Je, Rais Magufuli atahudhuria kikao cha UN General Assembly cha mwaka huu?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,484
51,058
Kikao cha UN General assembly kinafanyika tena mwezi wa tisa mwaka huu kama ilivyo ada

Ni mwaka wa nne huu wa utawala wa Rais Magufuli hajawahi kusafiri kutoka nje ya Afrika, tofauti na watangulizi wake, Mheshimiwa Magufuli hajahudhuria kikao hata kimoja cha UN General assembly.
Kikawaida vikao vya General assmebly ni vikao vyenye hadhi ya wakuu wa nchi ambapo mambo mengi huzungumzwa pale lakini ukiacha mbali na hapo huwa ni nafasi nzuri kwa mkuu wa nchi mmoja kupata nafasi ya kuongea na kukubaliana mambo mengi ya maendeleo na wakuu wenzie wa nchi mbalimbali.

Kwa sasa mathalani zao letu la korosho limeyumba, huu ulikuwa ni muda muafaka wa raisi Magufuli kuongea na wakuu wenzie wenye viwanda na masoko ya korosho kuona Tanzania inaweza kunufaika vipi na fursa zilizoko kwao.

Lakini pia nchi yetu inahitaji uwekezaji mbalimbali wa mitaji, hii ni nafasi ya kukutana na wafanyabiashara wakubwa ambao hufunga safari kipindi hiki ili waweze kukutana na viongozi wa nchi mbalimbali kuzungumza masuala ya uwekezaji.

Pia kwa kuwa nchi yetu ina utalii basi hiyo pia ni fursa nzuri ya kuongea na wadau wa utalii na kuona namna gani tunaweza kuleta watalii wengi zaidi.

Swali langu ni kwamba Miaka minne Mheshimiwa Raisi hajaenda kukutana na Kiongozi yeyote wa Taifa kubwa na wala hajahudhuria kikao chochote cha UN General assembly.

Je safari hii itaenda?
 
Kikao cha UN General assembly kinafanyika tena mwezi wa tisa mwaka huu kama ilivyo ada

Ni mwaka wa nne huu wa utawala wa Rais Magufuli hajawahi kusuafiri kutoka nje ya Afrika, tofauti na watangulizi wake, Mheshimiwa Magufuli hajahudhuria kikao hata kimoja cha UN General assembly.
Kikawaida vikao vya General assmebly ni vikao vyenye hadhi ya wakuu wa nchi ambapo mambo mengi huzungumzwa pale lakini ukiacha mbali na hapo huwa ni nafasi nzuri kwa mkuu wa nchi mmoja kupata nafasi ya kuongea na kukubaliana mambo mengi ya maendeleo na wakuu wenzie wa nchi mbalimbali.

Kwa sasa mathalani zao letu la korosho limeyumba, huu ulikuwa ni muda muafaka wa raisi Magufuli kuongea na wakuu wenzie wenye viwanda na masoko ya korosho kuona Tanzania inaweza kunufaika na fursa zilizoko kwao.

Lakini pia nchi yetu inahitaji uwekezaji mbalimbali wa mitaji, hii ni nafasi ya kukutana na wafanyabiashara wakubwa ambao hufunga safari kipindi hiki ili waweze kukutana na viongozi wa nchi mbalimbali kuzungumza masuala ya uwekezaji.

Pia kwa kuwa nchi yetu ina utalii basi hiyo pia ni fursa nzuri ya kuongea na wadau wa utalii na kuona namna gani tunaweza kuleta watalii wengi zaidi.

Swali langu ni kwamba Miaka minne Mheshimiwa Raisi hajaenda kukutana na Kiongozi yeyote wa Taifa kubwa na wala hajahudhuria kikao chochote cha UN General assembly.

Je safari hii itaenda?

Ndio kitu mnachokumbuka na kupigania kirudi tena. Zile safari za kila mwezi za Ulaya na Marekani. Kuhudhuria kuanzia mkutano wa kunguni, nzi, mbu na hata viroboto. Mnaweza kutuonyesha kitu gani kikubwa kilifanyika mpaka muanze kutuaminisha kwamba bila kwenda huko kwenye hiyo mikutano tunakosa kitu kikubwa?
 
Hajui lugha yoyote ya huko duniani huyu atasalimiana na nani? Atabakia bubu muda wote wa kikao. Kwanza hana hata gestures za wanadiplomasia, bora abaki hapa hapa na Bashite asije akatuabisha huko nje
 
Hajui lugha yoyote ya huko duniani huyu atasalimiana na nani? Atabakia bubu muda wote wa kikao. Kwanza hana hata gestures za wanadiplomasia, bora abaki hapa hapa na Bashite asije akatuabisha huko nje

Ndio usomi wetu ulipofika ukomo. Kuongea kiingereza, hata kama unachoongea ni shit tupu. Nchi yetu ni Zaidi ya mtu mmoja ambaye tunapenda kuona kama ndio sababu ya kila tatizo letu. Matatizo yetu hayapo mbali na sisi. yapo ndani ya kila mmoja wetu kwa nafasi yake. Unless tunayaanza hayo, kiingereza tutaongea lakini hakitupi status yoyote popote pale.
Hizi kelele ambazo ndani ni empty, hazimzuii tembo kunywa maji. Tuwe strategic
 
Ndio usomi wetu ulipofika ukomo. Kuongea kiingereza, hata kama unachoongea ni shit tupu. Nchi yetu ni Zaidi ya mtu mmoja ambaye tunapenda kuona kama ndio sababu ya kila tatizo letu. Matatizo yetu hayapo mbali na sisi. yapo ndani ya kila mmoja wetu kwa nafasi yake. Unless tunayaanza hayo, kiingereza tutaongea lakini hakitupi status yoyote popote pale.
Hizi kelele ambazo ndani ni empty, hazimzuii tembo kunywa maji. Tuwe strategic
Mbona unaongea kwa woga? Funguka wewe acha kumbwelambwela! Tamka kimamlaka...nini hoja yako?
 
Mbona unaongea kwa woga? Funguka wewe acha kumbwelambwela! Tamka kimamlaka...nini hoja yako?
Nimuogope nani? Kuna lugha mtu akiongea unajua anasema kutokea nafasi gani. Uko shimoni. Hizi ni lugha za mkosaji. Toka lini kiingereza kimekuwa issue ya muhimu kwa political leaders?
Hata kama anajua kiingereza, akienda Russia na Ufaransa au China anafanyaje? Tunajua nguvi dola iliyonayo kwenye mambo ya diplomasia?
 
Nimuogope nani? Kuna lugha mtu akiongea unajua anasema kutokea nafasi gani. Uko shimoni. Hizi ni lugha za mkosaji. Toka lini kiingereza kimekuwa issue ya muhimu kwa political leaders?
Hata kama anajua kiingereza, akienda Russia na Ufaransa au China anafanyaje? Tunajua nguvi dola iliyonayo kwenye mambo ya diplomasia?
Eeeh! Kuna aliyekitaja kingereza hapa? Nimesema jiwe hajui lugha yoyote ya duniani huko. Iwe kichina, kirusi, kingereza, kijermani, kihispania ama kiyunani. Hajui.!!
 
Eeeh! Kuna aliyekitaja kingereza hapa? Nimesema jiwe hajui lugha yoyote ya duniani huko. Iwe kichina, kirusi, kingereza, kijermani, kihispania ama kiyunani. Hajui.!!

Msijidanye nyie waja. Kuongoza nchi kama ingekuwa ndio kuongoza nyumba ndogo tayari mngeshakuwa viongozi. Haikushindikana kwa bahati mbaya. Na haitakaa kuja kutokea. Mtasubiri mpaka mtaenda kwenye yale mashimo tuliyoumbiwa waja wote
 
Ndio kitu mnachokumbuka na kupigania kirudi tena. Zile safari za kila mwezi za Ulaya na Marekani. Kuhudhuria kuanzia mkutano wa kunguni, nzi, mbu na hata viroboto. Mnaweza kutuonyesha kitu gani kikubwa kilifanyika mpaka muanze kutuaminisha kwamba bila kwenda huko kwenye hiyo mikutano tunakosa kitu kikubwa?

Mkuu, hata Nyerere alikuwa akienda hizi safari za UN, si mnasema Magufuri kama Nyerere, vipi tena basi kwenye nyanja hii muhimu ya Diplomasia mbona hafuati nyayo?
 
Kikao cha UN General assembly kinafanyika tena mwezi wa tisa mwaka huu kama ilivyo ada

Ni mwaka wa nne huu wa utawala wa Rais Magufuli hajawahi kusafiri kutoka nje ya Afrika, tofauti na watangulizi wake, Mheshimiwa Magufuli hajahudhuria kikao hata kimoja cha UN General assembly.
Kikawaida vikao vya General assmebly ni vikao vyenye hadhi ya wakuu wa nchi ambapo mambo mengi huzungumzwa pale lakini ukiacha mbali na hapo huwa ni nafasi nzuri kwa mkuu wa nchi mmoja kupata nafasi ya kuongea na kukubaliana mambo mengi ya maendeleo na wakuu wenzie wa nchi mbalimbali.

Kwa sasa mathalani zao letu la korosho limeyumba, huu ulikuwa ni muda muafaka wa raisi Magufuli kuongea na wakuu wenzie wenye viwanda na masoko ya korosho kuona Tanzania inaweza kunufaika na fursa zilizoko kwao.

Lakini pia nchi yetu inahitaji uwekezaji mbalimbali wa mitaji, hii ni nafasi ya kukutana na wafanyabiashara wakubwa ambao hufunga safari kipindi hiki ili waweze kukutana na viongozi wa nchi mbalimbali kuzungumza masuala ya uwekezaji.

Pia kwa kuwa nchi yetu ina utalii basi hiyo pia ni fursa nzuri ya kuongea na wadau wa utalii na kuona namna gani tunaweza kuleta watalii wengi zaidi.

Swali langu ni kwamba Miaka minne Mheshimiwa Raisi hajaenda kukutana na Kiongozi yeyote wa Taifa kubwa na wala hajahudhuria kikao chochote cha UN General assembly.

Je safari hii itaenda?
Siamini kama UN General Assembly ni muarobaini wa mahitaji ama matatizo uliyoolozesha.
UN haina meno,wenye meno ni mataifa makubwa machache tajiri.nchi kama zetu bila juhudi binafsi hazitasonga mbele,ni kazi za wasaidizi wa rais kuyafanya hayo usemayo,wakiwemo mabalozi
 
Back
Top Bottom