Je, Tanzania tupo katika hatua gani kiuchumi?

Alexander The Great

JF-Expert Member
Aug 28, 2018
4,502
23,581
Habari ndugu wana Jamii Intelligence,

Katika kupitia pitia vitabu vyangu siku ya jana, nikapitia kitabu cha mwanafalsafa mmoja aitwae "Walt Whitman Rostow" (Rostow's Stages Of Economic Growth, 1960 - Hatua za ukuaji kiuchumi za Rostow).

Kwa wanavyuoni waliosomea maswala ya Uchumi, Sheria, Biashara (baadhi ya Course), na Public Administration Course mtakua mmempitia huyu bwana na wengine wengi tu.

Kilichonivutia zaidi kuandika thread hii, ni kutokana na taarifa/habari nzuri tunazopata hivi sasa kuhusiana na ukuaji wa uchumi katika nchi yetu Tanzania, nikasema niwaletee ili tujadili uwiano na uhalisia wa principles (kanuni) na stages (hatua) za wafalsafa na wanavyuoni wa uchumi.

Pia wanajografia (Geographers) jinsi wanavyoweka matabaka ya nchi kimaendeleo na uchumi, wakiyapa matabaka kama vile; Nchi zilizo endelea (Developed Countries), Nchi zilizo katika hatua ya kuendelea (Developing Countries), Nchi za dunia ya kwanza (First World Countries - Yani nchi zilizo endelea), Nchi za dunia ya tatu (Third World Countries - Nchi zisizoendelea).

Wanatuachia maswali magumu sana kujibu, nini maana ya kuendelea kwa nchi? Na kwanini nchi nyingine zimeendelea na nyingine hazija endelea? (Hapa tutabishana sana na kila mmoja atatoa jibu lake).


Nirudi katika hoja ya msingi,

NB: AFDB imeripoti ya kua Tanzania inaukuaji wa uchumi kwa asilimia 6.7% kwa mwaka 2018.

Tuangalie katika uhalisia wa uchumi Tanzania, pamoja na uwiano wa wanafalsafa wa uchumi. (Tukimuangalia bwana Rostow).

Bwana "Walt Whitman Rostow" ni miongoni mwa wanafalsafa bingwa wa uchumi, na ameandika mambo mengi kuhusiana na hatua za kukua kwa uchumi. Miongoni mwa hayo maandiko ni yale ya mwaka 1960, nlioandika hapo juu (Rostow's Stages Of Economic Growth).
Hatua za ukuaji wa uchumi katika nchi, alizotaja mwanafalsafa huyu ni 5, kama zifuatazo;

1) Jamii za kale/jadi (Traditional Society Stage).

Hii hatua inatafsiriwa uchumi wa kujikimu kwa kutegemea kilimo, uwindaji, ufugaji na ukusanyaji wa mambo muhimu kwa matumizi ya watu. Kazi ngumu sana na biashara (trade) kua katika hali ya chini. Watu kutokujali maswala ya teknolojia ya kidunia (limited technology). Hakuna utulivu wa wananchi na wala system ya kisiasa (No centralized nation or political systems).

NB Hapa ndio taifa linaanza hatua ya kwanza katika ukuaji kiuchumi na kuingia ya pili.


2) Sharti La Awali La Kuondoka (Precondition To Take Off Stage).

Mahitaji ya mali ghafi kwa kina, kilimo cha biashara kwajili ya mauzo ya nafaka nje ya nchi (agriculture for export purpose), utengenezaji wa bidhaa muhimu, ukuaji wa kibiashara na ubadilikaji wa mazingira ya kuishi, utambulishwaji wa kitaifa na vitambulisho, ukuaji wa teknolojia na uhamasishaji wa ufumbuzi wa kiteknolojia.

3) Kuondoka (Take Off Stage).

Bwana Rostow ameelezea kua hii hatua ni ya muda mfupi sana na ukuaji ni waharaka sana (short period intensive growth). Hapa watu hushawishika sana katika kuwekeza kwenye sekta ya viwanda kwa kasi, na mtazamo wao ni kwenye viwanda.
300px-Table_for_take-off.jpg


4) Uendeshaji kuelekea kwenye Ukomavu (Drive to Maturity Stage).

Hatua hii huchukua muda mrefu, watu hubadilika kutoka katika kuwekeza kwenye biashara zenye faida kubwa/biashara zilizo katika uhitaji wa hali ya juu (Investment Driven Profit Goods) na kuwekeza katika viwanda/biashara nyingi na tofauti tofauti. Uanzishaji wa biashara/viwanda ni wa haraka kwa watu. Shule, hospitali, vyuo na maswala muhimu ya kijamii sio tatizo tena.
300px-Table_for_drive_to_maturity.jpg


5) Umri Wa Matumizi ya Hali Ya Juu (Age of Mass Consumption).

Hapa viwanda ndio vinashikilia uchumi wa nchi, na si wananchi wa kima cha chini kutegemewa kukamata uchumi/kodi ya nchi. Viwanda vya magari (automobiles) na matumizi ya magari ni muhimu kwa kila mtu, vifaa vya bei za juu kutengenezwa kwa urahisi na wingi (viwanda kama vya simu za mkononi, television n.k). Vijiji hugeuka miji na watu hukimbilia kwenye miji mikubwa.

Baada ya hatua hio, wananchi hujikuta wakiishi katika nchi yenye utulivu wa kiuchumi, amani, usalama wa biashara zao na uongozi bora. Na kutegemea uvumbuzi wa vifaa/mambo/viwanda/upelelezi wa kisayansi wa miaka ya mbeleni badala ya hapo waliopo. (Future Researches). - BEYOND CONSUMPTION.

Mwana falsafa huyu alielezea nia na madhumuni ya kuandika hizi hatua, ili kusaidia taifa kujua ni mambo gani yanapaswa kuzingatiwa na hatua zipi kuchukuliwa ili kushawishi ukuaji wa uchumi.

Mfano,

Nchi ya Singapore, ipo mashariki mwa bara la Asia, taifa hili lilipata uhuru mwaka 1965, na lilitumia njia hizi kujikwamua kutoka katika hali duni ya kiuchumi mpaka kukua kiuchumi kufikia hatua ya kua miongoni mwa mataifa yenye uchumi imara na mataifa yanayo chochea uchumi wa dunia. Sasa ni miongoni mwa mataifa yalioendelea ki miji mikubwa na yenye kipato kikubwa kwa mtu kushinda hata baadhi ya nchi za ulaya (Higher Per-Capita Income).
tumblr_inline_p7ge91yfJI1s7lryg_540.jpg
marina_sands_view_of_singapore_by_furiousxr-d4r5nhv.jpg




Kwa mtazamo wa sisi raia tunaoishi ndani ya taifa letu, tunafanya kazi, tunasoma kusoma, na kufanya biashara.

1) Je, tupo katika hatua gani sasa ya kiuchumi?

2) Je, Tanzania tunachukua hatua gani kukuza uchumi wa nchi yetu?

3) Na hizo hatua tuazochukua, zinachochea ukuaji wa uchumi kwa kasi kama tunavyotarajia na kuona katika report?

4) Vikwazo gani unahisi vinazuia ukuaji wa uchumi nchini? (Mfano labda kodi, sheria si rafiki kwa biashara na uanzishaji wa viwanda n.k).

5) Mahusiano ya Tanzania na mataifa ya nje, yana akisi ukuwaji wa uchumi kwa taifa letu?

6) Utawala wetu una mikakati na mipango gani kukuza uchumi kwa sera na utendaji uliopo?


Pamoja tujenge taifa letu,
 
Habari ndugu wana Jamii Intelligence,

Katika kupitia pitia vitabu vyangu siku ya jana, nikapitia kitabu cha mwanafalsafa mmoja aitwae "Walt Whitman Rostow" (Rostow's Stages Of Economic Growth, 1960 - Hatua za ukuaji kiuchumi za Rostow).

Kwa wanavyuoni waliosomea maswala ya Uchumi, Sheria, Biashara (baadhi ya Course), na Public Administration Course mtakua mmempitia huyu bwana na wengine wengi tu.

Kilichonivutia zaidi kuandika thread hii, ni kutokana na taarifa/habari nzuri tunazopata hivi sasa kuhusiana na ukuaji wa uchumi katika nchi yetu Tanzania, nikasema niwaletee ili tujadili uwiano na uhalisia wa principles (kanuni) na stages (hatua) za wafalsafa na wanavyuoni wa uchumi.

Pia wanajografia (Geographers) jinsi wanavyoweka matabaka ya nchi kimaendeleo na uchumi, wakiyapa matabaka kama vile; Nchi zilizo endelea (Developed Countries), Nchi zilizo katika hatua ya kuendelea (Developing Countries), Nchi za dunia ya kwanza (First World Countries - Yani nchi zilizo endelea), Nchi za dunia ya tatu (Third World Countries - Nchi zisizoendelea).

Wanatuachia maswali magumu sana kujibu, nini maana ya kuendelea kwa nchi? Na kwanini nchi nyingine zimeendelea na nyingine hazija endelea? (Hapa tutabishana sana na kila mmoja atatoa jibu lake).


Nirudi katika hoja ya msingi,

NB: AFDB imeripoti ya kua Tanzania inaukuaji wa uchumi kwa asilimia 6.7% kwa mwaka 2018.

Tuangalie katika uhalisia wa uchumi Tanzania, pamoja na uwiano wa wanafalsafa wa uchumi. (Tukimuangalia bwana Rostow).

Bwana "Walt Whitman Rostow" ni miongoni mwa wanafalsafa bingwa wa uchumi, na ameandika mambo mengi kuhusiana na hatua za kukua kwa uchumi. Miongoni mwa hayo maandiko ni yale ya mwaka 1960, nlioandika hapo juu (Rostow's Stages Of Economic Growth).
Hatua za ukuaji wa uchumi katika nchi, alizotaja mwanafalsafa huyu ni 5, kama zifuatazo;

1) Jamii za kale/jadi (Traditional Society Stage).
Hii hatua inatafsiriwa uchumi wa kujikimu kwa kutegemea kilimo, uwindaji, ufugaji na ukusanyaji wa mambo muhimu kwa matumizi ya watu. Kazi ngumu sana na biashara (trade) kua katika hali ya chini. Watu kutokujali maswala ya teknolojia ya kidunia (limited technology). Hakuna utulivu wa wananchi na wala system ya kisiasa (No centralized nation or political systems).

NB Hapa ndio taifa linaanza hatua ya kwanza katika ukuaji kiuchumi na kuingia ya pili.


2) Sharti La Awali - Kuondoka (Precondition To Take Off Stage).
Mahitaji ya mali ghafi kwa kina, kilimo cha biashara kwajili ya mauzo ya nafaka nje ya nchi (agriculture for export purpose), utengenezaji wa bidhaa muhimu, ukuaji wa kibiashara na ubadilikaji wa mazingira ya kuishi, utambulishwaji wa kitaifa na vitambulisho, ukuaji wa teknolojia na uhamasishaji wa ufumbuzi wa kiteknolojia.

3) Kuondoka (Take Off Stage).
Bwana Rostow ameelezea kua hii hatua ni ya muda mfupi sana na ukuaji ni waharaka sana (short period intensive growth). Hapa watu hushawishika sana katika kuwekeza kwenye sekta ya viwanda kwa kasi, na mtazamo wao ni kwenye viwanda.View attachment 888028

4) Uendeshaji kuelekea kwenye Ukomavu (Drive to Maturity Stage).
Hatua hii huchukua muda mrefu, watu hubadilika kutoka katika kuwekeza kwenye biashara zenye faida kubwa/biashara zilizo katika uhitaji wa hali ya juu (Investment Driven Profit Goods) na kuwekeza katika viwanda/biashara nyingi na tofauti tofauti. Uanzishaji wa biashara/viwanda ni wa haraka kwa watu. Shule, hospitali, vyuo na maswala muhimu ya kijamii sio tatizo tena.View attachment 888029

5) Umri Wa Matumizi ya Hali Ya Juu (Age of Mass Consumption).
Hapa viwanda ndio vinashikilia uchumi wa nchi, na si wananchi wa kima cha chini kutegemewa kukamata uchumi/kodi ya nchi. Viwanda vya magari (automobiles) na matumizi ya magari ni muhimu kwa kila mtu, vifaa vya bei za juu kutengenezwa kwa urahisi na wingi (viwanda kama vya simu za mkononi, television n.k). Vijiji hugeuka miji na watu hukimbilia kwenye miji mikubwa.

Baada ya hatua hio, wananchi hujikuta wakiishi katika nchi yenye utulivu wa kiuchumi, amani, usalama wa biashara zao na uongozi bora. Na kutegemea uvumbuzi wa vifaa/mambo/viwanda/upelelezi wa kisayansi wa miaka ya mbeleni badala ya hapo waliopo. (Future Researches). - BEYOND CONSUMPTION.

Mwana falsafa huyu alielezea nia na madhumuni ya kuandika hizi hatua, ili kusaidia taifa kujua ni mambo gani yanapaswa kuzingatiwa na hatua zipi kuchukuliwa ili kushawishi ukuaji wa uchumi.

Mfano,

Nchi ya Singapore, ipo mashariki mwa bara la Asia, taifa hili lilipata uhuru mwaka 1965, na lilitumia njia hizi kujikwamua kutoka katika hali duni ya kiuchumi mpaka kukua kiuchumi kufikia hatua ya kua miongoni mwa mataifa yenye uchumi imara na mataifa yanayo chochea uchumi wa dunia. Sasa ni miongoni mwa mataifa yalioendelea ki miji mikubwa na yenye kipato kikubwa kwa mtu kushinda hata baadhi ya nchi za ulaya (Higher Per-Capita Income).View attachment 888030View attachment 888031



Kwa mtazamo wa sisi raia tunaoishi ndani ya taifa letu, tunafanya kazi, tunasoma kusoma, na kufanya biashara.

1) Je, tupo katika hatua gani sasa ya kiuchumi?

2) Je, Tanzania tunachukua hatua gani kukuza uchumi wa nchi yetu?

3) Na hizo hatua tuazochukua, zinachochea ukuaji wa uchumi kwa kasi kama tunavyotarajia na kuona katika report?

4) Vikwazo gani unahisi vinazuia ukuaji wa uchumi nchini? (Mfano labda kodi, sheria si rafiki kwa biashara na uanzishaji wa viwanda n.k)


Pamoja tujenge taifa letu,
Zitto

Pascal Mayalla Kanungila Karim lucas mobutu Frank Wanjiru Zero IQ Sky Eclat GENTAMYCINE
Mkuu sizani kuendelea kwetu eti mpaka tupitia izoo hatua,mfano taifa limevunjika na kutengeneza nchi mbili na zaidi.Soo nchi hizoo hazna ulazma wa kupitia hizo hatua kama the traditional society.
Nazani utakuwa umenipata kwani kuna moja ya theory of underdevelopment ndani ya Development studies inasema kuwa"The source of underdevelopment in Africa(TZ) is to depend on developed countries (UK).
Kwa hiyo basi maendeleo yetu si lazma eti yapitie hatua ambazo wao wameona kwa macho yao no sahihi.
 
Mkuu sizani kuendelea kwetu eti mpaka tupitia izoo hatua,mfano taifa limevunjika na kutengeneza nchi mbili na zaidi.Soo nchi hizoo hazna ulazma wa kupitia hizo hatua kama the traditional society.
Nazani utakuwa umenipata kwani kuna moja ya theory of underdevelopment ndani ya Development studies inasema kuwa"The source of underdevelopment in Africa(TZ) is to depend on developed countries (UK).
Kwa hiyo basi maendeleo yetu si lazma eti yapitie hatua ambazo wao wameona kwa macho yao no sahihi.
Nimekuelewa point yako mkuu, na hii "he source of underdevelopement in Africa depends on the developed countries" theory ni sahihi kwa 100%. Nakubaliana na wewe.

Impacts za misaada toka mataifa yalioendelea tunazopata tunaya shuhudia kwa macho, ila sidhani kamaa tunaiifundisha lolote. Kwa mfano wa nchi ya zambia impact walizopata toka mikopo ya uchina, madhara yake wanazidi kunyonywa zaidi, Zesco (kampuni ya umeme ya zambia) imeshahukuliwa na China kwa kuvunja makubaliano ya mkopo, airport ya zambia imechachukuliwa na uchina kwa tatizo hilo hilo, pia television za taifa la zambia zimechukuliwa kwa 60% na uchina.

Hizi principle alizoandika Roatow, ni hatua ambazo nchi kama nchi ni lazima ipitie kama itataka kusimama kiuchumi yenyewe bila misaada kutoka taifa jingine (misaada nikimaaanisha mikopo ya riba n.k). Na mfano mzuri ni hio nchi ya singapore hapo.

Nia na madhumuni ya kuweka hoja zangu, ni kuliangalia Taifa letu kama tupo kwenye stage kati ya hizo, ukiziangalia kwa makini zina mantiki, sikua na nia tubishane mapungufu ya theory za bwana Rostow. (Natumai imenielewa)
 
Habari ndugu wana Jamii Intelligence,

Katika kupitia pitia vitabu vyangu siku ya jana, nikapitia kitabu cha mwanafalsafa mmoja aitwae "Walt Whitman Rostow" (Rostow's Stages Of Economic Growth, 1960 - Hatua za ukuaji kiuchumi za Rostow).

Kwa wanavyuoni waliosomea maswala ya Uchumi, Sheria, Biashara (baadhi ya Course), na Public Administration Course mtakua mmempitia huyu bwana na wengine wengi tu.

Kilichonivutia zaidi kuandika thread hii, ni kutokana na taarifa/habari nzuri tunazopata hivi sasa kuhusiana na ukuaji wa uchumi katika nchi yetu Tanzania, nikasema niwaletee ili tujadili uwiano na uhalisia wa principles (kanuni) na stages (hatua) za wafalsafa na wanavyuoni wa uchumi.

Pia wanajografia (Geographers) jinsi wanavyoweka matabaka ya nchi kimaendeleo na uchumi, wakiyapa matabaka kama vile; Nchi zilizo endelea (Developed Countries), Nchi zilizo katika hatua ya kuendelea (Developing Countries), Nchi za dunia ya kwanza (First World Countries - Yani nchi zilizo endelea), Nchi za dunia ya tatu (Third World Countries - Nchi zisizoendelea).

Wanatuachia maswali magumu sana kujibu, nini maana ya kuendelea kwa nchi? Na kwanini nchi nyingine zimeendelea na nyingine hazija endelea? (Hapa tutabishana sana na kila mmoja atatoa jibu lake).


Nirudi katika hoja ya msingi,

NB: AFDB imeripoti ya kua Tanzania inaukuaji wa uchumi kwa asilimia 6.7% kwa mwaka 2018.

Tuangalie katika uhalisia wa uchumi Tanzania, pamoja na uwiano wa wanafalsafa wa uchumi. (Tukimuangalia bwana Rostow).

Bwana "Walt Whitman Rostow" ni miongoni mwa wanafalsafa bingwa wa uchumi, na ameandika mambo mengi kuhusiana na hatua za kukua kwa uchumi. Miongoni mwa hayo maandiko ni yale ya mwaka 1960, nlioandika hapo juu (Rostow's Stages Of Economic Growth).
Hatua za ukuaji wa uchumi katika nchi, alizotaja mwanafalsafa huyu ni 5, kama zifuatazo;

1) Jamii za kale/jadi (Traditional Society Stage).
Hii hatua inatafsiriwa uchumi wa kujikimu kwa kutegemea kilimo, uwindaji, ufugaji na ukusanyaji wa mambo muhimu kwa matumizi ya watu. Kazi ngumu sana na biashara (trade) kua katika hali ya chini. Watu kutokujali maswala ya teknolojia ya kidunia (limited technology). Hakuna utulivu wa wananchi na wala system ya kisiasa (No centralized nation or political systems).

NB Hapa ndio taifa linaanza hatua ya kwanza katika ukuaji kiuchumi na kuingia ya pili.


2) Sharti La Awali - Kuondoka (Precondition To Take Off Stage).
Mahitaji ya mali ghafi kwa kina, kilimo cha biashara kwajili ya mauzo ya nafaka nje ya nchi (agriculture for export purpose), utengenezaji wa bidhaa muhimu, ukuaji wa kibiashara na ubadilikaji wa mazingira ya kuishi, utambulishwaji wa kitaifa na vitambulisho, ukuaji wa teknolojia na uhamasishaji wa ufumbuzi wa kiteknolojia.

3) Kuondoka (Take Off Stage).
Bwana Rostow ameelezea kua hii hatua ni ya muda mfupi sana na ukuaji ni waharaka sana (short period intensive growth). Hapa watu hushawishika sana katika kuwekeza kwenye sekta ya viwanda kwa kasi, na mtazamo wao ni kwenye viwanda.View attachment 888028

4) Uendeshaji kuelekea kwenye Ukomavu (Drive to Maturity Stage).
Hatua hii huchukua muda mrefu, watu hubadilika kutoka katika kuwekeza kwenye biashara zenye faida kubwa/biashara zilizo katika uhitaji wa hali ya juu (Investment Driven Profit Goods) na kuwekeza katika viwanda/biashara nyingi na tofauti tofauti. Uanzishaji wa biashara/viwanda ni wa haraka kwa watu. Shule, hospitali, vyuo na maswala muhimu ya kijamii sio tatizo tena.View attachment 888029

5) Umri Wa Matumizi ya Hali Ya Juu (Age of Mass Consumption).
Hapa viwanda ndio vinashikilia uchumi wa nchi, na si wananchi wa kima cha chini kutegemewa kukamata uchumi/kodi ya nchi. Viwanda vya magari (automobiles) na matumizi ya magari ni muhimu kwa kila mtu, vifaa vya bei za juu kutengenezwa kwa urahisi na wingi (viwanda kama vya simu za mkononi, television n.k). Vijiji hugeuka miji na watu hukimbilia kwenye miji mikubwa.

Baada ya hatua hio, wananchi hujikuta wakiishi katika nchi yenye utulivu wa kiuchumi, amani, usalama wa biashara zao na uongozi bora. Na kutegemea uvumbuzi wa vifaa/mambo/viwanda/upelelezi wa kisayansi wa miaka ya mbeleni badala ya hapo waliopo. (Future Researches). - BEYOND CONSUMPTION.

Mwana falsafa huyu alielezea nia na madhumuni ya kuandika hizi hatua, ili kusaidia taifa kujua ni mambo gani yanapaswa kuzingatiwa na hatua zipi kuchukuliwa ili kushawishi ukuaji wa uchumi.

Mfano,

Nchi ya Singapore, ipo mashariki mwa bara la Asia, taifa hili lilipata uhuru mwaka 1965, na lilitumia njia hizi kujikwamua kutoka katika hali duni ya kiuchumi mpaka kukua kiuchumi kufikia hatua ya kua miongoni mwa mataifa yenye uchumi imara na mataifa yanayo chochea uchumi wa dunia. Sasa ni miongoni mwa mataifa yalioendelea ki miji mikubwa na yenye kipato kikubwa kwa mtu kushinda hata baadhi ya nchi za ulaya (Higher Per-Capita Income).View attachment 888030View attachment 888031



Kwa mtazamo wa sisi raia tunaoishi ndani ya taifa letu, tunafanya kazi, tunasoma kusoma, na kufanya biashara.

1) Je, tupo katika hatua gani sasa ya kiuchumi?

2) Je, Tanzania tunachukua hatua gani kukuza uchumi wa nchi yetu?

3) Na hizo hatua tuazochukua, zinachochea ukuaji wa uchumi kwa kasi kama tunavyotarajia na kuona katika report?

4) Vikwazo gani unahisi vinazuia ukuaji wa uchumi nchini? (Mfano labda kodi, sheria si rafiki kwa biashara na uanzishaji wa viwanda n.k)


Pamoja tujenge taifa letu,
Zitto

Pascal Mayalla Kanungila Karim lucas mobutu Frank Wanjiru Zero IQ Sky Eclat GENTAMYCINE

Alexander the Great; unajitafutia depression isiyokuwa na sababu.
 
Mkuu sizani kuendelea kwetu eti mpaka tupitia izoo hatua,mfano taifa limevunjika na kutengeneza nchi mbili na zaidi.Soo nchi hizoo hazna ulazma wa kupitia hizo hatua kama the traditional society.
Nazani utakuwa umenipata kwani kuna moja ya theory of underdevelopment ndani ya Development studies inasema kuwa"The source of underdevelopment in Africa(TZ) is to depend on developed countries (UK).
Kwa hiyo basi maendeleo yetu si lazma eti yapitie hatua ambazo wao wameona kwa macho yao no sahihi.
Kingine Africa hatujashtuka bado, ya kua ulaya inatuvuruga ili tusifate stage hizo za maendeleo kama wao waliopitia kwa umakini (kwa mfano USA na UK walivopitia maswala ya INDUSTIALIZATION PERIOD n.k), sisi wanatufanya kuruka baadhi ya stage ili tukienda mbele then turudi nyuma mkuu. Wenzetu wamepitia kama zilivyo ukifanya research, sisi hatujafikia kipindi cha industrialization tusharukia kwengine kabisa.
 
Kingine Africa hatujashtuka bado, ya kua ulaya inatuvuruga ili tusifate stage hizo za maendeleo kama wao waliopitia kwa umakini (kwa mfano USA na UK walivopitia maswala ya INDUSTIALIZATION PERIOD n.k), sisi wanatufanya kuruka baadhi ya stage ili tukienda mbele then turudi nyuma mkuu. Wenzetu wamepitia kama zilivyo ukifanya research, sisi hatujafikia kipindi cha industrialization tusharukia kwengine kabisa.

Ndio maana nikakuambia unajitafutia depression isiyokuwa na sababu. Hivi ukiwa na nyumba ya kupangisha (na unahitaji elfu 50 kwa chumba kama kodi) lakini ukaamua kumuachia mtoto wako jukumu la kusimamia upangishaji na yeye akampangisha mtu chumba kwa elfu moja utamlaumu mpangaji?
Alietuzuia kufuata hizo stage ni nani? Naamini kuwa si lazima tufuate hizo stage, sasa anaetuzuia tusitafute mbadala wake ni nani? Hata kama yupo, ameshawahi kutushikia bunduki ili tufuate matakwa yake badala ya tunachokitaka? Nani ametulazimisha tukubaliane na mikataba isiyokuwa na manufaa kwetu? Ni nani alietulazimisha tuone kuwa kununua wabunge ili wahamie tupatakapo badala ya kununua dawa za kutibu watu ni nani?
Alietuambia tuteuwe watu "vichaa" kushika nafasi nyeti ni mzungu gani?
 
Tanzania karne ya 21 bado watu wanaona ni lazima mtoto apigwe viboko Shuleni ndo aweze kusoma na kuelewa, bila kuacha huu ukatili wa kupiga watoto usitegemee kuwa na kizazi ambacho kinaweza kufikiria straight, kwa kifupi > 85% ya Watanzania wana mental illness /inferiority complexes kwa sababu ya kulelewa kwa Ukatili na Wazazi, Walezi au Walimu, ongea na Mtanzania wa kawaida mwambie akuangalie machoni kama anaweza, hawezi kwa maana hajiamini!


Uanategemea huyu mtoto aje kuwa productive human being ambaye anaweza kufikiri na kufanya kazi kwa umakini kama analelewa na kukuzwa na ukatili kama huu?
1538907944111.png


vs Binadamu wengine

1538907990155.png
 
Tanzania karne ya 21 bado watu wanaona ni lazima mtoto apigwe viboko Shuleni ndo aweze kusoma na kuelewa, bila kuacha huu ukatili wa kupiga watoto usitegemee kuwa na kizazi ambacho kinaweza kufikiria straight, kwa kifupi > 85% ya Watanzania wana mental illness /inferiority complexes kwa sababu ya kulelewa kwa Ukatili na Wazazi, Walezi au Walimu, ongea na Mtanzania wa kawaida mwambie akuangalie machoni kama anaweza, hawezi kwa maana hajiamini!


Uanategemea huyu mtoto aje kuwa productive human being ambaye anaweza kufikiri na kufanya kazi kwa umakini kama analelewa na kukuzwa na ukatili kama huu?
View attachment 889450

vs Binadamu wengine

View attachment 889452
Point nzuri sana mkuu, 100%
 
Mjadala mzuri sana, ila naamini tunahitaji mental reformation in AFRICA, mental independence, decision making reformation, to archieve what we want else,
 
Back
Top Bottom