nikipata jimama likanipenda na nikalipenda aaah sisikilizi watu wanasema nini mimi nagidua tuu YOLO

Ukiona unaelekea huko, jiandae kuimbiwa.....Niagieni niagieni. Au kupunguza akiba ya ARV .....au kusemewa maneno .....sisi tulikupenda lakini muda c mrefu Mungu atakupenda zaidi..........Wengi wa hao ingawa sio wote kutokana na uchepukaji wa waliokuwa waume zao au wao wenyewe, afya huwa ni mgogoro.
 
Ukiona unaelekea huko, jiandae kuimbiwa.....Niagieni niagieni. Au kupunguza akiba ya ARV .....au kusemewa maneno .....sisi tulikupenda lakini muda c mrefu Mungu atakupenda zaidi..........Wengi wa hao ingawa sio wote kutokana na uchepukaji wa waliokuwa waume zao au wao wenyewe, afya huwa ni mgogoro.

Ila wazee wa kiume wao always wanakuwa fiti kiafya .........
 
Ila wazee wa kiume wao always wanakuwa fiti kiafya .........

Kama anaoa Binti ina maana wataenda kupima kwanza kabla ya kufunga ndoa, lakini kama anachepuka naye tu nyimbo kama hizo za kwako zinamsubiri huyo Binti. Na ieleweke kuwa Binti wa miaka 20 - 30 anapoolewa na Mzee wa miaka 60, tayari ni mjane matarajiwa kwa sababu umri wa kuishi mwanaume wa Kitanzania ni miaka 54.
 
Kama anaoa Binti ina maana wataenda kupima kwanza kabla ya kufunga ndoa, lakini kama anachepuka naye tu nyimbo kama hizo za kwako zinamsubiri huyo Binti. Na ieleweke kuwa Binti wa miaka 20 - 30 anapoolewa na Mzee wa miaka 60, tayari ni mjane matarajiwa kwa sababu umri wa kuishi mwanaume wa Kitanzania ni miaka 54.

Bora niwe mjane mdg mwenye pesa atiiiiiiii!!!!!!
 
Kama anaoa Binti ina maana wataenda kupima kwanza kabla ya kufunga ndoa, lakini kama anachepuka naye tu nyimbo kama hizo za kwako zinamsubiri huyo Binti. Na ieleweke kuwa Binti wa miaka 20 - 30 anapoolewa na Mzee wa miaka 60, tayari ni mjane matarajiwa kwa sababu umri wa kuishi mwanaume wa Kitanzania ni miaka 54.

Kwa hiyo sisi wa kiume kwenye akili yako unaona hatuwezi kwenda kupima ila vizee ndo vina kumbu kumbu ya kwenda kupima acha kugeneralize mambo mkuu
 
ivi unaatambua suala la tabia ni ngumu sana

kwann mtu achepuke na serengti boy alafu amlaumu mumewe hafikishi???
dhana ya uvumilivu kwenye ndoa/mausiano ni shida
wtu wanatenda makosa afu wannasema wenza wao ndo tatizo.
 
Back
Top Bottom