Je, Serikali imeanza kulegeza kamba? Yaruhusu Uraia Pacha kwa Watoto

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
42,390
49,040
Masauni.JPG

Picha: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni

SERIKALI imelieleza Bunge kuwa hairuhusu uraia pacha kwa watu wazima isipokuwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 18.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni, alitoa kauli hiyo bungeni jana alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Agnesta Lambert.

Alihoji kama serikali iko tayari kuruhusu uraia pacha kwa Watanzania wenye uraia wa nchi nyingine.

Akijibu swali hilo, Masauni alisema uraia wa Tanzania unaongozwa na Sheria ya Uraia ya Tanzania Sura ya 357, marejeo ya mwaka 2002.

“Sheria hii inabainisha aina tatu za uraia wa Tanzania ambazo ni uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajnisi. Kwa mujibu wa Sheria ya Uraia tajwa hapo juu, serikali hairuhusu uraia pacha kwa watu wazima isipokuwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 18 ambao wanakuwa na uraia wa Tanzania na uraia wa nchi nyingine,” alisema.

Source: Nipashe
 
Mbona uraia pacha upo siku nyingi ila haupo wazi, nakumbuka baadhi ya vigogo walishatajwa kuwa raia wa marekani kitambo sana na hasa wanaojiita maaskofu na wanasheria kadhaa
Cc zuhura Yunus Salim Kikeke marehemu Lemutuz, Mulamula ( hadi akawa waziri wa mambo ya nje), kigagula ajuza mbishi FaizaFoxy anayo ya canada na bongo.
 
Binafsi napinga sana swala la Uraia Pacha,mtu ameukana Utanzania wa nini kumbembeleza?
Serikali yetu tafadhali sana tunaomba mu-extend uraia pacha uwe na kwa watu wazima. Hii itatusaidia sana kuweza kufanya shughuli zetu kwa tija na manufaa zaidi tukiwa nje na wakati huo huo tukiwa na moyo na uzalendo kwa nchi yetu Tanzania.
 
Dalili za kuanza kulegea.
Akichoingea kiko siku nyingi mbona kuwa mtoto yeyote akizaliwa Tanzania au nje ya Tanzania na wazazi wa Tanzania atahesabika raia hadi atakapofikisha miaka 18 baada ya hapo ataamua awe raia wa nchi gani Tanzania au nje sasa hao uraia pacha waliuchachukua uraia wa nje baada ya kufikia umri.zaidi ya miaka 18
 
Hapana, nchi zingine zinaruahusu, huna haja ya kuukana Utanzania.

Tanzania ndiyo inalazimisha uukane uraia wa bchi nyingine ukitaka kuwa raia.

Usipotoshe.
Kuna comment hapo juu inasema una uraia wa Canada!
 
Watoto wa walimu hamna akili.

Under 18 haruhusiwi chagua Uraia hadi avuke 18 ndo anachagua
 
Cc zuhura Yunus Salim Kikeke marehemu Lemutuz, Mulamula ( hadi akawa waziri wa mambo ya nje), kigagula ajuza mbishi FaizaFoxy anayo ya canada na bongo.
Wapo wengi sana kwa maelfu kama siyo malaki lakini kwa Tanzania unabaki kuwa ni Mtanzania tu.

Wacha hao wa Ulaya na wa nchu za mbali. Tanzania imepakana na nchi ngapi? Takriban raia wote wa mipakani wana uraia pacha.

Tanzania iruhusu tu uraia pacha.

Wazanzibari 100% wana uraia pacha, kwani wana serikali yao ya Zanzibar na wana serikali ya muungano.
 
Back
Top Bottom