Je,Tanga Tech school ni Special school?

WENYELE

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,415
1,378
Wakuu
Naomba kufahamishwa,Tanga Tech nayo ni shule maalum kama ilivyo Mzumbe,Ilboru au Tabora Boys?
Asante
 
Tanga Technical ni special school lakini si kama zilivyo hizo ulizotaja,yenyewe ina masomo ambayo hizo shule hazina na pia ukienda shule hii sahau somo la History kama upo O'level!mimi nimesoma hapo!
 
SIO ni shule ya ufundi, levels ziko hivi
1.Shule maalum (Tabora boys,mzumbe,kibaha ,Ilboru)
2.Shule za ufundi (Tanga tech,Musoma tech n.k)
3.Shule za bweni za kawaida (Sengerema,Nsumba ,Songea boys n.k)
4.Shule za kutwa Kongwe
5.Shule za kata
 
SIO ni shule ya ufundi, levels ziko hivi
1.Shule maalum (Tabora boys,mzumbe,kibaha ,Ilboru)
2.Shule za ufundi (Tanga tech,Musoma tech n.k)
3.Shule za bweni za kawaida (Sengerema,Nsumba ,Songea boys n.k)
4.Shule za kutwa Kongwe
5.Shule za kata
kuwa shule ya ufundi hicho ni kigezo kwamba hiyo ni special kwa masomo hayo ambayo shule nyingine hazitoi!labda ungeelezea u-special wa shule kama Mzumbe,Kibaha na Ilboru upo vipi kwa sababu masomo wanayosoma ni yale yale yanayotolewa na shule nyingine!
 
Usijifikirie mara mbili kwenda TTS(Tanga Technical School) nenda tu mkuu kama ni mwanao mpeleke hapo pako good sana na ni shule ya kwanza kabisa ya secondary ya serikali kwa Tanzania

VIVA KIUNGANI
 
hiyo shule iko vizuri sana Kuna bro wang alisomea hapo lkn hakuendelea advance
 
Laiti serikali yetu ingeboresha hizi Technical schools Leo hii tungekuwa mbali.

Shule Za ufundi kama Moshi Tech, Mbeya Tech, Musoma Tech to mention but few zingekuwa zimepiga hatua.

Mfano mzuri, unawezaona Arusha Tech Kwa sasa imekuwa Na hadhi kubwa Na inatoa degree Za ufundi. Hivyo , hata hizi zingine zingewezeshwa
 
Usijifikirie mara mbili kwenda TTS(Tanga Technical School) nenda tu mkuu kama ni mwanao mpeleke hapo pako good sana na ni shule ya kwanza kabisa ya secondary ya serikali kwa Tanzania

VIVA KIUNGANI
Mkuu wa matokeo yake jinsi yalivyo nilidhani angeenda Mzumbe and Co. Lakini amejikuta ameweka hapo,natamani asome PCM,PCB au CBG badaye maana ndio sehem pekee yakuweza kujiajiri badae
 
Mkuu wa matokeo yake jinsi yalivyo nilidhani angeenda Mzumbe and Co. Lakini amejikuta ameweka hapo,natamani asome PCM,PCB au CBG badaye maana ndio sehem pekee yakuweza kujiajiri badae
Tanga School ina PCB na PCM,CBG iliondolewa na sidhani kama imerudishwa!

Halafu kama ni O'level anaanza shule hiyo huwa wanaangalia zaidi ufaulu kwenye Hesabu na Sayansi!
Na akimaliza form four hata soma combination za Arts kwa sababu hakuna History hapo!
 
Special school is for specal talented student ,, ( kibaha, iliboru, mzumbe ,tabora boy, kisimiri , msalato na kilakala)
 
Mkuu wa matokeo yake jinsi yalivyo nilidhani angeenda Mzumbe and Co. Lakini amejikuta ameweka hapo,natamani asome PCM,PCB au CBG badaye maana ndio sehem pekee yakuweza kujiajiri badae
Siku hizi technical school ukimaliza form four una option ya kusoma comb hizi tu PCB na PCM kama ulichagua biology over geography na PCM, EGM, na PGM kama ulichagua geography over biology so haiwezekani kusoma CBG. Tanga school ni shule nzuri akijitahidi atafaulu ila masomo ya ufundi ni magumu na syllabus yake haipo vizuri.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom