Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Hoja yako ni mufilisi.
Eti hoja mufilisi... hoja mufilisi au HUELEWI!!
Huwezi kutenganisha Urais alioupata Samia bila kuweka Uzanzibari wake.
Kwahiyo kama angekuwa amegombea, ndo angeweza kuongoza mambo ya bara yasiyo ya muungano?!

REMEMBER, kama angegombea usingeangaliwa u-ZNZ wake bali Utanzania wake!!

Na kwa mawazo yako, kwavile hakugombea basi mamlaka yake yanakuwa tofauti kulinganisha kama angegombea wakati anatumia katiba ile ile na sheria zile zile?! Kwamba, kwavile ametokea kuwa VP, basi urais wake hauwezi kuwa kama yule ambae aligombea?!
Katiba imetamka, Rais akifariki, Makamu( ambaye ni lazima atoke Zanzibar) anarithi kiti. Sasa unatenganishaje haya mawili.
Sio kutenganisha... niliweka wazi mapema kwa sababu nilishashuku kwamba huenda unau-judge urais wake sio kama rais bali kama rais aliyekuja kuwa rais akitokea kuwa VP!

Unashindwa kufahamu kwamba, a moment alipoapishwa, huyu akawa rais na u-VP wake ukakoma hapo!

Na kwavile akaja kuwa rais, ana wajibu na mamlaka ya kuhudumu kama rais bila kuangalia kama alisimama majukwaani kuomba achaguliwe kuwa rais, au vinginevyo!

Muhimu ni kwamba, urais wake ni halali kwa mujibu wa katiba!
Lakini hoja yangu sio Samia kuwa Rais wa JMT. Hoja yangu ni Samia kuongoza mambo ambayo siyo ya muungano as per constitution. Over!!!!!
Na nimeshakuambia, sifa ya mtu kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kwa mhusika kuwa raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano, PERIOD!

Na hakuna popote kwenye katiba panaposema rais aliyechaguliwa majukumu yake ni haya, na yule ambae ameingia akitokea kuwa VP, majukumu yake ni haya!

Na hakuna inaposema Rais wa Jamhuri anayetokea ZNZ majukumu yake ni haya na yule anayetokea bara, majukumu yake ni haya!

Na katiba haijasema kwa sababu hicho kingekuwa ni kiroja!!
 
Hoja ni kwamba, Tumekubaliana kuungana kwenye (mf.) Mambo ya Nje na Uhamiaji, lakini mambo ya Ujenzi na Maji hatujakubalina kuungana.

Sasa Iweje zao la muungano kutoka upande wa pili wa muungano aje kuongoza kwa mambo ya Ujenzi na Maji ambayo siyo ya muungano?

Mantiki iko wapi hapa??? Nn shida kuelewa hoja hii
Hatujaanza leo wala jana kulitumia zao la muungano kwa faida ya wote.

Makamu wa JK alikuwa Profesa Gharib, lolote lingempata JK Profesa angemalizia muda uliobaki.

Ndio aina ya muungano tulionao tuna haki sawa.
 
You could have raised that query by then, ila kwa sasa usinipangie cha kuuliza. Baki kwenye hoja yangu, ila usinipangie cha kuuliza sasa au kwa nini sikuiliza kabla.
Tuwe wapole tu huyu Mama ndio rais wetu kuelekea 2025 na Mpango makamu wake.

Nafasi ya urais haikubaliani na ombwe hata siku moja. JPM alipolala usingizi wa milele yule aliyetembea nae muda wote wakati wa kampeni ndio kavaa viatu vyake.

Ni takwa la kikatiba hayawi mapenzi ya mtu binafsi.
 
Sasa una hakika gani kwamba nilikuwepo kipindi cha Mzee Ruksa? Au, what if IQ za watu wa sasa zimeongezeka kuliko kipindi chenu hicho?

Kama wewe mtu mzima hukuwa na akili za kuhoji kipindi hicho ukiwa kijana, ndo hutaki sisi vijana wa sasa tuhoji?

Oooh please!!!
Wewe ni mfinyu kiakili na bado ni mtoto sababu kwanza inaonekana kabla hujaleta hii hoja hukusumbua kichwa chako kujiuliza maswali. Hoja yako kwa sasa haina mashiko kutokana na katiba tuliyonayo ambayo haiwezi kuondoa uhalali wa mama kuwa Rais. Aidha ninachokiona hapa kwenye hoja yako ni mama kuwa Rais, sivyo ungehoji kwa nini mzee Ruksa alipelekwa Ikulu 1985-1995 kwa katiba hii hii ambayo leo unaiona mbovu. Sasa mshachelewa Mama Samia kwa sasa ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa katiba hii unayoiona leo ni mbaya baada ya kifo cha Dikteta Magufuri. Nakushauri kakae na mkeo mjue maisha yataendaje
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Mzee nilikuwa sijakuelewa kutokana heading ila nimesoma mara mbili mbili nimekuelewa. Kudos
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Suluhisho ni tatu au moja basi
 
Kwani Magufuli alikuwa anawatawala hadi mambo yenu ambayo sio ya Muungano??.
Hapa issue ni kuwa hatutaki kutawaliwa na Mzanzibari hadi kwenye mambo ambayo sio ya Muungano.huyo Ali Hassan ana bahati watu wengi walikuwa hawana shule.
siyo kweli, G55 ilikuwa 1993 wakati wa utawala wa Mwinyi Ali Hassan
 
Wewe unajikanganya hapa, kama unasema hakuna anayepinga Bi Mkubwa kutawala Tanzania hii hoja kwa nini umeileta hapa? Na kwa nini umeileta baada ya kifo cha Dikteta ?, na kwa nini hukuleta hoja sababu ipi CCM imemteua VP mwenye asili ya zanzibar, je ulikuwa hujui kama Rais atashindwa kutimiza majukumu yake kwa ugonjwa au kifo makamu wake ndiye ataapishwa kuwa Rais. Wewe hilo ulikuwa hulijui? Na kumbuka katiba ya mzee warioba ilipendekeza mfumo wa serikali tatu lakini haikupendekeza asili ya mtu ametokea wapi sababu ya kuepusha ubaguzi, kumbuka pengine labda utoto tu unakusumbua kule Zanzibar Raia wengi wana asili ya Bara ambao walipelekwa kulima mashamba ya karafuu pemba ambayo yalimilikiwa na waarabu. Kifupi Mwl. Nyerere ndiye aliyemshawishi Hayati Mzee karume waungane baada ya karume kuomba msaada wa kuunganisha tabaka mbili la wapemba na waunguja ambao wana asili ya bara, suala la vita baridi ilikuwa ni kisingizio tu. Na baada kuondolewa utawala wa sultan Jamshid bin Abdulla mwaka 1963 Mzee karume aliwataka Wazanzibar weusi na weupe (waarabu) waoane ili kuondoa chuki baina yao iliyotokana na kukandamizwa kwa watu weusi. Hivyo kwa muktadha wa huko tulikotoka hakuna mtu anayeitwa mzanzibar wala mtanganyika wote sisi ni waTz. Hoja yako haina mashiko bali unataka kutugombanisha

Acha uzwazwa, sasa umejibu hoja au umeleta historia?

Hivi ninyi kizazi cha 70 mnashida gani? Mbona mnaonekana wote ni mburulaz?

Changia hoja kama huna soma na pita kimya
 
Wewe unajikanganya hapa, kama unasema hakuna anayepinga Bi Mkubwa kutawala Tanzania hii hoja kwa nini umeileta hapa? Na kwa nini umeileta baada ya kifo cha Dikteta ?, na kwa nini hukuleta hoja sababu ipi CCM imemteua VP mwenye asili ya zanzibar, je ulikuwa hujui kama Rais atashindwa kutimiza majukumu yake kwa ugonjwa au kifo makamu wake ndiye ataapishwa kuwa Rais. Wewe hilo ulikuwa hulijui? Na kumbuka katiba ya mzee warioba ilipendekeza mfumo wa serikali tatu lakini haikupendekeza asili ya mtu ametokea wapi sababu ya kuepusha ubaguzi, kumbuka pengine labda utoto tu unakusumbua kule Zanzibar Raia wengi wana asili ya Bara ambao walipelekwa kulima mashamba ya karafuu pemba ambayo yalimilikiwa na waarabu. Kifupi Mwl. Nyerere ndiye aliyemshawishi Hayati Mzee karume waungane baada ya karume kuomba msaada wa kuunganisha tabaka mbili la wapemba na waunguja ambao wana asili ya bara, suala la vita baridi ilikuwa ni kisingizio tu. Na baada kuondolewa utawala wa sultan Jamshid bin Abdulla mwaka 1963 Mzee karume aliwataka Wazanzibar weusi na weupe (waarabu) waoane ili kuondoa chuki baina yao iliyotokana na kukandamizwa kwa watu weusi. Hivyo kwa muktadha wa huko tulikotoka hakuna mtu anayeitwa mzanzibar wala mtanganyika wote sisi ni waTz. Hoja yako haina mashiko bali unataka kutugombanisha
Anavyoandika kuhusu wazanzibari utadhani hawana uhusiano kabisa na watu wa huku bara.

Hajui kuwa wajomba na baba wadogo wa huyo Rais wa sasa wana asili ya huku.

Hajui historia ya Karume kuwa asili yake ni huku bara.

Akiambiwa kuwa hii mada ina ubaguzi ndani yake analeta ubishi wakati kila kitu kipo bayana kabisa.
 
Anavyoandika kuhusu wazanzibari utadhani hawana uhusiano kabisa na watu wa huku bara.

Hajui kuwa wajomba na baba wadogo wa huyo Rais wa sasa wana asili ya huku.

Hajui historia ya Karume kuwa asili yake ni huku bara.

Akiambiwa kuwa hii mada ina ubaguzi ndani yake analeta ubishi wakati kila kitu kipo bayana kabisa.
Baadae ataanza ya kanda, maeneo fulani weshatoa maraisi fulani ila bado maeneo fulani..


Alotupiga zongo keshafariki..... Sisi vijana na wazee wa nchi hii hatuna sera ya nchi , bali matakwa ya raisi wa zamu, ndo maana unakuta mijadala kama hii imejaa humu, isiyo na tija yoyote kwa umma na maendeleo ya Tanzania.
 
Iko hivi, hatuwezi kuacha kuhoji mambo ya muungano kwa vitisho kutoka Serikalini.

Jambo la msingi tuhoji kwa hekima na busara. Kwani huu Muungano umekua Biblia au Msahafu kwamba usihojiwe??

Huyo VP mwenyewe ametokana na Katiba ambayo ndiyo tuna raise query zake hapa.

Uzalendo sio kuogopa kuhoji mapungufu yaliyopo waziwazi.

No, Never
Nimeielewa concern yako. Ninachosema ni kuwa hakuna kipya utakacholeta hapa JF kuhusu mapungufu ya muungano ambacho hakikuwahi kujadiliwa.
Fikiria, hata Rais wa kwanza wa Zanzibar naye alihoji kuhusu baadhi ya mambo ambayo aliona yanaminya uhuru (autonomy) wa Zanzibar. Hakuwahi kupewa jibu muafaka hadi anafariki.
Mwanzoni ilikuwa ni Rais wa kwanza wa JMT aliyekuwa na “stranglehold” kwenye suala la muungano; hakuna aliyeweza kuhoji muungano mbele ya Nyerere.
Baadaye ni CCM kama chama kimegundua kuwa muungano ni kete yake muhimu kujihakikishia madaraka ya kisiasa na ki-dola katika pande zote mbili za muungano. Pia kuituliza Zanzibar. Wabunge wa Zanzibar wanajaza viti na kuongeza ruzuku.
Halafu, imagine Zanzibar ingekuwa nchi huru, chama tawala cha enzi zile, ASP, kingeshang’olewa madarakani siku nyingi bila msaada wa dola ya “Tanganyika”. Na kuna uwezekano mkubwa kuwa bila usimamizi wa Tanganyika, Zanzibar ingekuwa kisiwa cha vurugu mechi kila wakati.
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Yaani pesa za Tanganyika au za muungano?
 
Tuelewe kwamba Zanzibar ilipata Uhuru wake kutoka kwa Waingereza 1963 lakini wazalendo walitaka kumuondoa Sultan na walifanikiwa kufanya hivyo mwaka1964.

Sultan alikimbilia Uingereza lakini nchi yake ya asili yaani Oman ilikua tayari kumpa msaada wa kijeshi arudi Zanzibar. Wazalendo waliomba msaada Bara na huu muungano kuzaliwa.

Wazalendo gani hao unaowakusudia? Mana Muungano ulikua ni wa Karume na Nyerere hakuna mwengne aliyeshirikishwa, Karume hakushauriana na hata baraza lake la mawaziri.
Hawa majamaa nchi walizifanya milki yao na ndio matunda yake haya. Kuendelea kuwatukuza wapuuzi kama hawa ni kujizidishia laana tu
 
Nimeielewa concern yako. Ninachosema ni kuwa hakuna kipya utakacholeta hapa JF kuhusu mapungufu ya muungano ambacho hakikuwahi kujadiliwa.
Fikiria, hata Rais wa kwanza wa Zanzibar naye alihoji kuhusu baadhi ya mambo ambayo aliona yanaminya uhuru (autonomy) wa Zanzibar. Hakuwahi kupewa jibu muafaka hadi anafariki.
Mwanzoni ilikuwa ni Rais wa kwanza wa JMT aliyekuwa na “stranglehold” kwenye suala la muungano; hakuna aliyeweza kuhoji muungano mbele ya Nyerere.
Baadaye ni CCM kama chama kimegundua kuwa muungano ni kete yake muhimu kujihakikishia madaraka ya kisiasa na ki-dola katika pande zote mbili za muungano. Pia kuituliza Zanzibar. Wabunge wa Zanzibar wanajaza viti na kuongeza ruzuku.
Halafu, imagine Zanzibar ingekuwa nchi huru, chama tawala cha enzi zile, ASP, kingeshang’olewa madarakani siku nyingi bila msaada wa dola ya “Tanganyika”. Na kuna uwezekano mkubwa kuwa bila usimamizi wa Tanganyika, Zanzibar ingekuwa kisiwa cha vurugu mechi kila wakati.
Siasa za machoni huwa tofauti na zile za mbali na macho.

Mtu akitazama taratibu za kisheria zinazoandikwa vitabuni anaweza akadhani maisha halisi yapo hivyo hivyo.

Muungano wetu tangu mwanzo ulikuwa na mazingira yenye kujitofautisha na miungano mingine. Na pande zote mbili zimekuwa zikielewa ni kwanini hali ipo kama ilivyo.
 
Wazalendo gani hao unaowakusudia? Mana Muungano ulikua ni wa Karume na Nyerere hakuna mwengne aliyeshirikishwa, Karume hakushauriana na hata baraza lake la mawaziri.
Hawa majamaa nchi walizifanya milki yao na ndio matunda yake haya. Kuendelea kuwatukuza wapuuzi kama hawa ni kujizidishia laana tu
Waulize wakubwa kiumri waliokuwepo wakati huo ili uweze kupata kuyajua mengi yenye manufaa.

Tulikuwa na dunia mbili ndani ya moja, ile ya kibepari na kijamaa na zote zilikuwa na mivutano mingi.

Walipoamua kuungana walitazama masuala kama hayo. Haikuwa dunia kama hii ya sasa ya simu za viganjani.
 
Back
Top Bottom