Je, Serikali imekuwa Madalali wa Mitandao ya Kijamii?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Kama kuna jambo ambalo limekuwa naliona lina mapungufu mengi kisheria ni hili la kutaka watu siyo tu wajiandikishe TCRA wanapofungia 'channels' za YouTube lakini pia kutakiwa kulipa zaidi ya Shilingi milioni moja kila mwaka.

Hii ni kwa sababu mtandao kama YouTube ni bure na Serikali haijawekeza gharama zozote katika uanzishwaji wake wala haina uhusika katika uendeshaji wake. Inapotokea unaweka gharama kama hizi ni kama vile inajinasibisha wewe kama ni mmoja wa wamiliki wake na una mamlaka ya kufanya hivyo kitu ambacho naona wazi kuwa serikali haina mamlaka hayo.

Hii haina tofauti na matapeli wa nyumba na viwanja wanaopeleka watu site wakijidai wao ni wamiliki au mawakala halali wa uuzwaji wa nyumba hizo wakati hata haziuzwi. Hii inalazimisha hata wamiliki wa nyumba kuchafua kuta za nyumba zao kwa maandishi ya 'OGOPA MATAPELI. NYUMBA HII HAIUZWI'.

Juzi nimesikia wameitoza faini YouTube Channel moja kwa kutoweka wazi Terms and Conditions kwa watazamaji wake. Hivi watumiaji wa Youtube wanaweza kujitengenezea terms zao wenyewe tofauti na zile za YouTube ambazo ziko wazi kwa yoyote kuziona? Haya mambo yanachekesha na kustaajabisha sana.

Tushukuru tu kuwa soko letu bado ni dogo sana, hivi hivi Google (wamiliki wa Youtube) wangestahili kuchukua hatua kwenye hili. Au hili jambo linafanyika kwa ushirikiano na Google bila kuwekwa wazi?

Wanasheria wetu mnakwama wapi?
 
Kwanza hakuna kodi au tozo ya leseni inayotolewa bila kutungiwa sheria. Sheria inatungwa na bunge kutokana na sababu ya hitajio.

Serikali kutomiliki mtandao wa youtube hakuinyimi haki ya tozo. Serikali inatozo kwa vyombo vya habari lakini haimiliki mitambo ya uchapishaji.

YouTube channel zenye tozo ni zile zinazotoa maudhui (zinazotumika kutoa habari za kila siku) hizo kwa sheria ya sasa lazima TCRA iratibu, idhibiti na kuhakiki taarifa zake hivyo kulazimu kuwa leseni.
 
Kufanya bihashara katika developing countries ni ngumu sana, sio mchezo maana unaanza projects unapigwa vita na ukishaanzisha wanataka kodi mara wakupige faini zisizo na kichwa wala miguuu na wakati apo apo TTCL imeshimdwa kupambana katika soko hili.


Ugali Maharagwe umeharibu Akili za Watanzania
 
Kwanza hakuna kodi au tozo ya leseni inayotolewa bila kutungiwa sheria. Sheria inatungwa na bunge kutokana na sababu ya hitajio.

Serikali kutomiliki mtandao wa youtube hakuinyimi haki ya tozo. Serikali inatozo kwa vyombo vya habari lakini haimiliki mitambo ya uchapishaji.

YouTube channel zenye tozo ni zile zinazotoa maudhui (zinazotumika kutoa habari za kila siku) hizo kwa sheria ya sasa lazima TCRA iratibu, idhibiti na kuhakiki taarifa zake hivyo kulazimu kuwa leseni.

Tofauti ni kubwa sana ila umejitia upofu au kuamua kutetea uongo. Kilichofanyika ni kutafuta shortcut huku tatizo likibaki palepale kama siyo kukua zaidi.

Kama nia ilikuwa kuratibu, kudhibiti na kuhakiki maudhui ya habari, wangeweza kuendelea kutumia sheria zilezile za habari zilizokuwepo.
 
Kufanya bihashara katika developing countries ni ngumu sana, sio mchezo maana unaanza projects unapigwa vita na ukishaanzisha wanataka kodi mara wakupige faini zisizo na kichwa wala miguuu na wakati apo apo TTCL imeshimdwa kupambana katika soko hili.


Ugali Maharagwe umeharibu Akili za Watanzania

Tunamiss nafasi za kutengeneza mifumo imara yenye tija kwa sababu ya ubabe na utumiaji vibaya wa madaraka badala ya ubunifu na kuwasikiliza wengine.
 
Tofauti ni kubwa sana ila umejitia upofu au kuamua kutetea uongo. Kilichofanyika ni kutafuta shortcut huku tatizo likibaki palepale kama siyo kukua zaidi.

Kama nia ilikuwa kuratibu, kudhibiti na kuhakiki maudhui ya habari, wangeweza kuendelea kutumia sheria zilezile za habari zilizokuwepo.
Uongo ni upi? Huamini kuwa online tv na publications zimetungiwa sheria ya kuwa na leseni? Sheria gani ya zamani inge accomodate Online TV na publications ambazo wakati wa utungwaji wake hivi vitu havikuwapo!!??

Rejea kesi ya kufungiwa Gazeti la Mwanahalisi miaka kadhaa iliyopita. Waliendelea kuwa hewani ktk mtandao hali iliyoleta tafaruku ya kisheria sababu haikuhusu online publication
 
Uongo ni upi? Huamini kuwa online tv na publications zimetungiwa sheria ya kuwa na leseni? Sheria gani ya zamani inge accomodate Online TV na publications ambazo wakati wa utungwaji wake hivi vitu havikuwapo!!??

Rejea kesi ya kufungiwa Gazeti la Mwanahalisi miaka kadhaa iliyopita. Waliendelea kuwa hewani ktk mtandao hali iliyoleta tafaruku ya kisheria sababu haikuhusu online publication

Domain ya serikali kwenye mitandao inaanzia wapi na kuishia wapi? Unapolinganisha YouTube channel na kampuni kama ITV au AZAM, je hizo YouTube channel zinalazimika kufuata sheria zote za habari ambazo zinafuatwa na hizo kampuni zingine? Je unahitaji hata kuwa na kampuni iliyosajiliwa ili kupewa leseni na TCRA ya kuendesha YouTube channel?

Kama suala ni udhibiti, ilitakiwa tu kukumbushana kuwa ili ufanye BIASHARA halali, inabidi ujisajili BRELA au mamlaka zingine za usajili wa taasisi na mashirika. Hapo mambo ya leseni kwa mamlaka husika yanakuja automatically. Unadhani miaka yote Press Cards za waandishi wa habari kazi yake ilikuwa ni nini?

Hivi unajua hata makanisa yanayorusha mahubiri yake YouTube yanalazimika kufuata sheria hizo mpya?

Suala la kutunga sheria fulani siyo issue. Leo hii inaweza kutungwa sheria kuwa hairuhusiwi kuvaa kofia, ikapitishwa na kutekelezwa na machoni pako ikawa halali kwa kuwa tu tayari ni sheria. Hapa nahoji UHALALI wa sheria hiyo.
 
Domain ya serikali kwenye mitandao inaanzia wapi na kuishia wapi? Unapolinganisha YouTube channel na kampuni kama ITV au AZAM, je hizo YouTube channel zinalazimika kufuata sheria zote za habari ambazo zinafuatwa na hizo kampuni zingine? Je unahitaji hata kuwa na kampuni iliyosajiliwa ili kupewa leseni na TCRA ya kuendesha YouTube channel?

Kama suala ni udhibiti, ilitakiwa tu kukumbushana kuwa ili ufanye BIASHARA halali, inabidi ujisajili BRELA au mamlaka zingine za usajili wa taasisi na mashirika. Hapo mambo ya leseni kwa mamlaka husika yanakuja automatically. Unadhani miaka yote Press Cards za waandishi wa habari kazi yake ilikuwa ni nini?

Hivi unajua hata makanisa yanayorusha mahubiri yake YouTube yanalazimika kufuata sheria hizo mpya?

Suala la kutunga sheria fulani siyo issue. Leo hii inaweza kutungwa sheria kuwa hairuhusiwi kuvaa kofia, ikapitishwa na kutekelezwa na machoni pako ikawa halali kwa kuwa tu tayari ni sheria. Hapa nahoji UHALALI wa sheria hiyo.
Hapo naona unajichanganya. Sheria haikutungwa kwa kuwalenga Youtube. Imelenga mtu binafsi au Kampuni iliyosajiliwa Tanzania (Brela) kwa biashara ya kurusha maudhui mtandaoni. Youtube ni kipitishio tu kinacho ruhusu watu au kampuni isio na uwezo wa kuwa na Domain (Malipo ya mwaka) kupitishia taarifa zao. Na si kweli kuwa ukisajiliwa Brela unaendelea na biashara bila kuwa na leseni toka mamlaka husika, na vyombo vya habari ni TCRA. Watumishi au mtu Kuweka mahubiri, video, haihitaji leseni bali makosa yake yanakemewa na sheria ya makosa ya maadili mtandaoni.
 
Hapo naona unajichanganya. Sheria haikutungwa kwa kuwalenga Youtube. Imelenga mtu binafsi au Kampuni iliyosajiliwa Tanzania (Brela) kwa biashara ya kurusha maudhui mtandaoni. Youtube ni kipitishio tu kinacho ruhusu watu au kampuni isio na uwezo wa kuwa na Domain (Malipo ya mwaka) kupitishia taarifa zao. Na si kweli kuwa ukisajiliwa Brela unaendelea na biashara bila kuwa na leseni toka mamlaka husika, na vyombo vya habari ni TCRA. Watumishi au mtu Kuweka mahubiri, video, haihitaji leseni bali makosa yake yanakemewa na sheria ya makosa ya maadili mtandaoni.

Ndiyo maana nasema unapotosha kwa kujua au kutojua, na nadhani UNAJUA UNACHOFANYA. Hakuna sehemu ninapojichanganya.

Nimekuuliza mswali, ungeyajibu wazi upotoshaji wako ungedhihirika.

Ninaposema 'domain ya serikali' namaanisha 'MAMLAKA au MIPAKA ya serikali. Simaanishi domain name.

Na sijasema kuwa ukisajiliwa BRELA unaweza kuendelea na biashara bila leseni. Yaani hoja niliyoitumia kukukosoa umeigeuza kama vile haujaielewa!!

Na haujanijibu nilipokuuliza MTU BINAFSI aambaye Youtube HAWANA matatizo naye kuanzisha YouTube channel, anaweza pia kujisajili TCRA kuendesha channel hiyo bila kusajili kwanza kampuni?

Kwa kumalizia, ninamjua Mchungaji ambaye ilibidi asitishe kuweka mahubiri yake Youtube mpaka alipowekana sawa na TCRA. Namjua mtu mwingine pia ambaye anauza vitu kwenye kablog kake, alipoenda TCRA aliambiwa kuwa inabidi afanye mchakato ule ule wa kusajili.

Hili suala lingeweza kushughulikiwa kwa kukazia sheria zilizokuwepo. Wahusika hawakutaka tu kuumiza vichwa, wakaona watafute njia za mkato ambazo hazileti mantiki yoyote.

Nimalizie kwa kukuuliza swali la ziada. Hivi Mtanzania akitupia picha zake binafsi za ngono katika mitandao ya ngono iliyoko nje ya nchi, je serikali ina MAMLAKA ya kumuadhibu kwa sheria zozote za nchi ZILIZOPO?
 
Back
Top Bottom