Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,415
- 21,109
- Thread starter
- #21
Mkuu acha kupotosha watu, ni sawa binadamu wa leo akaye na malaika au jini halafu binadamu aseme kwamba kaumbwa kwa udongo na jini kaumbwa kwa moto kwa hiyo haimaanishi kwa kusema hivyo imfanye huyo binadamu awe ndiye binadamu wa kwanza kuumbwa.Kwanza ufahamu si majini wote ni waovu kipindi bado binadamu hajakuja duniani kulikuwa na majini wanaomuabudu mungu na majini ambao walikuwa wakimuasi mungu.
Soma hizi aya mbili
“ ‘I am better than him (Adam), You created me from fire, and him You created from clay’”
[al-A’raaf 7:12]
Hii aya inaonesha iblis ametengenezwa na mungu kutokana na moto (hajazaliwa)
“Will you then take him (Iblees) and his offspring as protectors and helpers rather than Me while they are enemies to you?”
[al-Kahf 18:50]
Hapa inaonesha Iblis ana watoto kama nimetafsiri vizuri,
Kama nilivyokuambia hapo juu kuna majini wema na wabaya hivyo iblis alikuwa kundi la majini mema na aliungana na malaika kupigana vita na majini wabaya (battle of good and evil) na malaika pamoja na iblis wakashinda na majini wabaya wakatokomezwa, baada ya vita iblis akitegemea ushindi wake atapata zawadi fulani amazing kama kupewa awe kiongozi wa dunia hivi ila Mwenyezi Mungu alikuwa na plan nyengine akamuumba adam, na kumpa uongozi wa dunia, hope stori inavyoendelea unaijua.
Na si kweli kwamba malaika walisaidiwa na majini ili kupambana na majini wengine , kaa ukijua malaika wawili tu wanaweza wakasambaratisha majini yote yaliyopo duniani sasa unaposema malaika walisaidiwa na majini inamaanisha kwamba malaika walikuwa wamezidiwa nguvu na majini kitu ambacho ni kufuru kubwa sana.