Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,794
Hii ni mada hojaji... Ni mada ulizo... Ni mada swali... Tushirikiane kupata majibu..!!!
Hapo kabla ya awamu hii. Huko nyuma, kesi mbaya ilikuwa mauaji.. Kesi hii haina dhamana... Na watuhumiwa wakubwa wa ubambikaji(kusingiziwa mashtaka ya uongo) walikuwa ni police... Kwamba kama una bifu nao ama wamekukamata kwenye patrol zao na ukawavimbia sana, ukifikishwa selo unapewa kesi ya kichwa yaani ya mauaji.
Hii ilitokana kuwa na kesi nyingi za mauaji zisizo na watuhumiwa hivyo na kuwa na majalada open ya hizo kesi. Sambamba na hilo ubambikaji mwingine ukawa kwenye madawa ya kulevya.
Watu walichomekewa sana kete na misokoto ya bhangi, lakini uzuri wake wakati ule nyingi ya kesi hizi hazikuwa za kisiasa bali kwa sehemu kubwa mabifu ya mitaani huko kwenye jamii
Mambo yalianza kubadilika mwaka juzi kwenye juhudi za kusafisha uozo mkubwa uliokuwepo serikalini na taasisi zake.. Watu walikuwa wamepiga ndefu za kueleweka na wengi walipiga kupitia kalamu.. Na kwa sehemu kubwa walikuwa ni wafanyakazi serikalini wakishirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu
Asili ya uhujumu uchumi ni kampeni ya mwaka 1984 iliyofanywa na hayati Edward Moringe Sokoine aliyekuwa waziri mkuu kipindi hicho.. Kampeni iliyopata baraka zote za Hayati Mwl. J. K. Nyerere.
Kampeni ile iliwalenga wafanyabiashara.. Pesa ziliadimika mtaani na bank.. Bidhaa pia ziliadimika madukani. Serikali ikagundua kuwa ni mbinu ya wafabiashara kuficha bidhaa ziadimike kisha wauze kwa bei ya kuruka ili wapate faida kubwa.
Serikali kupitia waziri huyo Mkuu Sokoine ikatoa ultimatum pesa zisalimishwe bank na bidhaa zijazwe madukani.
Na kipindi kilichowekwa kikipita na ukafanyika msako ukakutwa na pesa nyingi ndani na bidhaa.. Kwanza utafilisiwa kisha utashtakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi.. Kilichotokea kwa waliokuwepo wakati ule wanakijua vema
Awamu hii kama nilivyotangulia kusema katika juhudi zake za kusafisha uozo serikalini, ndio ikaja na hili la uhujumu uchumi.. Kosa ambalo halina dhamana lakini baadae likaongezeka na kosa lingine lisilokuwa na dhamana pia.. Kosa la kutakatisha fedha haramu
Makosa haya mawili yakatumiwa vibaya dhidi ya wale waliokuwa na mitazamo kinzani ya kisiasa.. Ikawa sasa sio kupewa kesi ya kichwa tena ama unga bali ni uhujumu uchumi na kutakatisha fedha haramu..
Utaratibu wa kufungua kesi unajulikana... Lazima awepo mshtaki na mshtakiwa.. Ni mara chache police kuwa mshtaki na ikitokea hivyo anafanya kwa niaba ya serikali
Tumewasikia live viongozi wa KISIASA majukwaani wakiongea bila kificho na bila woga kuwa ukikataa kutii maagizo yao ama ukikinzana nao kimtazamo watakupa kesi ya uhujumu uchumi ama kutakatisha fedha ukaozee jela kwakuwa kesi hizi hazina dhamana
Tunapowatuhumu polisi kubambika kesi tusiwasahau na hawa viongozi wa KISIASA waliotamka kwa uwazi mchana kweupe na bila woga!
Jr
Hapo kabla ya awamu hii. Huko nyuma, kesi mbaya ilikuwa mauaji.. Kesi hii haina dhamana... Na watuhumiwa wakubwa wa ubambikaji(kusingiziwa mashtaka ya uongo) walikuwa ni police... Kwamba kama una bifu nao ama wamekukamata kwenye patrol zao na ukawavimbia sana, ukifikishwa selo unapewa kesi ya kichwa yaani ya mauaji.
Hii ilitokana kuwa na kesi nyingi za mauaji zisizo na watuhumiwa hivyo na kuwa na majalada open ya hizo kesi. Sambamba na hilo ubambikaji mwingine ukawa kwenye madawa ya kulevya.
Watu walichomekewa sana kete na misokoto ya bhangi, lakini uzuri wake wakati ule nyingi ya kesi hizi hazikuwa za kisiasa bali kwa sehemu kubwa mabifu ya mitaani huko kwenye jamii
Mambo yalianza kubadilika mwaka juzi kwenye juhudi za kusafisha uozo mkubwa uliokuwepo serikalini na taasisi zake.. Watu walikuwa wamepiga ndefu za kueleweka na wengi walipiga kupitia kalamu.. Na kwa sehemu kubwa walikuwa ni wafanyakazi serikalini wakishirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu
Asili ya uhujumu uchumi ni kampeni ya mwaka 1984 iliyofanywa na hayati Edward Moringe Sokoine aliyekuwa waziri mkuu kipindi hicho.. Kampeni iliyopata baraka zote za Hayati Mwl. J. K. Nyerere.
Kampeni ile iliwalenga wafanyabiashara.. Pesa ziliadimika mtaani na bank.. Bidhaa pia ziliadimika madukani. Serikali ikagundua kuwa ni mbinu ya wafabiashara kuficha bidhaa ziadimike kisha wauze kwa bei ya kuruka ili wapate faida kubwa.
Serikali kupitia waziri huyo Mkuu Sokoine ikatoa ultimatum pesa zisalimishwe bank na bidhaa zijazwe madukani.
Na kipindi kilichowekwa kikipita na ukafanyika msako ukakutwa na pesa nyingi ndani na bidhaa.. Kwanza utafilisiwa kisha utashtakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi.. Kilichotokea kwa waliokuwepo wakati ule wanakijua vema
Awamu hii kama nilivyotangulia kusema katika juhudi zake za kusafisha uozo serikalini, ndio ikaja na hili la uhujumu uchumi.. Kosa ambalo halina dhamana lakini baadae likaongezeka na kosa lingine lisilokuwa na dhamana pia.. Kosa la kutakatisha fedha haramu
Makosa haya mawili yakatumiwa vibaya dhidi ya wale waliokuwa na mitazamo kinzani ya kisiasa.. Ikawa sasa sio kupewa kesi ya kichwa tena ama unga bali ni uhujumu uchumi na kutakatisha fedha haramu..
Utaratibu wa kufungua kesi unajulikana... Lazima awepo mshtaki na mshtakiwa.. Ni mara chache police kuwa mshtaki na ikitokea hivyo anafanya kwa niaba ya serikali
Tumewasikia live viongozi wa KISIASA majukwaani wakiongea bila kificho na bila woga kuwa ukikataa kutii maagizo yao ama ukikinzana nao kimtazamo watakupa kesi ya uhujumu uchumi ama kutakatisha fedha ukaozee jela kwakuwa kesi hizi hazina dhamana
Tunapowatuhumu polisi kubambika kesi tusiwasahau na hawa viongozi wa KISIASA waliotamka kwa uwazi mchana kweupe na bila woga!
Jr