Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Wakati wa kumuapisha Waziri wa mambo ya ndani, Kangi Lugora, alieleza kwa kirefu namna ambavyo baadhi ya wasaidizi wake anaowateua namna ambavyo hawamuelewi anachokitaka katika Utendaji wao.
Hakufafanua zaidi ni nini hiko anachokitaka kutoka kwa wasaidizi wake
Lakini kutokana na teuzi za Jana, nadhani wengi watakuwa wamemuelewa......
Amemteua Ali Hapi na kumpandisha cheo kuwa RC wa Iringa
Tukumbuke pia kuwa huyu Ali Hapi aliwahi kumweka ndani kwa Masaa 48, mbunge wa kuchaguliwa na wananchi, mbunge wa Kawe, kwa tiketi ya Chadema, Halima Mzee
Tusisahau pia kuwa wilaya yake imefanya uchaguzi mdogo hivi karibuni, uchaguzi ambao umelalamikiwa sana na upinzani kuwa haukuwa huru na haki
Amemteua pia Jerry Muro kuwa DC mpya wa Arumeru
Tukumbuke kuwa huyu Jerry Muro anaaminika kuwa anapenda kutumia "mkono wa chuma" katika mambo yake mengi anayoyafanya
Tukumbuke pia huyo Jerry Muro anamrithi DC Alexander Mnyeti ambaye naye alipandishwa cheo na kuwa RC wa Manyara kutokana na kazi "nzuri" aliyofanya hapo Arumeru.
Tukumbuke kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema, Joshua Nassari aliwaonyesha waandishi wa habari clip ya video inayomwomyesha Mkuu huyo wa wilaya, Alexander Mnyeti, "akiwanunua" madiwani wa Chadema
Je uteuzi wa jana wa Mheshimiwa Rais unamaanisha nini?
Kwa jinsi nilivyouelewa Mimi ni kuwa uteuzi huo "unawahamasisha" viongozi wa upinzani wahamie CCM, ambako kuna "uhakika" wa uteuzi wa chap chap katika nafasi za Uongozi wa Umma!
Na wale walioko ndani ya CCM, nilichojifunza ni kuwa wateule hao wa Rais, hususani katika maeneo ambayo yana mbunge na madiwani wengi wa upinzani, wamechaguliwa wale ambao wanaweza kuutumia vyema "mkono wa chuma"
Je "mkono wa chuma" ndicho alichomaanisha Mheshimiwa Rais aliposema kuwa wasaidizi wake wengi hawamuelewi anataka nini katika serikali yake??
Hakufafanua zaidi ni nini hiko anachokitaka kutoka kwa wasaidizi wake
Lakini kutokana na teuzi za Jana, nadhani wengi watakuwa wamemuelewa......
Amemteua Ali Hapi na kumpandisha cheo kuwa RC wa Iringa
Tukumbuke pia kuwa huyu Ali Hapi aliwahi kumweka ndani kwa Masaa 48, mbunge wa kuchaguliwa na wananchi, mbunge wa Kawe, kwa tiketi ya Chadema, Halima Mzee
Tusisahau pia kuwa wilaya yake imefanya uchaguzi mdogo hivi karibuni, uchaguzi ambao umelalamikiwa sana na upinzani kuwa haukuwa huru na haki
Amemteua pia Jerry Muro kuwa DC mpya wa Arumeru
Tukumbuke kuwa huyu Jerry Muro anaaminika kuwa anapenda kutumia "mkono wa chuma" katika mambo yake mengi anayoyafanya
Tukumbuke pia huyo Jerry Muro anamrithi DC Alexander Mnyeti ambaye naye alipandishwa cheo na kuwa RC wa Manyara kutokana na kazi "nzuri" aliyofanya hapo Arumeru.
Tukumbuke kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema, Joshua Nassari aliwaonyesha waandishi wa habari clip ya video inayomwomyesha Mkuu huyo wa wilaya, Alexander Mnyeti, "akiwanunua" madiwani wa Chadema
Je uteuzi wa jana wa Mheshimiwa Rais unamaanisha nini?
Kwa jinsi nilivyouelewa Mimi ni kuwa uteuzi huo "unawahamasisha" viongozi wa upinzani wahamie CCM, ambako kuna "uhakika" wa uteuzi wa chap chap katika nafasi za Uongozi wa Umma!
Na wale walioko ndani ya CCM, nilichojifunza ni kuwa wateule hao wa Rais, hususani katika maeneo ambayo yana mbunge na madiwani wengi wa upinzani, wamechaguliwa wale ambao wanaweza kuutumia vyema "mkono wa chuma"
Je "mkono wa chuma" ndicho alichomaanisha Mheshimiwa Rais aliposema kuwa wasaidizi wake wengi hawamuelewi anataka nini katika serikali yake??
Last edited: