Je, Scholarship ni mbinu ya kutengeneza Vibaraka hasa wa Kisiasa?

JE SCHOLARSHIP NI MBINU YA KUTENGENEZA VIBARAKA WA KISIASA?

Anaandika Robert Heriel.

Scholarship inaweza kuwa na maana nyingi, mojawapo ni kumsaidia mtu/mwanafunzi kirasilimali aweze kupata elimu Fulani; Rasilimali hiyo inaweza kuwa Fedha, au mahali pa kuishi(makazi), au chakula, au vitendea kazi vya kujifunzia.

Mara nyingi kama zote Scholarship hutolewa Kwa sababu kadhaa, zipo sababu za wazi na zile sababu za siri/nyeti ambazo mtoa scholarship hazitaji Mwanzoni.

Zipo scholarship zinazotolewa na Makundi Yafuatayo;
1. Mtu binafsi
2. Kampuni au shirika
3. SERIKALI

Mtu binafsi Kama Mimi na Wewe tunaweza kutoa scholarship Kwa wanafunzi wengine. Hata hivyo hatuwezi kukataa ukweli kuwa Scholarship haitolewi burebure.

Wapo watu waliopewa Scholarship wakasome ili waje kuoa/kuolewa na mtoto wa mtoa Scholarship. Wengine hutoa scholarship Kwa kusomesha watoto Yatima lakini katika hao Yatima wapo ambao baadaye hupewa majukumu Fulani huko mbeleni wakishafanikiwa kimasomo, huingizwa kwenye aidha mambo ya Siasa, au kuajiriwa katika sekta nyeti ili walinde maslahi ya waliowasomesha. Hata hivyo si lengo langu Kueleza scholarship za watu binfasi.

Pia makampuni, taasisi na mashirika makubwa hutoa scholarship Kwa watu wake Kwa lengo la kuimarisha future ya kundi husika.
Zipo taasisi za Kidini, hutoa scholarship na kuhakikisha zinapenyeza watu wao katika Sekta nyeti ndani ya serikali au katika makampuni na mashirika mengine. Vyama vya Kisiasa navyo hutoa Scholarship Kwa baadhi ya wanachama wake. Hata hivyo ni kawaida Kwa chama kimoja kinaweza kumsomesha mwanachama wa chama kingine pasipo chama husika kujua, kisha baadaye kumtumia mtu huyo katika kuangusha chama hasimu. Mfano, CCM inauwezo wa kumsomesha mwanachama wa CHADEMA bila CHADEMA kujua, mwanachama huyo akaenda mpaka Ulaya huku akiendelea kushiriki Kwa Hali na Mali na shughuli za CHADEMA mpaka kufikia kuaminika, alafu mwisho wa siku akipewa Madaraka makubwa au yanayokaribia ukubwa hukiteteresha Kama sio kukiangusha chama, hiyo ni kawaida kisiasa. Hata hivyo sina lengo pia la Kueleza Jambo hili.

Scholarship zitolewazo na serikali ndio lengo langu kuu katika andiko hili. Kila serikali inanamna yake ya kujiimarisha katika siku za usoni, moja ya mbinu za kufanya hivyo ni Kutoa Scholarship Kama sehemu ya kuwekeza Kwa watu Kwa maslahi ya siku zijazo.

Serikali nyingi za Afrika ikiwemo nch yetu mara nyingi huwapa Scholarship watoto wa viongozi bila kuangali na kufuata vigezo muhimu.
Scholarship Kwa maslahi ya Future ya nchi inapaswa ifuate na kutafuta watu wenye vigezo maalumu. Nitataja Kwa uchache;

1. Wenye Akili na Maarifa ya juu Kabisa
Sio akili za Darasani Bali hata akili za Mtaani, akili za kuongoza watu Kwa kutumia Akili. Zingatia ukiona nguvu kubwa inatumika sehemu ujue akili ndogo imetumika, na ukiona akili nyingi inatumika ujue nguvu ndogo itatumika.

Kiongozi anayetumia nguvu kubwa ujue akili yake huwa kisoda.

2. VIPAJI NA KARAMA ZA JUU
Mtu mwenye kipaji iwe uimbaji, uchoraji, Machale na maono, Hesabu, kipaji cha lugha, kujua lugha ngeni Kwa wepesi, kuchezea computer na masuala yote ya IT, Ubunifu wa Teknolojia mpya au zilizopita kuziboresha, n.k.
Hawa ndio wanapaswa kupewa Scholarship Kwa maslahi ya nchi.

3. UZURI NA MVUTO WA MAUMBILE
Wanawake wazuri kupitiliza, na vijana wenye mvuto ni muhimu Sana kupewa scholarship hasa kwenye ishu za intelejensia ya nchi.

Kwa Wazungu wao Kwa kulijua hili ndio maana wakaanzisha MASHINDANO YA WALIMBWENDE ambayo hujulikana Kama MISS WORLD ambayo Kwa nje yanaonekana ni sehemu ya kukuza vipaji vya fasheni na uanamitindo lakini ajenda za ndani kabisa ni tofauti.

Hawa walimbwende wanaoshinda, wengi wao huzikimbia nchi zao, na kutokomea nchi za baridi huko Ulaya. Husomeshwa na Wale wasio na akili za darasani hupewa majukumu Fulani na kupewa mitaji ya pesa na connection kubwa kubwa.

Warembo hawa baadaye wengi wao hata hapa nchini tunajua wanashobokewa na kuolewa na vigogo Kama sio wafanyabiashara Wakubwa. Bado hujaelewa what next? 😀😀 Wakubwa mmeelewa.

Tusikubali wanawake Wazuri kupitiliza WA nchi hii watumike na watu wa nchi zingine.

Sitaki kuelezea baadhi Yao ambao huweza kuingizwa kwenye biashara hatari na nyeusi ambazo ni jinai kubwa hapa nchini. Biashara za madawa ya kulevya ambazo warembo wetu huweza kutumika Kama Punda kuzitoa upande mmoja wa nchi kwenda nchi zingine.

Hata hivyo ni lazima warembo hawa wajiingize katika mapenzi mazito na vigogo wa nchi husika, utashangaa Mrembo mkali Grade one wa nchi yetu akiingia katika penzi zito na Rais au kigogo wa nchi Fulani, nchi hiyo hata wamkamate huyu mrembo hawawezi kumfanya kitu sababu tayari ana-connection ya moja Kwa moja na vigogo wa nchi hiyo.

Tuachane na haya.

4. WATU WENYE KARAMA ZA UCHUNGAJI NA USHEIKHE NA UGANGA
Kundi hili ni nyeti Kwa sababu ni kimbilio na waovu na Wema.
Scholarship ni muhimu Kwa kundi hili kuliweka mahususi Kwa mipango ya siku zijazo.
Nani asiyejua hata hapa nchini wapo viongozi tena wa ngazi ya Urais kabisa walitoka hapa nchini kwenda mpaka Nigeria Kwa TB Joshua, unafikiri mtu Kama anashida akifika Kwa mganga au mchungaji au Sheikhe hatasema mambo yote kusudi asaidiwe?

Hapa nchini ni nadra Sana Kwa Kiongozi mkubwa wa Kisiasa au wakurugenzi WA makampuni au mashirika makubwa kutojihusisha na Uganga, ama wachungaji wakubwa au masheikhe wakubwa. Wengi WA watu au vigogo wakubwa lazima wawe na mganga wanayemtegemea au mchungaji au Sheikhe. Hilo pia Kwa Majambazi, wezi na wafanya dili HATARI.

Tukiachana na watu wenye sifa hizo.

Mataifa makubwa ya Ulaya, hutumia watu niliowataja hapo juu kuzitawala nchi ZETU.

Vijana wanasomeshwa, wanasoma na kufunzwa hasa namna ya kuwa kibaraka mtiifu. Kisha akihitimu shahada ya kwanza, huja nchini na kuanzisha viprogramu vyake vya hapa na pale.
Kisha huenda tena kusoma na kuchukua degree ya pili mpaka yatatu. Alafu anarudi.

Baadhi Yao hupewa majukumu ya kijamii Kwa kuanzisha vishirika visivyo vya kiserikali Kwa kulenga moja ya mambo Yafuatayo;
1. Kutetea haki za wanawake
2. Kutetea mashoga na wasagaji au mapenzi ya mtu na mnyama
3. Kutetea Demokrasia inayozua ghasia na kuchafua Amani ya nchi.
4. Kutafiti na kuwa consultant wa mambo ya kiuchumi na kupewa nyenzo zote. Hapa utaona vita katika tenda za serikali utashangaa nyingi zinashikiliwa na makampuni ya kigeni ingawaje makampuni mengine huwa na majina ya Watanzania Kama Geresha tuu. Yaani utashangaa Mimi Taikon namiliki Kampuni kubwa lakini kumbe nyuma yangu wapo mabeberu.
5. Kutetea maslahi ya Wazungu hasa kwenye mikataba inayopitishwa bungeni. Miongoni mwa mambo mengine.

Ukiachana na hayo;

Scholarship huweza kuathiri sekta nyeti Kama usalama wa taifa, Bunge na mahakama.

Siku zote hakuna kitu cha Bure.

Ushauri:
Serikali inapaswa iwe Makini Sana katika Jambo hili.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
DAR ES SALAAM

Andiko lako zuri na ni fikirishi sana.
Ukisoma kitabu cha John Perkins named The Confession of Economic Hit-man na kama umetizama series named Covert Affairs inayoelezea National Clandestine Services moja ya idara ya kijasusi CIA kuna jambo la kujifunza.

John Perkins alikuwa na interest kufanya kazi na NSA, wao wakaona ana potential kubwa kufanya nae kwenye private interprise kwa maslahi yao makubwa unlike angebaki NSA. Na hata baada ya kusema ukweli wamekanusha kuwa hawamtambui ana anadanganya ila ukisoma between the lines ya nini kaandika vs nini kinatokea kwenye nchi za dunia ya 3, unapata kujua nini Perkins anatuasa.

Covert affairs inaonesha namna CIA imejira operatives na assets. Na kwenye level ya assets ni watu wa kawaida hawana day to-day involvement na majukumu ya CIA, ila unaona namna gani contacts ya operatives na assets inatengenezwa na mambo yaliyokusudiwa yanafanyika kutimiza lengo la idarani.

Nataka kuamini hata sisi hapa wakubwa wanaondesha nchi wako vizuri sana, ila kuna maeneo nadhani hawajafanya vya kutosha ikiwamo economic intelligence and economic security.

Haiwezekani na haingii akilini nchi kama Comoro jirani na Tanzania unakuata basic consumables anatoa India, China na Tanzania iko very close halafu nikinukuu alichowahi kusema mwandazake, tuna PhD 18 BoT achilia mbali walioko hazina, vyuo vikuu na kwingineko.
Kama tungewekeza kwenye economic intelligence, kwa kuzingatia all skills za how it takes tuwe at the cutting age ya basic consumables ili tuifikie hata SADC tu, nchi hii watu wangefurahia kuishi. Ila sasa, kama ulivyotoa maelezo, sijui tunafeli wapi?

Nihitimishe kwa mfano midogo miwili, umesema vema scholarships nyingi wanapewa watoto wa wazeiya. Wakienda wanarejea na vyeti ila kichwani inakuwa kawaida sana. Masihi hakuzaliwa nyumba ya Herode, alitokea kwenye Nazareth ila alifanya maajabu sana na akawa chanzo cha imani ya Ukristo, wenye uelewa watanielewa.

Farao alipopata ndoto ya masuke 7 manono yakimezwa na masuke 7 manyonge, the ng'ombe 7 wenye afya wakemezwa na ng'ombe 7 waliokonda; Farao alihangaika sana kujua nini ni suluhu ya ndoto ile.
Alietoa tafsiri ni Yusuf aliekuwa mfungwa; tukizungumza kwa lugha rahisi Yusuf alikuwa outsider kwenye governance system ya Egypt. Yet ndie alikuja na tafsiri ya how to develop 14 years food reserve and distribution system sio kwa Egyptians pekee, ila hata wageni nje ya Egypt njaa ikitokea. Nakuelewa unaposema akili ya kitaa, sio kila Profesa anayo. Kuna IQ ambayo watu wanayo, wame-develop skills zao outside the governance settings ila kama wakiombwa kuwa sehemu ya kuijenga nchi hii wanaweza kuwa na mchango mkubwa sana bila kuathiri nafasi za waliopo.

Kuna wakati waliopo wanaogopa kuwa out-shined, na hapo ndipo umasikini wa fikra unapoanzia. Wao wana majukumu yao mengi na wakisikia kuna new brain inaleta solution wanataka kudesa ili wafanye wao ili sifa wapate wao, bahati mbaya huwa ukidesa in the absence ya mwenye DNA ya project whicg leads to solution, ukiondoka kama ni Mwanza kwenda Dar, ukifika Ilula mpakani mwa Mwanza na Shinyanga ramanani inapotea au kama waenda Mwanza toka dar, ukifika round about ta Msamvu, unapotea njia. Na kama utafika badala ya safari kuchukua muda mfumpim wazungu wanasema "it will take forever".
7 years za wingi wa chakula ilikuwa muhimu sana kwa Yusuf kujenga food reserve system, kuweka ulizi, kuweka madawa ya kuzuia chakula kisibanguliwe ili miaka 7 sio tu wananchi wasife ila hata wanyama wasife.

Imagine leo msimu mmoja tu mvua zimechelewa, tumeanza kuaswa kutumia vema nafaka, wanyama wanakufa; wakati kuna watu karne nyingi BC, walikuwa na reserve ya 7 years za ukame. Wenye akili na wafahamu.

Jioni njema.

F
 
Nadhani huelewi mleta mada scholarship ni nini?

Mfano Serikali kupitia body ya mikopo hukopesha watu wasome maskini hiyo in scholarship ulichoeleza kwenye hili hata hujagusa

Scholarship namba mbili hulipiwa rare proffession ambazo vyuo vya ndani havitoi na hazipo na nchi inahitaji ya ndani au nje au dunia sababu ya wanafunzi kukwepa kusomea kutokana na ugumu wa hayo masomo wale waliotayari hupewa scholarship

Tatu Scholarship nyingi hutolewa kwa wavumbuzi na wenye outstanding performance iwe masomo nk kuwa in future waweza saidia nchi au dumia


Hizo scholarship zingine ni za vibaka na matapeli ohh tunatoa scholarship za mashoga kufundisha ushoga vyuoni nk wanawapiga pesa wachangiaji na kiduchu ndio wanasomeshea

Iwe dini ,sijui yatima ,mazingira magumu nk mfadhili lazima apige pesa .
 
"Dini" ni imani potofu over "dini" nyingine si ndio ?

Anyways nakuelewa maana hata dini ilikuja Afrika kutoka Arabuni inaona ile iliyotoka mashariki ya kati ni potofu, ya mashariki ya kati inaona ile iliyotokea Uchina ni potufu, ya uchina inaona ile India ni upotofu, ya bara Hindi inaona ile ya hapahapa Afrika ni upotofu na ushenzi mkubwa.

Maybe it is how they work.
Hakuna DINI potofu. DINI ni moja tu safi--imani kwa Mungu. Upotofu hauko kwenye DINI, bali uko kwa mwanadamu ambaye ameamua kujichagulia uelekeo wake mwenyewe. Akili ya mwanadamu ndiyo imejaa matongotongo yanayomzuia kumwona Mungu kwa mtazamo halisi.
 
Hakuna DINI potofu. DINI ni moja tu safi--imani kwa Mungu. Upotofu hauko kwenye DINI, bali uko kwa mwanadamu ambaye ameamua kujichagulia uelekeo wake mwenyewe. Akili ya mwanadamu ndiyo imejaa matongotongo yanayomzuia kumwona Mungu kwa mtazamo halisi.
Dini ni njia ya mwanadamu kumtafuta na kumfahamu Mungu wake.
Kama umekili kwamba mwanadamu ana akili yenye matongotongo, basi njia yake (ya kumfahamu Mungu) lazima itakua na makandokando.

Kusema dini iko straight wakati akili ya binadamu haiko straight nadhani sio sahihi sana.

Na ushahidi wa hilo upo. Ushahidi huo ni DINI NYINGI. Na kibaya zaidi aliye kwenye dini A, Anaseme yule aliye kwenye dini B amepotoka. Wa dini C anamshutumu wa dini D. Ni vurugu tupu.

Sioni straightness katika mkanganyiko huu.
 
Andiko lako zuri na ni fikirishi sana.
Ukisoma kitabu cha John Perkins named The Confession of Economic Hit-man na kama umetizama series named Covert Affairs inayoelezea National Clandestine Services moja ya idara ya kijasusi CIA kuna jambo la kujifunza.

John Perkins alikuwa na interest kufanya kazi na NSA, wao wakaona ana potential kubwa kufanya nae kwenye private interprise kwa maslahi yao makubwa unlike angebaki NSA. Na hata baada ya kusema ukweli wamekanusha kuwa hawamtambui ana anadanganya ila ukisoma between the lines ya nini kaandika vs nini kinatokea kwenye nchi za dunia ya 3, unapata kujua nini Perkins anatuasa.

Covert affairs inaonesha namna CIA imejira operatives na assets. Na kwenye level ya assets ni watu wa kawaida hawana day to-day involvement na majukumu ya CIA, ila unaona namna gani contacts ya operatives na assets inatengenezwa na mambo yaliyokusudiwa yanafanyika kutimiza lengo la idarani.

Nataka kuamini hata sisi hapa wakubwa wanaondesha nchi wako vizuri sana, ila kuna maeneo nadhani hawajafanya vya kutosha ikiwamo economic intelligence and economic security.

Haiwezekani na haingii akilini nchi kama Comoro jirani na Tanzania unakuata basic consumables anatoa India, China na Tanzania iko very close halafu nikinukuu alichowahi kusema mwandazake, tuna PhD 18 BoT achilia mbali walioko hazina, vyuo vikuu na kwingineko.
Kama tungewekeza kwenye economic intelligence, kwa kuzingatia all skills za how it takes tuwe at the cutting age ya basic consumables ili tuifikie hata SADC tu, nchi hii watu wangefurahia kuishi. Ila sasa, kama ulivyotoa maelezo, sijui tunafeli wapi?

Nihitimishe kwa mfano midogo miwili, umesema vema scholarships nyingi wanapewa watoto wa wazeiya. Wakienda wanarejea na vyeti ila kichwani inakuwa kawaida sana. Masihi hakuzaliwa nyumba ya Herode, alitokea kwenye Nazareth ila alifanya maajabu sana na akawa chanzo cha imani ya Ukristo, wenye uelewa watanielewa.

Farao alipopata ndoto ya masuke 7 manono yakimezwa na masuke 7 manyonge, the ng'ombe 7 wenye afya wakemezwa na ng'ombe 7 waliokonda; Farao alihangaika sana kujua nini ni suluhu ya ndoto ile.
Alietoa tafsiri ni Yusuf aliekuwa mfungwa; tukizungumza kwa lugha rahisi Yusuf alikuwa outsider kwenye governance system ya Egypt. Yet ndie alikuja na tafsiri ya how to develop 14 years food reserve and distribution system sio kwa Egyptians pekee, ila hata wageni nje ya Egypt njaa ikitokea. Nakuelewa unaposema akili ya kitaa, sio kila Profesa anayo. Kuna IQ ambayo watu wanayo, wame-develop skills zao outside the governance settings ila kama wakiombwa kuwa sehemu ya kuijenga nchi hii wanaweza kuwa na mchango mkubwa sana bila kuathiri nafasi za waliopo.

Kuna wakati waliopo wanaogopa kuwa out-shined, na hapo ndipo umasikini wa fikra unapoanzia. Wao wana majukumu yao mengi na wakisikia kuna new brain inaleta solution wanataka kudesa ili wafanye wao ili sifa wapate wao, bahati mbaya huwa ukidesa in the absence ya mwenye DNA ya project whicg leads to solution, ukiondoka kama ni Mwanza kwenda Dar, ukifika Ilula mpakani mwa Mwanza na Shinyanga ramanani inapotea au kama waenda Mwanza toka dar, ukifika round about ta Msamvu, unapotea njia. Na kama utafika badala ya safari kuchukua muda mfumpim wazungu wanasema "it will take forever".
7 years za wingi wa chakula ilikuwa muhimu sana kwa Yusuf kujenga food reserve system, kuweka ulizi, kuweka madawa ya kuzuia chakula kisibanguliwe ili miaka 7 sio tu wananchi wasife ila hata wanyama wasife.

Imagine leo msimu mmoja tu mvua zimechelewa, tumeanza kuaswa kutumia vema nafaka, wanyama wanakufa; wakati kuna watu karne nyingi BC, walikuwa na reserve ya 7 years za ukame. Wenye akili na wafahamu.

Jioni njema.

F
Ngoja nitafute hivi vitabu niongeze maarifa.
 
Watumishi wa Umma au waTanzania
Inawezekana, binafsi nilichojifunza na ambacho ni kweli kabisa 80% watumishi wa serikali yetu ni vilaza, hivyo hata vision ya nchi huwa ngumu, wengi wa watumishi wetu hawana uwezo wa kuchambua mambo kikawaida tu.
 
Dini ni njia ya mwanadamu kumtafuta na kumfahamu Mungu wake.
Kama umekili kwamba mwanadamu ana akili yenye matongotongo, basi njia yake (ya kumfahamu Mungu) lazima itakua na makandokando.

Kusema dini iko straight wakati akili ya binadamu haiko straight nadhani sio sahihi sana.

Na ushahidi wa hilo upo. Ushahidi huo ni DINI NYINGI. Na kibaya zaidi aliye kwenye dini A, Anaseme yule aliye kwenye dini B amepotoka. Wa dini C anamshutumu wa dini D. Ni vurugu tupu.

Sioni straightness katika mkanganyiko huu.
Tatizo unang'ang'ana na njia za wanadamu na kuacha DINI ya Mungu. DINI ni safi haina upotofu. Huko ndiko tunapaswa kuifuata njia. Umeelewa?
 
Tatizo unang'ang'ana na njia za wanadamu na kuacha DINI ya Mungu. DINI ni safi haina upotofu. Huko ndiko tunapaswa kuifuata njia. Umeelewa?
"Dini ya Mungu" ni dini ipi ?

Ninavyojua mimi ni kwamba dini ni jambo la kibinadamu kumuelekea Mungu. Sio jambo la kimungu kumuelekea binadamu. Kama ninakosea kwenye uelewa naomba kufahamishwa.

Haya hiyo dini ya Mungu kwa mujibu wako ni ipi ?
Uislam,
Ukristo
Hindu
Budha
Au dini za kiafrika ?

Na hata ukisema moja kati ya hizo hapo juu ndio dini ya Mungu, haifuti ukweli kwamba hizo zinazobakia nazo pia ni "dini".
Vinginevyo uwe mgeni kabisa hapa duniani, yaani ndio unawasili muda huu kwaiyo hujui yanayoendelea kuhusu dini na hata ukasema ipo dini moja tu.

Kumbuka hoja hapa sio "ni ipi dini ya kweli". Hoja ni duniani kuna dini zaidi ya moja ama la, maana mzizi wa mjadala huu ni kwamba sisi waafrika kuna dini fulani na fulani tuliletewa kutoka kwa wenzetu weupe. (Kama umefuatilia mada toka mwanzo).
 
"Dini ya Mungu" ni dini ipi ?

Ninavyojua mimi ni kwamba dini ni jambo la kibinadamu kumuelekea Mungu. Sio jambo la kimungu kumuelekea binadamu. Kama ninakosea kwenye uelewa naomba kufahamishwa.

Haya hiyo dini ya Mungu kwa mujibu wako ni ipi ?
Uislam,
Ukristo
Hindu
Budha
Au dini za kiafrika ?

Na hata ukisema moja kati ya hizo hapo juu ndio dini ya Mungu, haifuti ukweli kwamba hizo zinazobakia nazo pia ni "dini".
Vinginevyo uwe mgeni kabisa hapa duniani, yaani ndio unawasili muda huu kwaiyo hujui yanayoendelea kuhusu dini na hata ukasema ipo dini moja tu.

Kumbuka hoja hapa sio "ni ipi dini ya kweli". Hoja ni duniani kuna dini zaidi ya moja ama la, maana mzizi wa mjadala huu ni kwamba sisi waafrika kuna dini fulani na fulani tuliletewa kutoka kwa wenzetu weupe. (Kama umefuatilia mada toka mwanzo).

Soma kwa kutafakari nilichoandika. Nimesema, na hapa nakariri tena, kwamba DINI ni moja tu ya Mungu, na ndiyo dini ya kweli, safi. Usiniwekee midomoni mambo ambayo sijayatamka.

Pia, tofautisha kati ya mitazamo na mafundisho na mapokeo ya wanadamu na DINI ya Mungu ya kweli ambayo kimsingi ina-transcend miapaka ya mitazamo na fikra za wanadamu, rangi, hali, hadhi na maeneo ya kijiografia.

Nilisema hapo mwanzo DINI ya Mungu haina mipaka na wala si lazima wakati wote mtu afundishwe na mtu mwingine ili aifahamu.

Please, never call apples mangoes!
 
Soma kwa kutafakari nilichoandika. Nimesema, na hapa nakariri tena, kwamba DINI ni moja tu ya Mungu, na ndiyo dini ya kweli, safi. Usiniwekee midomoni mambo ambayo sijayatamka.

Pia, tofautisha kati ya mitazamo na mafundisho na mapokeo ya wanadamu na DINI ya Mungu ya kweli ambayo kimsingi ina-transcend miapaka ya mitazamo na fikra za wanadamu, rangi, hali, hadhi na maeneo ya kijiografia.

Nilisema hapo mwanzo DINI ya Mungu haina mipaka na wala si lazima wakati wote mtu afundishwe na mtu mwingine ili aifahamu.

Please, never call apples mangoes!
Uwe na asubuhi njema mkuu.
 
Mkalimani wetu leo anatafasiri lugha ya Kifaransa ndani ya Ikulu tena mbele ya Rais na Mabalozi wa mataifa ya nje. Lakini Kifaransa kinaonekana kumpiga chenga kidogo anakaa kimya na mabalozi wanacheka . Ila yote kwa yote anajitahidi https://t.co/3deNOCrKgt

Jana tulijadili hapa.

Muda sio mrefu, mkalimani akafanya tofauti na matarajio ya wengi.
 
Mkalimani wetu leo anatafasiri lugha ya Kifaransa ndani ya Ikulu tena mbele ya Rais na Mabalozi wa mataifa ya nje. Lakini Kifaransa kinaonekana kumpiga chenga kidogo anakaa kimya na mabalozi wanacheka . Ila yote kwa yote anajitahidi https://t.co/3deNOCrKgt

Jana tulijadili hapa.

Muda sio mrefu, mkalimani akafanya tofauti na matarajio ya wengi.


Ngoja tufatilie
 
Back
Top Bottom