vukani
JF-Expert Member
- Dec 30, 2009
- 245
- 165
Kuna baadhi ya misemo inanitatiza, lakini naamini hapa kuna wajuzi wa lugha, ya Kiswahili ambao watanipatia msaada.
Ninachotaka kujua, Je nini asili au chanzo cha misemo hii kutumika?
Misemo yenyewe ni hii ifuatayo:
Haikufua dafu (Msemo huu hutumika zaidi pale mtu anapojaribu kitu kikashidikana, kwa mfano mtu anaweza kuumwa akanywa dawa fulani kisha ikashindwa kufanya kazi, anaweza kusema nimekunywa dawa Fulani lakini haikufua dafu-Tafsiri ni yangu)
Mungu sio Athumani (Huu msemo nao hutumika pale mtu anapokuwa amefanikiwam katika jambo ambalo hakulitarajia-Tafsiri ni yangu)
Hamadi Kibindoni (Msemo huu hutumika pale mtu anapokuwa amepata bahati ya kuokota kitu aua kupata kitu-Tafsiri ni yangu)
Kasimama pale kama mzungu wa reli (Msemo huu unatumika pale mtu anaposimama mahali muda mrefu bila kusogea, na ndo huambiwa kuwa amesimama kama mzungu wa reli-Tafsiri ni yangu)
Ninachotaka kujua, Je nini asili au chanzo cha misemo hii kutumika?
Misemo yenyewe ni hii ifuatayo:
Haikufua dafu (Msemo huu hutumika zaidi pale mtu anapojaribu kitu kikashidikana, kwa mfano mtu anaweza kuumwa akanywa dawa fulani kisha ikashindwa kufanya kazi, anaweza kusema nimekunywa dawa Fulani lakini haikufua dafu-Tafsiri ni yangu)
Mungu sio Athumani (Huu msemo nao hutumika pale mtu anapokuwa amefanikiwam katika jambo ambalo hakulitarajia-Tafsiri ni yangu)
Hamadi Kibindoni (Msemo huu hutumika pale mtu anapokuwa amepata bahati ya kuokota kitu aua kupata kitu-Tafsiri ni yangu)
Kasimama pale kama mzungu wa reli (Msemo huu unatumika pale mtu anaposimama mahali muda mrefu bila kusogea, na ndo huambiwa kuwa amesimama kama mzungu wa reli-Tafsiri ni yangu)