Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,397
- 3,884
Mkandara said:Wala hatuna haja ya kuweka mikwara sii wao wataanza kukata misaada. Wakikata misaada na kufunga balozi zao ina maana wawekezaji wote nchini wanakuwa hawana mdhamana wala sheria haipo tena. Hapo ndipo nasi tutalazimika kufuta mahusiano na kulamba dume kina Barrick..Mkuu hawawezi Sii umeona Marekani na Syria?.. wanashindwa nini kuingia pale wakashambulia kama sii kuogopa kuipoteza Iraq maana kule Mashia wote wataungana against America ndio maana wanatafuta mtu mwingine na Turkey seems to be the best bet!.. Mturuki naye chale zimemcheza...
JokaKuu,
Nimeichukua hiyo post ya Mkandara kwa sababu kwa kiasi kikubwa inashabihiana na uelewa wangu wa mambo haya dunia yanavyokwenda. Nilikuwa nahangaika kidogo juzi kuweka mawazo yangu sawa lakini hii post yake itanisaidia sana kuweza kujieleza kwa ufasaha kwa sababu naamini kabisa alichosema ni kweli, ingawa sina uhakika kama atakubaliana na mimi kwa nitakachosema. Itabidi nimsukumie hii post yangu ili nione anafikiria nini.
Kwa kuanzia ningependa kusema kwamba katika dunia ya sasa kuna pande mbili zinazopingana. Naamini wote mnajua hilo, ingawa wengi wanafikiri haya mambo yamekwisha toka miaka ya 80. Hii ni rahisi kujua, si tu kwa kuangalia siasa ya dunia inavyoendeshwa sasa, lakini hata uchumi.
Naamini wewe uelewa wako ni mpana zaidi kuliko baadhi ya watu, wengine ninaowaona humu, wanaodhani JK kauza nchi kwa t-shirts za kampeni na masuti. Ningependa kuamini hivyo la sivyo hii post yangu itakuwa kupoteza muda.
Nikiendelea, vita ya sasa kwa kiasi kikubwa ni muendelezo wa vita za miaka ya 60-70, tofauti kubwa ni kwamba China siyo tena nchi masikini, Afrika tuna kete zenye nguvu zaidi ya wakati ule ingawa wanajaribu kutupuuza kwa sababu tunafanya mlinganyo wa mbinu (strategic equation) za magharibi kuwa mgumu sana kwao, na kwamba siasa za ndani ya Marekani zinatumika kwa kiasi kikubwa katika mchezo huu mpana.
Kingine, ni kwamba siasa, uchumi na mambo mengine NJE ya marekani vinashawishi kwa kiasi kikubwa tabia, fikra na maamuzi ya wapiga kura wa marekani kwa sasa kuliko wakati mwingine wowote (nitalielezea hili kwa upana baadaye).
Nimewahi kukaa chini na kuzungumza na watu kadhaa wenye upeo tofauti kuhusu haya mambo. Zamani tulikuwa tunaishia kwenye malumbano na sababu kubwa ni kwamba 'mentality' ya watunga sera, hasa kuhusu mambo ya nje ni tofauti kabisa na, tuseme, watunga sheria, ukiacha hata watu wa kawaida.
Kujua sheria kwa kiasi kikubwa kunasaidia kuwa mtunga sera mzuri wa mambo ya nje kwa sababu unajifunza jinsi ya kuzivunja hizo sheria baadaye, na kwa kisi kikubwa hiyo ndiyo inakuwa kazi yako. Kwa kifupi, hivyo ndivyo sera ya mambo ya nje ya marekani inavyoendeshwa, na China inaelekea imenakili na kufanisi mbinu hiyo.
China haitumii mbinu hiyo kwenye mahusiano yao na nchi zinazoendelea (Africa, Caribbean, Latin America), na hata kwa majirani zake kwa sababu lengo lao ni moja. Kwa kifupi, nchi rafiki hazitumii mlengo huo baina yao. Kwa kusema hivyo, bila kuwepo kwa uhasama wa waziwazi, watu wanaweza kuangalia mambo madogo madogo (watalii, viongozi kutembeleana, misaada mbalimbali na hata mawasiliano kati ya jeshi na jeshi) katika uhusiano baina ya nchi mbili zilizo na ushindani wa siri na kudhani zina uhusiano mzuri.
Nchi zilizoweza kujenga mihimili ya sera zao sawasawa zina uwezo wa kuendesha sera 2-3 tofauti zisizoshabihiana kwa wakati mmoja bila sera hizo kugongana. Ndiyo maana naamini miaka ile walipotuchukua watumwa, na baadaye kujigawanyia Afrika, kwa kiasi kikubwa wananchi wa ndani wa nchi zile walikuwa hawajui military adventurism (zizimizi za kijeshi??) nchi zao zinazofanya nje ya nchi. Hata leo hii, mbinu hizo bado zinawezekana na zinaendelea, ingawa inakuwa ngumu sana kuzitekeleza kwa sababu ya vitu kama mtandao.
Kama umesoma hadi hapa, unaweza kuwa unajiuliza, haya yote ninayoongelea yanahusiana vipi na meli za mafuta za Iran kubeba bendera ya TZ. Naomba niendelee (niwie radhi, itanichukua posts kadhaa kuweza kuelezea yote ninayotaka kusema)........