msovero
JF-Expert Member
- Jun 30, 2019
- 839
- 1,472
Kuna muda nakuwa nashindwa kuielewa hii serikali yangu.
Pengine labda ni kutokana na uelewa na ufahamu mdogo nilionao kuhusu uendeshaji wa shirika letu la ndege kwani kauli na kaguzi zinazotolewa na serikali kuhusu uendeshwaji wa shirika hili zinanichanganya sana.
Kwenye ripoti ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka 2017/2018, CAG alibainisha kuwa kuna mashirika ya serikali yanajiendesha kwa hasara na hayaingizi faida yoyote. Miongoni mwa mashirika hayo mdhibiti alitaja ni pamoja na shirika letu la ndege ATCL.
Lakini haikuishia hapo kwani katika ripoti ya CAG ya mwaka 2019/2020 makaguzi wa hesabu za serikali alienda mbali na kudai shirika letu la ndege si tu linajiendesha kwa hasara bali limeingiza hasara 'loss' ya zaidi ya billion 150 kwa miaka mitano mfululizo tangu lilipofufuliwa na hayati magufuli.
Juzi msemaji wa serikali anaibuka na kauli kwamba serikali iko mbioni kununua ndege zingine tano na tayari billion 212.95 zimeshatolewa kama malipo ya awali ya ununuzi wa ndege hizo.
Sasa hapa ndipo panapo nipa utata kwa sababu katika hali ya kawaida ni mjinga pekee ndiye anaweza kufanya biashara ambayo haiingizi faida.
Sasa Kama serikali yenyewe inakiri kwamba shirika linajiendesha kwa hasara na haliingizi faida kuna haja gani ya kwenda kununua ndege zingine wakati zilizopo tu zimeshindwa kutengeneza faida na kuliingiza taifa kwenye hasara ya mabilioni?
Pengine labda ni kutokana na uelewa na ufahamu mdogo nilionao kuhusu uendeshaji wa shirika letu la ndege kwani kauli na kaguzi zinazotolewa na serikali kuhusu uendeshwaji wa shirika hili zinanichanganya sana.
Kwenye ripoti ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka 2017/2018, CAG alibainisha kuwa kuna mashirika ya serikali yanajiendesha kwa hasara na hayaingizi faida yoyote. Miongoni mwa mashirika hayo mdhibiti alitaja ni pamoja na shirika letu la ndege ATCL.
Lakini haikuishia hapo kwani katika ripoti ya CAG ya mwaka 2019/2020 makaguzi wa hesabu za serikali alienda mbali na kudai shirika letu la ndege si tu linajiendesha kwa hasara bali limeingiza hasara 'loss' ya zaidi ya billion 150 kwa miaka mitano mfululizo tangu lilipofufuliwa na hayati magufuli.
Juzi msemaji wa serikali anaibuka na kauli kwamba serikali iko mbioni kununua ndege zingine tano na tayari billion 212.95 zimeshatolewa kama malipo ya awali ya ununuzi wa ndege hizo.
Sasa hapa ndipo panapo nipa utata kwa sababu katika hali ya kawaida ni mjinga pekee ndiye anaweza kufanya biashara ambayo haiingizi faida.
Sasa Kama serikali yenyewe inakiri kwamba shirika linajiendesha kwa hasara na haliingizi faida kuna haja gani ya kwenda kununua ndege zingine wakati zilizopo tu zimeshindwa kutengeneza faida na kuliingiza taifa kwenye hasara ya mabilioni?