mafutamingi
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 2,772
- 2,171
Ni dhahiri kwamba Tume Ya Uchaguzi iliyopo si tume huru kama misingi ya chaguzi za kidemokrasia inavyohitaji.
Mojawapo ya mapungufu ya tume yetu (NEC) ni kwamba watendaji wake wote wanachaguliwa na Rais ambaye pia
ni mmoja wapo wa wagombea. Watendaji hawa wanawajibika kwake na anaweza kuwaondoa wakati wowote ikitegemea
ameamkaje siku hiyo.
Hali hii inakihakikishia ushindi CCM na serikali haitakubali hata siku moja pawepo na Tume iliyo huru.
Mojawapo ya ushahidi kuwa tume si huru ni mambo yaliyojiri wakati wa kampeni za uchaguzi ambao unaofanyika leo. Ushahidi uko wazi jinsi ambavyo TBC ambayo ni taasisi ya serikali ilivyokuwa ikionyesha muda wote kampeni za mgombea urais wa CCM na kuvinyima vyama vya upinzani fursa hiyo.
Pia tume ilikataa kupokea malalamiko ya vyama vya upinzani kuhusu mgombea wa CCM pale alipoamuru Katibu Mkuu wa TAMISEMI apeleke pesa Hedaru za kujenga kituo cha Afya wakati huo huo kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi. Kwa kuwa wito wa kuwa na tume huru ya uchaguzi unagonga mwamba je ni wakati wa kuwepo shinikizo kutoka nje ili pawepo na Tume Huru ya Uchaguzi?
Ikumbukwe kwamba si jambo geni kwa sheria kadhaa kutungwa au kubadili sheria zilizopo hapa Tanzania kutokana na shinikizo kutoka nje.
Sote tunakumbuka jinsi ambavyo sheria ya kupambana na ugaidi ilivyopitishwa mwanzoni mwa miaka ya 2000 kutokana na shinikizo kutoka Marekani.
Tumeona jinsi ambavyo watanzania walishiriki katika tukio hilo ambalo limefanyika hapa wakipelekwa marekani ili wakakabiliane na mashtaka huko.
Hata hivi majuzi Rais alipopitisha Executive Order ya kuzuia wasichana wanaopata mimba wakiwa shuleni waisruhusiwe kendelea na masomo baadaya kujifungua, agizo hilo liliondolewa kutokana na shinikizo kutoka nje. Hata sheria ya makosa ya mtandao na sheria ya takwimu ilipunguzwa makali kutokana na shinikizo kutoka nje.
Je, wakati umefika kwa wale wanaotaka Tume Huru ya Uchaguzi kutumia mkondo wa kuomba shinikizo kutoka nje?
Nawasilisha.
Mojawapo ya mapungufu ya tume yetu (NEC) ni kwamba watendaji wake wote wanachaguliwa na Rais ambaye pia
ni mmoja wapo wa wagombea. Watendaji hawa wanawajibika kwake na anaweza kuwaondoa wakati wowote ikitegemea
ameamkaje siku hiyo.
Hali hii inakihakikishia ushindi CCM na serikali haitakubali hata siku moja pawepo na Tume iliyo huru.
Mojawapo ya ushahidi kuwa tume si huru ni mambo yaliyojiri wakati wa kampeni za uchaguzi ambao unaofanyika leo. Ushahidi uko wazi jinsi ambavyo TBC ambayo ni taasisi ya serikali ilivyokuwa ikionyesha muda wote kampeni za mgombea urais wa CCM na kuvinyima vyama vya upinzani fursa hiyo.
Pia tume ilikataa kupokea malalamiko ya vyama vya upinzani kuhusu mgombea wa CCM pale alipoamuru Katibu Mkuu wa TAMISEMI apeleke pesa Hedaru za kujenga kituo cha Afya wakati huo huo kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi. Kwa kuwa wito wa kuwa na tume huru ya uchaguzi unagonga mwamba je ni wakati wa kuwepo shinikizo kutoka nje ili pawepo na Tume Huru ya Uchaguzi?
Ikumbukwe kwamba si jambo geni kwa sheria kadhaa kutungwa au kubadili sheria zilizopo hapa Tanzania kutokana na shinikizo kutoka nje.
Sote tunakumbuka jinsi ambavyo sheria ya kupambana na ugaidi ilivyopitishwa mwanzoni mwa miaka ya 2000 kutokana na shinikizo kutoka Marekani.
Tumeona jinsi ambavyo watanzania walishiriki katika tukio hilo ambalo limefanyika hapa wakipelekwa marekani ili wakakabiliane na mashtaka huko.
Hata hivi majuzi Rais alipopitisha Executive Order ya kuzuia wasichana wanaopata mimba wakiwa shuleni waisruhusiwe kendelea na masomo baadaya kujifungua, agizo hilo liliondolewa kutokana na shinikizo kutoka nje. Hata sheria ya makosa ya mtandao na sheria ya takwimu ilipunguzwa makali kutokana na shinikizo kutoka nje.
Je, wakati umefika kwa wale wanaotaka Tume Huru ya Uchaguzi kutumia mkondo wa kuomba shinikizo kutoka nje?
Nawasilisha.