Msaada kwenye tuta,
Mimi nimekuwa katika ajira na mwajiri wangu mpya yapata mwaka sasa. Katika mkataba wa ajira, tulikubaliana mambo kadha wa kadha (mbali na mshahara), ni pamoja na marupurupu kwa ajili ya kodi ya nyumba, mawasiliano na usafiri.
Hata hivyo, tangu mwenzi wa kwanza katika kumtumikia, marupurupu hayo yameonekana kuwa ni hadithi tu, kila kukicha ni subiri na subiri. Mwaka waisha sasa. Binafsi, nahisi kutotendewa haki na kwa maana nyingine nachukulia suala hili ni mpango tu wa kuhujumu utendaji na ufanisi wangu katika kazi.
Baada ya kuwa nikifuatilia suala hili, pengine na hata kuonekana nakuwa bughudha, taratibu nilianza kuishiwa na hari ya kazi na pia kuanza kufikiria kutafuta ajira mpya.
Hivi punde nimepata wito kutoka kwa mwajiri mpya, ambaye agependa nijiunge naye mapema iwezekanavyo.
Swali langu la msingi ni je, naweza kuamua kuacha kazi kwa short notice? Moja pia kati ya makubaliano katika mkataba ni kutoa notice ya mwezi mmoja!
Naomba msaada kwa wenye kujua na kuwa na uzoefu na masuala haya ya haki za wafanyakazi na sheria kwa ujumla.
Ahsanteni
Mimi nimekuwa katika ajira na mwajiri wangu mpya yapata mwaka sasa. Katika mkataba wa ajira, tulikubaliana mambo kadha wa kadha (mbali na mshahara), ni pamoja na marupurupu kwa ajili ya kodi ya nyumba, mawasiliano na usafiri.
Hata hivyo, tangu mwenzi wa kwanza katika kumtumikia, marupurupu hayo yameonekana kuwa ni hadithi tu, kila kukicha ni subiri na subiri. Mwaka waisha sasa. Binafsi, nahisi kutotendewa haki na kwa maana nyingine nachukulia suala hili ni mpango tu wa kuhujumu utendaji na ufanisi wangu katika kazi.
Baada ya kuwa nikifuatilia suala hili, pengine na hata kuonekana nakuwa bughudha, taratibu nilianza kuishiwa na hari ya kazi na pia kuanza kufikiria kutafuta ajira mpya.
Hivi punde nimepata wito kutoka kwa mwajiri mpya, ambaye agependa nijiunge naye mapema iwezekanavyo.
Swali langu la msingi ni je, naweza kuamua kuacha kazi kwa short notice? Moja pia kati ya makubaliano katika mkataba ni kutoa notice ya mwezi mmoja!
Naomba msaada kwa wenye kujua na kuwa na uzoefu na masuala haya ya haki za wafanyakazi na sheria kwa ujumla.
Ahsanteni