Omusolopogasi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 7,105
- 18,004
Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kiamataifa, Prof. Kabudi aliongea na vyombo vya habari kuhusu Tanzania kujadiliwa na Kamati ya Bunge la Ulaya kuhusu kuminywa kwa demokrasia na matumizi ya pesa kutoka Jumuiya ya Ulaya kwa ajili ya virus vya korona.
Prof. Kabudi alitamba kuwa Tanzania ni nchi huru. Asichokijua Prof. Kabudi ni kuwa duniani kote hakuna nchi yenye uhuru wa kuua watu wake huku Jumuiya ya Kimataifa ikiangalia. Hakuna uhuru wa aina hiyo asilani. Katika ngazi ya familia, pia iko hivyo. Hakuna baba anayeweza kuua watoto wake huku akidai kuwa familia yake iko huru. Prof Kabudi aelewe kuwa baba anayeua watoto wake, anatenda kosa la mauaji kwa mujibu wa sheria za nchi. Nchi inayokandamiza watu wake na kuua inafanya kosa kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
Prof Kabudi, macho yakiwa kodo, alitamba kuwa “Watanzania” wanathamini sana utu na uhuru wao na hawatatishwa kwa vile hawajawahi kushindwa vita. Swali langu ni kuwa ni “Watanzania” wapi wanaoongelewa hapa? Je, anawazungumzia Watanzania wa kweli waliojitokeza kupiga kura zao tarehe 28 Okt 2020 ama kile kikundi cha mafia kilicho chafua uchaguzi huo kwa makusudi?
Je, ni kweli kuwa Watanzania wanaunga mkono kuporwa haki yao ya kuchagua viongozi wanao wataka? Ni kweli kuwa Watanzania milioni 60 walifurahia kitendo cha wagombea wa upinzani kuporwa fomu na kukamatwa na vyombo vya dola ili wagombea wa CCM akiwemo Kabudi, wapiti bila kupingwa? Je, ni kweli Watanzania walipenda uchaguzi uamuliwe na wapigakura wale wa tarehe 27 Okt 2020 kule Zanzibar? Je, ni kweli Watanzania milioni 60 walipenda mawakala wa vyama vya upinzani kufukuzwa katika vituo? Je, ni kweli kuwa Watanzania walifurahia kitendo cha kura kupigwa nyumbani na mahotelini na baadae kupenyezwa katika vituo zikiwa ziemebebwa kwenye mabegi na vikapu? Hawa “Watanzania” anaowaongelea Kabudi ni wapi.
Prof. Kabudi amejazwa kiburi na JWTZ, polisi na TISS kiasi cha kuona kuwa ni sawa kwa kikundi kidogo cha kimafia cha CCM kuamua matokeo ya uchaguzi kwa manufaa yao na kusema “Watanzania” wameamua. Na kwamba Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa wanatakiwa kutabasamu tu kana kwamba hakuna kitu kimetokea!
Prof. Kabudi ajue kuwa Watanzania wa kweli tunaililia haki yetu ya kuchagua viongozi tunaowataka wenyewe kupitia sanduku la kura. Kabudi asichanganye CCM na Watanzania. CCM ni kundi dogo sana miongoni mwa Watanzania milioni 60 ila tu lina majeshi yenye silaha za moto. Kama vikwazo vitaleta haki ya Watanzania milioni 60 kupiga kura na kuchagua viongozi wanao wataka bila ya kuamualia na jeshi, polisi, TISS, NECCM, Msajili wa Vyama, nk, na vije. Tunavisubiri kwa hamu kubwa.
Kweli huu ndio utu wa Mtanzania anaongelea Prof. Kabudi na kutoa macho kiasi kile huku akinyeshea microphone na mvua ya mate vile? Kwa hakika huu siyo utu wa Mtanzania. Ni utu wa CCM:
Prof. Kabudi alitamba kuwa Tanzania ni nchi huru. Asichokijua Prof. Kabudi ni kuwa duniani kote hakuna nchi yenye uhuru wa kuua watu wake huku Jumuiya ya Kimataifa ikiangalia. Hakuna uhuru wa aina hiyo asilani. Katika ngazi ya familia, pia iko hivyo. Hakuna baba anayeweza kuua watoto wake huku akidai kuwa familia yake iko huru. Prof Kabudi aelewe kuwa baba anayeua watoto wake, anatenda kosa la mauaji kwa mujibu wa sheria za nchi. Nchi inayokandamiza watu wake na kuua inafanya kosa kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
Prof Kabudi, macho yakiwa kodo, alitamba kuwa “Watanzania” wanathamini sana utu na uhuru wao na hawatatishwa kwa vile hawajawahi kushindwa vita. Swali langu ni kuwa ni “Watanzania” wapi wanaoongelewa hapa? Je, anawazungumzia Watanzania wa kweli waliojitokeza kupiga kura zao tarehe 28 Okt 2020 ama kile kikundi cha mafia kilicho chafua uchaguzi huo kwa makusudi?
Je, ni kweli kuwa Watanzania wanaunga mkono kuporwa haki yao ya kuchagua viongozi wanao wataka? Ni kweli kuwa Watanzania milioni 60 walifurahia kitendo cha wagombea wa upinzani kuporwa fomu na kukamatwa na vyombo vya dola ili wagombea wa CCM akiwemo Kabudi, wapiti bila kupingwa? Je, ni kweli Watanzania walipenda uchaguzi uamuliwe na wapigakura wale wa tarehe 27 Okt 2020 kule Zanzibar? Je, ni kweli Watanzania milioni 60 walipenda mawakala wa vyama vya upinzani kufukuzwa katika vituo? Je, ni kweli kuwa Watanzania walifurahia kitendo cha kura kupigwa nyumbani na mahotelini na baadae kupenyezwa katika vituo zikiwa ziemebebwa kwenye mabegi na vikapu? Hawa “Watanzania” anaowaongelea Kabudi ni wapi.
Prof. Kabudi amejazwa kiburi na JWTZ, polisi na TISS kiasi cha kuona kuwa ni sawa kwa kikundi kidogo cha kimafia cha CCM kuamua matokeo ya uchaguzi kwa manufaa yao na kusema “Watanzania” wameamua. Na kwamba Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa wanatakiwa kutabasamu tu kana kwamba hakuna kitu kimetokea!
Prof. Kabudi ajue kuwa Watanzania wa kweli tunaililia haki yetu ya kuchagua viongozi tunaowataka wenyewe kupitia sanduku la kura. Kabudi asichanganye CCM na Watanzania. CCM ni kundi dogo sana miongoni mwa Watanzania milioni 60 ila tu lina majeshi yenye silaha za moto. Kama vikwazo vitaleta haki ya Watanzania milioni 60 kupiga kura na kuchagua viongozi wanao wataka bila ya kuamualia na jeshi, polisi, TISS, NECCM, Msajili wa Vyama, nk, na vije. Tunavisubiri kwa hamu kubwa.
Kweli huu ndio utu wa Mtanzania anaongelea Prof. Kabudi na kutoa macho kiasi kile huku akinyeshea microphone na mvua ya mate vile? Kwa hakika huu siyo utu wa Mtanzania. Ni utu wa CCM: