Je, Shekilango na Urafiki ndio Stendi mpya za Mabasi yaendayo mikoani?

Ukweli ni kuwa mtoa mada hajui alisemalo.
Basi zote lazima ziingie stendi ya Magufuli. Haijalishi imetoka Shekilango, kariakoo au magomeni.

Mapato ya serikali yapo pale pale.
Hivi lengo la kusema mabasi yaende pale stendi ya Magufuli ni ili tu yakalipe ushuru? Mfano kama bus halina abiria yoyote anaepanda/shuka magufuli terminal, kwanini liende? Ushuru si wanaweza wakalipa hata kwa mpesa au wakaamua kulipia mabasi yao yote kwa mwezi shida iko wapi?
 
Wabongo tunapenda sana kuoneana huruma hili ni suala jema ila kwa upande mwingne ni upumbavu mkubwa
Stand imejengwa kwa mapesa meng tena ukute niya mkopo arafu wanatokea wajinga wachache wenye mabasi wanakataa kufuata utarabibu mtu akiongea km mtoa mada hapa anaonekana mnafiki ametumwa
Sawa stand iko mbal na Jiji sawa atukatai ila sasa vyanzo vya uchumi vimeongezeka sabu
**** mtu wa boda atapata
Taxi atapata. Na ata bajaji na daladala wote watapata pesa kwa kusogeza abiria stand mpya
Haya gari linapaki Mbagala.

Abiria wengine wanakaaa Mbagala au Magomeni na maeneo ya Karibu.

Kwahiyo inatakiwa Bus litoke Mbagala likiwa TUPU mpaka Magufuli stand.

Na abiria apande daladala mpaka Magufuli stand kwenda kulipandq Hilo Bus.

Hii ni akili au mtindio wa ubongo????

Na Jioni ukifika Dar, Bus linatakiwa likushushe magufuli stand wakati unaenda Riverside na huko huko ndiko Bus linakoenda kulala??

Siyo???
 
Muwe mnasoma hoja vizuri, jamaa hazungumziii kukata tiketi, hoja ya msingi hapa na baadhi ya mabasi kutopitia kabisa Mbezi Bus Terminal, zinapandisha abiria hapo Urafiki na kupita juu kwa juu.
Habar za ticket nimequote jamaa aliyezungumza kuhusu ticket, ungeelewa kwanza yaye alisemaje ndo ukaniambia hivyo

Acheni papara nyie kujifanya kujua, hata hivyo suala la tiketi na usafiri ni nje ya mada?
 
Muwe mnasoma hoja vizuri, jamaa hazungumziii kukata tiketi, hoja ya msingi hapa na baadhi ya mabasi kutopitia kabisa Mbezi Bus Terminal, zinapandisha abiria hapo Urafiki na kupita juu kwa juu.
Yataje hayo mabasi
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya Shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal
Shekilango International Airport
 
Back
Top Bottom