Je, nini maana ya kusoma na kuelimika?

Quetzal

JF-Expert Member
Dec 9, 2018
6,330
10,749
Wasomi wengi ni wezi wanaibia makampuni.

Wasomi wengi ni wapiga deal

Wasomi ni watakatishaji fedha

Wasomi Ndo washinda wanabet kwenye kamari

Wasomi Ndo wazinifu na wenye kusifia huu uchafu, kuhalalisha uchepukaji

Wasomi wengi hujaza mabaa na makumbi ya starehe wakilewa

Wasomi wengine hubaka nakusingizia walishindwa kuzuia tamaa za mwili.

Sijasema wasomi wote.

Ila vijana wana mentality ya kutusua maisha bila kujali njia ilimradi awe na gari na nyumba na amiliki pisikali.

Je, msomi bila Maadili binafsi atakuwa na msaada katika jamii Yake?
 
Wasomi wengi wana PhD lakini hawajui kiingereza. Kwani uongo? Bwana yule si mnamfahamu!
 
Siku tuna graduate na degree ya kubeti ajira hamna....
Utabet ukifika Miaka 36 . Unasema umekata tamaa unataka kujiua..

Inabidi TUBUNI namna yakufanya tuweze kupata kipato vinginevyo wasomi tutaonekana hatuna Maana..

Na kubet ni kamali ... Omba Mungu usiwe addicted.
 
Wasomi wengi wana PhD lakini hawajui kiingereza. Kwani uongo? Bwana yule si mnamfahamu!
...Mkuu tunazungumzia Maadili ya wasomi na sio kujua English.

English Yake inamtosha.. Kuna mtu anaongea English vibaya mno na Ni msomi Ila hataki kufanya kazi...analewa Asubuhi hadi jioni, sigara na Bangi.

Je elimu Yake Hapo Ni kujua kusema yes no TU.
 
Ila vijana wana mentality ya kutusua maisha bila kujali njia ilimradi awe na gari na nyumba na amiliki pisikali.
Mkuu, ninadhani takwimu (data) za utafiti huu ulikuwa na mlengo mmoja hasi (biased). Japokuwa kuna hoja fikirishi umewasilisha. Kulewa, kubaka, wizi na mengine mengi uliyoyaandika hapa yanahusisha ugo mkubwa sana wa kimaadili. Matharani kwangu mimi na jamii yangu kuiba ni kosa lakini kwa yule na jamii yake ni vyema kuiba na ni kipimo cha ujanja.

Na hizo pisikali ulotaja hapo ndiyo huwa chanzo cha mengi katika orodha yako nyuma ya pazia.
 
Mkuu, ninadhani takwimu (data) za utafiti huu ulikuwa na mlengo mmoja hasi (biased). Japokuwa kuna hoja fikirishi umewasilisha. Kulewa, kubaka, wizi na mengine mengi uliyoyaandika hapa yanahusisha ugo mkubwa sana wa kimaadili. Matharani kwangu mimi na jamii yangu kuiba ni kosa lakini kwa yule na jamii yake ni vyema kuiba na ni kipimo cha ujanja.

Na hizo pisikali ulotaja hapo ndiyo huwa chanzo cha mengi katika orodha yako nyuma ya pazia.
Nikweli hizi data. Nimechukua zaidi kwenye vyombo vya habari na Experience yangu...Wasomi ndo wanabuni namna za kutapeli Watu KILA kukicha...wasomi Wanatumia Elimu zao kuibia wateja na waajari wao katika Mabenki...

Wasomi ndo wapo mstari wa kutaka mafanikio yaharaka...hivyo hula rushwa na wengine wakiishia Jela..

Wasomi wetu kutaka mafanikio ya haraka ndo insababisha kufanya mambo Ajabu..

Lakini Hawa wasomi Somo la Ethics huwa hawalielewi au wanapuuza?
 
Hiyo research uliifanya wapi hadi uje kuchafua wasomi humu?
Wasomi kushtakiwa kwa kuomba rushwa makazini...Kama juzi hapa Doctor kashatkiwa kwa kuomba na kupokea Rushwa ya laki 3 ...ili amtibu MGONJWA

Je kusoma huku Ni kuelimika au Kukariri madesa TU...

Je Wewe Kama msomi Elimu yako itakusaidia au itakuangamiza na kukuta upo Jela na mwizi wa vifaranga vya kuku chotara
 
mada yako nzuri bt umeitia makoro koro mengi, kitu pekee unapaswa kujua ni kua kusoma na kuelimika ni kuongeza upeo wa maarifa bt upeo huo hauwezi kumzuia mtu kufanya starehe yeyote, HUKO KUSOMA NA KUELIMIKA hakuwezi kuondosha matamanio ya mwanadam ambayo ni nature, matamanio ambayo ndo hua chanzo cha ukosefu wa mwanadam YEYOTE, tizama hata maandiko yameeleza namna mitume walivyokengeuka na kumkosea muumba wao ajili ya natural desire, inshort binadam yeyote bila kujali kasoma au lah huponzwa na matamanio HAYA ambayo ndo hupelekea kukosea OVA
 
Back
Top Bottom