Je, Tanzania tuna Media Freedom kubwa kuliko UK na US? Tushuhudie kitachompata Julian Assange wa WikiLeaks! Tujifunze kwake

Wanabodi,

Yule Mwandishi Julian Asange wa WikiLeaks, ametiwa nguvuni nchini Uingereza kwa kutakiwa na Marekani, sasa sisi Tanzania, tujifunze kwa kitachompata, tukitumie kujifanyia tathmini ya Press Freedom yetu, usikute sisi tuna press freedom kubwa kuliko UK na US, zaidi ya magazeti kufungiwa na vituo vya TV kutozwa faini, kwa hivi karibuni sijawahi kusikia Mwandishi wa habari wa Tanzania kukamatwa na kushitakiwa kwa alichoandika, ukiondoa enzi zile za Adam Mwaibabile "Mwana".

Media za Tanzania tuna kilio kikubwa cha kulakamikia kuminywa au kunyimwa uhuru, "freedom of the press", na wananchi wetu wanakosa haki ya kupata habari, "the right to information" mfano kuyajua mahela ya vote 20 ambayo kila Ripoti ya CAG ikiibuka, inaibuka nayo, na kila siku tunawaangalia waandishi wa nchi za wenzetu haswa UK na US kuwa wako huru zaidi.

Baada ya Asange kudakwa, Marekani inaitaka Uingereza iwakabidhi Asange ili wao ndio washughulike nae, somo kubwa la kujifunza hapa ni kufuatilia kwa makini, nini kitamkuta Asange, jee Uingereza itamkabidhi kwa Marekani washungulike nae au itamkingia kifua katika kulinda na kutetea uhuru wa habari?.

Kwa upande wa sisi media ya Tanzania, tunalalamika kuwa hatuko huru wakati waandishi wenyewe wa type ya Asange, wa kuibua ma vitu kama Stan Katabalo, hatuna!, sisi wengi wa waandishi wetu, tunakalia kuandika habari za mikutano, warsha, seminar, na makongamano na kuzikunja zile brown ..., badala ya kuandika investigative stories, sasa uhuru wa habari tunaoutafuta ni uhuru gani?.

Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, ya matumizi mabaya ya fedha za umma, tungekuwa na serious media, by now, tungeishajua for sure ile 1.5B ilikwenda wapi na imefanyia nini!, au hata kujua tuu hizi fedha zinazochotwa kila siku hazina bila idhini ya Bunge na kutumbukizwa kwenye Vote 20, mule huwa zinakwenda kufanyia nini?. Inamaana hiyo Vote 20, wao hawana mpango kazi, kila siku wanafanya kazi kwa zimamoto, then serious media ingeonyesha basi hata huo moto uliozimwa isije kuwa ni mchwa tuu anatafunia Vote 20?.

Kama UK inayojitapa kwa Press Freedom sasa inamshikilia Asange, sisi kwetu kuna Mwandishi gani amewahi kushikiliwa kwa maandishi yake ukiondoa kifo cha Daudi Mwangosi, na kupotea kwa Azory Gwanda na Ben Saanane wetu humu jf, jee kuna Mwandishi gani au media gani inaripoti investigative stories za kuhalalisha kutaka uhuru zaidi?.

Somo la kukamatwa kwa Asange kutupe funzo usikute sisi Tanzania tuna press freedom kubwa kuliko ya UK na US ila tumekosa waandishi wa kuitumia hii freedom kikamilifu.

Jumamosi Njema
Paskali




Mimi nafikiri kwenye ishu Asange,kuna Mengi kuliko yanayotufikia machoni,
Hivi kweli,unavujishiwa siri za jeshi uwanja wa vita,ambazo katika zikiwekwa wazi,zinaweza kuweka usalama wa nchi pabaya,unaweza kuleta mgogoro wa kidiplomasia kati ya nchi na nchi,
Huyu jamaa,pamoja na Edward Snowden,walivujisha mambo mabaya ambayo yanafanywa na taasisi za kiusalama,na kiinteligensia katika kuilinda USA.
Taarifa kama hizo ukiziweka wazi,wala usaidii wasomaji wako,unaweza kuiweka nchi nzima katika matatizo makubwa,kwa ufupi kuna vitu ambavyo havitakiwi kuwekwa hadharani,kama bajeti na manunuzi ya jeshi au idara ya usalama wa Taifa.
Mwandishi wa habari ukikurupuka ukazivujisha,inabidi yakukute makubwa.
Ubaya ni kwamba kwa huku kwetu Afrika,na TZ,wakubwa wanaweza wakakuambia huo mradi(kama meremeta) ni wa usalama wa Taifa,kumbe ni chaka LA kupiga pesa ya umma bila kuulizwa.huku kwetu uadirifu ni zero,wanakuambia wameua majambazi katika mapambano,kumbe watu wamekuwa executed,kisa wanaipinga serikali.
Na huko kwa wenzetu,Asange atakuwa na mawakili wake,uwezi kulinganisha na hapa bongo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Exactly!
Mkuu Paschal nimekuelewa Sana kwa hili hata mfano mzuri upo Kenya Wana waandishi wa habari za uchunguzi wazuri Sana.

Tatizo ninaloliona bongo Ni kukosekana kwa weledi pamoja na kutamalaki kwa rushwa katika media karibu 70%.

Kwa mfano kipindi Cha sekeseke la makonda kuwataja drug dealers nilishangaa Sana jinsi pesa chafu zilivyomwaga ili TU kuwasafisha wahusika na kumchafua makonda..badala waandishi wa habari wangeingia kufanya uchunguzi wa kina wao wakaanza kujifanya watetezi na kutunga stories nyingi nje ya kilichotarajiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo nadhani akili zangu zimegoma kuelewa.
BTW: Nachojua, Assange alikuwa ana-leak informations ambazo ni classified.
Hapa kwetu hata zile ambazo siyo classified hutakiwi kuziandika, mfano mdogo ni hii report ya CAG, leo hii Bunge linagoma kupublish vitabu vyote, website imekuwa shut down.
Wabunge wa chama tawala hawataki hata CAG atajwe na wabunge pinzani nk.
Uzuri wewe unayeandika haya uko kwenye Media.
Nina mtu ambaye yuko kwenye print media na ni gazeti ambalo liko very prominent, anakwambia kabla hamjaprint ni lazima font ferd itumwe kwa utawala ili wakuruhusu kuiprint, kila siku.
Naamini hilo la kutuma font ferd unalijua.
Alifanya kwa maslahi ya uma lakini. Nampongeza amefanya tukajua mengi juu ya ufwedhuli wa marekani na mataifa madhalimu ya kimagharibi. Kumkamata ni uonevu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,
Yule Mwandishi Julian Asange wa WikiLeaks, ametiwa nguvuni nchini Uingereza kwa kutakiwa na Marekani, sasa sisi Tanzania, tujifunze kwa kitachompata, tukitumie kujifanyia tathmini ya Press Freedom yetu, usikute sisi tuna press freedom kubwa kuliko UK na US, zaidi ya magazeti kufungiwa na vituo vya TV kutozwa faini, kwa hivi karibuni sijawahi kusikia Mwandishi wa habari wa Tanzania kukamatwa na kushitakiwa kwa alichoandika, ukiondoa enzi zile za Adam Mwaibabile "Mwana".
Media za Tanzania tuna kilio kikubwa cha kulakamikia kuminywa au kunyimwa uhuru, "freedom of the press", na wananchi wetu wanakosa haki ya kupata habari, "the right to information" mfano kuyajua mahela ya vote 20 ambayo kila Ripoti ya CAG ikiibuka, inaibuka nayo, na kila siku tunawaangalia waandishi wa nchi za wenzetu haswa UK na US kuwa wako huru zaidi.
Baada ya Asange kudakwa, Marekani inaitaka Uingereza iwakabidhi Asange ili wao ndio washughulike nae, somo kubwa la kujifunza hapa ni kufuatilia kwa makini, nini kitamkuta Asange, jee Uingereza itamkabidhi kwa Marekani washungulike nae au itamkingia kifua katika kulinda na kutetea uhuru wa habari?.
Kwa upande wa sisi media ya Tanzania, tunalalamika kuwa hatuko huru wakati waandishi wenyewe wa type ya Asange, wa kuibua ma vitu kama Stan Katabalo, hatuna!, sisi wengi wa waandishi wetu, tunakalia kuandika habari za mikutano, warsha, seminar, na makongamano na kuzikunja zile brown ..., badala ya kuandika investigative stories, sasa uhuru wa habari tunaoutafuta ni uhuru gani?.
Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, ya matumizi mabaya ya fedha za umma, tungekuwa na serious media, by now, tungeishajua for sure ile 1.5B ilikwenda wapi na imefanyia nini!, au hata kujua tuu hizi fedha zinazochotwa kila siku hazina bila idhini ya Bunge na kutumbukizwa kwenye Vote 20, mule huwa zinakwenda kufanyia nini?. Inamaana hiyo Vote 20, wao hawana mpango kazi, kila siku wanafanya kazi kwa zimamoto, then serious media ingeonyesha basi hata huo moto uliozimwa isije kuwa ni mchwa tuu anatafunia Vote 20?.
Kama UK inayojitapa kwa Press Freedom sasa inamshikilia Asange, sisi kwetu kuna Mwandishi gani amewahi kushikiliwa kwa maandishi yake ukiondoa kifo cha Daudi Mwangosi, na kupotea kwa Azory Gwanda na Ben Saanane wetu humu jf, jee kuna Mwandishi gani au media gani inaripoti investigative stories za kuhalalisha kutaka uhuru zaidi?.
Somo la kukamatwa kwa Asange kutupe funzo usikute sisi Tanzania tuna press freedom kubwa kuliko ya UK na US ila tumekosa waandishi wa kuitumia hii freedom kikamilifu.
Jumamosi Njema
Paskali
Asange alikuwa anaingilia mawasiliano ya vyombo vya ulinzi na usalama ili kupata hot news. Huyu bwana ni jasusi
 
Kuna point tatu za msingi za kukamatwa kwake, ambazo zingine zishatolewa ufafanuzi.

1. Tatizo sio habari yake, bali jinsi alivyozipata anadaiwa kashiriki ku-hack system ya CIA ili kupata hizo habari hilo ndio kosa lake

2. Ana kesi ya kubaka Sweden ambayo kaikimbia. UK kama mwanachama wa EU, bado alikuwa inside the same jurisdiction. Vyombo vya ulinzi ndani ya EU wanatakiwa kumkamata muhalifu ndani ya jumuiya na kumrudisha anapotakiwa. Alipokamatwa UK kwa hilo kosa na kupewa dhamana akakimbilia Ecuador embassy kwa ivyo ana breach of bail ndio maana alikabadhiwa kwao.

3. UK na US wana extradition treaty ni kawaida sana kukamatiana watu wanaowahitaji iwapo upande wa pili utathibitisha mahakamani ni kosa gani la kisheria za hiyo nchi alizovunja. Na mahakama ikiridhia kuna ushahidi wa kosa wakapewa huyo mtuhumiwa uwezi mshitaki kwa kosa lingine akifika huko.
 
Wanabodi,

Yule Mwandishi Julian Asange wa WikiLeaks, ametiwa nguvuni nchini Uingereza kwa kutakiwa na Marekani, sasa sisi Tanzania, tujifunze kwa kitachompata, tukitumie kujifanyia tathmini ya Press Freedom yetu, usikute sisi tuna press freedom kubwa kuliko UK na US, zaidi ya magazeti kufungiwa na vituo vya TV kutozwa faini, kwa hivi karibuni sijawahi kusikia Mwandishi wa habari wa Tanzania kukamatwa na kushitakiwa kwa alichoandika, ukiondoa enzi zile za Adam Mwaibabile "Mwana".

Media za Tanzania tuna kilio kikubwa cha kulakamikia kuminywa au kunyimwa uhuru, "freedom of the press", na wananchi wetu wanakosa haki ya kupata habari, "the right to information" mfano kuyajua mahela ya vote 20 ambayo kila Ripoti ya CAG ikiibuka, inaibuka nayo, na kila siku tunawaangalia waandishi wa nchi za wenzetu haswa UK na US kuwa wako huru zaidi.

Baada ya Asange kudakwa, Marekani inaitaka Uingereza iwakabidhi Asange ili wao ndio washughulike nae, somo kubwa la kujifunza hapa ni kufuatilia kwa makini, nini kitamkuta Asange, jee Uingereza itamkabidhi kwa Marekani washungulike nae au itamkingia kifua katika kulinda na kutetea uhuru wa habari?.

Kwa upande wa sisi media ya Tanzania, tunalalamika kuwa hatuko huru wakati waandishi wenyewe wa type ya Asange, wa kuibua ma vitu kama Stan Katabalo, hatuna!, sisi wengi wa waandishi wetu, tunakalia kuandika habari za mikutano, warsha, seminar, na makongamano na kuzikunja zile brown ..., badala ya kuandika investigative stories, sasa uhuru wa habari tunaoutafuta ni uhuru gani?.

Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, ya matumizi mabaya ya fedha za umma, tungekuwa na serious media, by now, tungeishajua for sure ile 1.5B ilikwenda wapi na imefanyia nini!, au hata kujua tuu hizi fedha zinazochotwa kila siku hazina bila idhini ya Bunge na kutumbukizwa kwenye Vote 20, mule huwa zinakwenda kufanyia nini?. Inamaana hiyo Vote 20, wao hawana mpango kazi, kila siku wanafanya kazi kwa zimamoto, then serious media ingeonyesha basi hata huo moto uliozimwa isije kuwa ni mchwa tuu anatafunia Vote 20?.

Kama UK inayojitapa kwa Press Freedom sasa inamshikilia Asange, sisi kwetu kuna Mwandishi gani amewahi kushikiliwa kwa maandishi yake ukiondoa kifo cha Daudi Mwangosi, na kupotea kwa Azory Gwanda na Ben Saanane wetu humu jf, jee kuna Mwandishi gani au media gani inaripoti investigative stories za kuhalalisha kutaka uhuru zaidi?.

Somo la kukamatwa kwa Asange kutupe funzo usikute sisi Tanzania tuna press freedom kubwa kuliko ya UK na US ila tumekosa waandishi wa kuitumia hii freedom kikamilifu.

Jumamosi Njema
Paskali




Mzee huwa mada zako zipo kisengele nyuma huwa najaribu kukuelewa ila nashindwa

Punguza kuandika magazeti yasiyo eleweka hapa jamvini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania hatuwazidi US na uingereza uhuru wa habari tu, bali hata Maendeleo tumewaacha mbali sana,
 
Leo nadhani akili zangu zimegoma kuelewa.
BTW: Nachojua, Assange alikuwa ana-leak informations ambazo ni classified.
Hapa kwetu hata zile ambazo siyo classified hutakiwi kuziandika, mfano mdogo ni hii report ya CAG, leo hii Bunge linagoma kupublish vitabu vyote, website imekuwa shut down.
Wabunge wa chama tawala hawataki hata CAG atajwe na wabunge pinzani nk.
Uzuri wewe unayeandika haya uko kwenye Media.
Nina mtu ambaye yuko kwenye print media na ni gazeti ambalo liko very prominent, anakwambia kabla hamjaprint ni lazima font ferd itumwe kwa utawala ili wakuruhusu kuiprint, kila siku.
Naamini hilo la kutuma font ferd unalijua.
Ndiyo Marekeni ilipofika kama bongo ama husomi habari? Sasa hivi tofauti ya Marekani na Bongo ni rangi za ngozi za rais na wabunge wa chama tawala. Hakuna tofauti kabisa. Huyo Asange katika Awamu ya Obama walizingatia katiba yao yaani 1st Ammendment ambayo haingalii umezipataje habari bali wanaangakia uhuru wa kutoa maoni yako. Sasa hivi wakati wa Donald Trump mambo yamebadilika DOJ wanamkingia kifua rais wanatetea mpaka maovu yake wakisaidiwa na Senate. Marekane Ifwirirwe vanyambara
 
Vitu vya kuandikwa viko vingi, tatizo hatuna competent media people to dig deep na kuviibua.
P
Mayalla kila siku hua nasema Tanzania hakuna waandishi wa habari bali wapo waandishi wa Udaku unadhani tangu lini waandishi wa udaku wanaweza kuwa investigative Journalists??? TV zinamilikiwa na watu kama kina Diamond na Joseph Kusaga wapiga debe wa uchaguzi wa rais leo hii unataka kuwe na documentary za kweli? Vijana wengi hapa hawataweza kufahamu kwamba wewe Mayalla ukiwa na Masai Studio ndiyo mlikua wa kwanza kuleta vichapo kwa viongozi na kipindi chako cha Kiti moto kupitia nadhani DTV na ndiyo maana hata mlipokuwa wa kwanza kuleta matokeo ya Uchaguzi wa Tanzzania visiwani mliwekwa PIN na wakubwa wako wakaingia mitini.

kama ungeweza kuwatafuta wale ma producer na researchers wako labda tungefika nusu ya Kenya. Pili Marehemu Lusekelo Adam pia alikufuata na kipindi cha malumbano ya Hoja yaliyokuwa yanarushwa na ITV. Baada ya kuendelea mbele uandishi wa habari na mabroadcaster manarudi nyuma kwenye ujima. Mnananunuliwa sana na wanasiasa habari zinakuwa kama magazeti yakufungia vitumbua tu hasa kama magazeti ya Musiba na Kubenea sijui kama tuyaite majarida ama vipeperushi
 
Ndiyo Marekeni ilipofika kama bongo ama husomi habari? Sasa hivi tofauti ya Marekani na Bongo ni rangi za ngozi za rais na wabunge wa chama tawala. Hakuna tofauti kabisa. Huyo Asange katika Awamu ya Obama walizingatia katiba yao yaani 1st Ammendment ambayo haingalii umezipataje habari bali wanaangakia uhuru wa kutoa maoni yako. Sasa hivi wakati wa Donald Trump mambo yamebadilika DOJ wanamkingia kifua rais wanatetea mpaka maovu yake wakisaidiwa na Senate. Marekane Ifwirirwe vanyambara

Marekani ipi?

CNN kila siku tunaona Trump anapondwa, vyombo vya sheria tunaona kesi dhidi ya Trump.

Wasanii wanatoa nyimbo za kumponda Trump na zinaingia kwenye mainstream.

Acheni hizo bana.
 
Marekani ipi?

CNN kila siku tunaona Trump anapondwa, vyombo vya sheria tunaona kesi dhidi ya Trump.

Wasanii wanatoa nyimbo za kumponda Trump na zinaingia kwenye mainstream.

Acheni hizo bana.
Unaona anavyowapiga vita? Kama rais wa nchi anahamasisha wahuni mpaka sasa waandishi wa habari kama April Ryan sasa anatembea na walinzi kuhofia maisha yake ndiyo unaona huo ni uhuru? mabomu mangapi yameteguliwa yakiwawinda wanahabari kwasababu ya Rais?? Usiamini sana unayaona wengine tunayaishi hayo Maisha hatuhitaji BBC ama CNN kuzianglia mkuu.

https://www.washingtonpost.com/news...ce-to-be-a-journalist/?utm_term=.90a77d4f80c9

soma hii habari
 
Nimeuliza jee Tanzania ni hatuna uhuru wa kuandika, au ni hatuna waandishi wa kuandika habari za uchunguzi?.

Ili kuhalalisha media tunatishwa media ziandike basi mambo mazito tuone serikali inaigopa. Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, media gani imekwenda deep, nakutolea mfano mdogo tuu wa Vote 20?

P

..Tafadhali Pascal Mayalla..tafadhali sana.

..wewe una heshima hapa JF.

..vijana wanakuamini ktk mabandiko yako.

..sasa siyo vizuri ukawapoteza namna hii.

..mgogoro wa Julian Asange unahusu KUDUKUA na kusambaza mawasiliano nyeti ya SEREKALI ya Marekani.

..ungewatendea haki vijana hawa wanaokuheshimu kama ungefafanua alichofanya Julian Asange, halafu ukalinganisha kama waTz tuna uhuru wa kufanya jambo linalokaribiana na alichofanya.

..au kwanini usituletee clip za MAHOJIANO kati ya VIONGOZI wa nchi za wenzetu na VYOMBO VYA HABARI halafu tuone kama na sisi tuko HURU na tuna WELEDI kiasi gani.
 
Hata Triump alipata emails za Hillary kupitia wikileaks

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli me naona Mayalla usifananishe issue ya Julian aisee Yale sio level ya Africa, kwavyovyote yule anatumia hackers kitu ambacho ni kosa la jinai. Kwa hacking tu unaweza kuiba hata Banks ndo maana kukawa na mifumo ya Security. Hizo habari anazo zisema mayala ni uchunguzi wa kuhoji sources lkn huwezi kuvunja na kufungua vilivyofungwa bila ruhusa ya wahusika huo ni ujambazi, ndo alipoangukia Julian.
 
Unaona anavyowapiga vita? Kama rais wa nchi anahamasisha wahuni mpaka sasa waandishi wa habari kama April Ryan sasa anatembea na walinzi kuhofia maisha yake ndiyo unaona huo ni uhuru? mabomu mangapi yameteguliwa yakiwawinda wanahabari kwasababu ya Rais?? Usiamini sana unayaona wengine tunayaishi hayo Maisha hatuhitaji BBC ama CNN kuzianglia mkuu.
https://www.washingtonpost.com/news...ce-to-be-a-journalist/?utm_term=.90a77d4f80c9
soma hii habari

Too bad, lakini angalau huko kwa kiasi kikubwa sheria zinawalinda.

Huku vyombo vya habari kufungiwa si jambo la ajabu.

Poleni mkuu, popote pale hakuna anayependa kusemwa vibaya.
 
Too bad, lakini angalau huko kwa kiasi kikubwa sheria zinawalinda.

Huku vyombo vya habari kufungiwa si jambo la ajabu.

Poleni mkuu, popote pale hakuna anayependa kusemwa vibaya.
Ni kweli kabisa kuna unafuu huwezi kulinganisha na huko nyumbani. Mimi nilishangaa kumsikia kamanda Muruto sijui mroto akisema ati waandamanaji wanapata kipigo sijajua wamepewa na nani mamlaka ya kupiga watu. Kama ingekua huku sidhani kama hiyo kazi angabaki nayo. Tatizo la Trump yeye ni bwenyenye aliyezoea kuwa CEO wa kampuni yake siyo mwanasiasa yupo kama jiwe anadhani kuwa rais kuwa anakua juu ya sheria mpaka ma judge anataka kuwamiliki.
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom