Je, nimuomba msamaha au nikaushe kuonesha ndio ukidume na kufuatilia matendo ya mke wangu?

Habari za asubuhi

Week iliyopita nilisafiri nje ya Mkoa wa DSM, nikamucha mchumba wangu, (Mke mtarajiwa) huko. Weekend akaniomba kwamba anaenda kutembea hivyo ana hamu ya kutoka out, nikasema sawa nikampa mpaka nauli na hela ya kunywa nikamsihi aende maeneo ambayo ingekuwa rahisi kummonita, kupitia vyanzo vyangu mbali mbali.

Akaenda alivyofika tukawasiliana vema, akaanza kunywa, nikamwambia akilewa achukue bajaji aende nyumbani. Akalewa kweli japo si sana akachukua bajaji akaondoka. Nikapewa habari na mwananke fulani kwamba vipi mkeo mbona namuona hapa? We ndio umemruhusu? Nikasema hapana, ili nisikie jibu linalofuata. Akasema yuko na Mr xxxx na wako very close.

Nikasema powa, nikamuuliza akasema tena wameondoka wote kwa gari muda si mrefu. Nikampigia mke wangu mara saba simu hapokei nikapiga tena video call hapokei, nikajua kama kalewa huwa hapokei hata simu, lakin nikajiuliza kwanini hajaniambia kwamba angalau kafika nyumbani, mawazo yakaanza kunijia kichwani kwamba huyu atakuwa ukweli kachepuka na huyo mtu.

Nikawaza sana, asubuhi na mapema akanipigia kwamba kafika usiku sana na kapiga simu mara kadhaa haikupatikana, nikawaza mbona nilikuwa hewani, lakin nikaamua tu kuendelea kumpeleleza yule mwanamke akasema na sasa hivi karudi naye yule jamaa wamekaa wanakunywa, hapo ni Jumapili. Nikapiga simu mke akapokea akasema anajiandaa kwenda kanisani, nikakausha ila nikaumia.

Ikabidi nifunge safari kurudi Dar, nikaenda Nyumbani bila kumwambia mke nikamkuta pale kibarazani amekaa na mdogo wake, nikaingia ndani kwa jazba, nikaanza kumuuliza mke wangu juzi alipokuwa na hakurudi nyumbani.

Akapanik naye akasema wapi, nikamwambia na aliyekuwa naye akasema si ukweli katika kulazimishana aseme ukweli nikamnasa kibao akalia kwa uchungu, bahati nzuri hata umpige mke wangu uwa si wa kunitukana wala kupiga matusi, akajifungia akalia, akaja kwa magoti mbele yangu nimweleze habari nilipozipata na tuthibitishe.


Nikamwambia aliyekuwa naye, akasema basi twende kwake tumuulize. Nikakataa akasema twende umuonye tu angalau kwamba sitaki mazoea na mke wangu kama umejiridhisha kweli. Nikiwa na hasira kali, nikamfukuza mbele yangu nikitamani kumchapa tena.

Nilikaa bar moja jana nikaamua niseme sasa ngoja nimface huyo mwanamue nimweleze ukweli. Nikafunga safari nilipofika kwake nikaambiwa ana siku kadhaa yuko hospitali alianguka na pikipiki ana kama siku 5 nyuma, sikuamini nikaamua kwenda hospital kumuona alikuwa kweli ana P.O.P

Niliporudi kwangu nikaendelea kukausha mbele ya mke, nikiendelea na uchunguzi. Nikamuulizaa ulitoka bar kule saa ngapi, akasema saa 7 usiku, na ukaelekea wapi akajibu hapa nyumbani uliletwa na nani akasema bajaji. Nikakausha nikaenda kumuuliza mlinzi akasema yes saa saba na nusu mpaka saa nane kuna bajaji siku fulani iliingia ndani na kutoka.

Nikaenda control room ya nyumba tunazokaa kuna CcTv camera nikaangalia kweli bajaji ilirudi na Mke alishuka akiwa amevaa mavazi fulani. Nikamuuliza je, Jumapili ulikaa wapi, akasema niliendaka kanisani kusali na nilisali na fulani na fulani na kwenye Jumuiya niliwasilisha mchango wetu kwa Muinjiristi.

Nikapeleleza ni ukweli alienda huko. Sasa nimegundua nimemtuhumu visivyo na ameonesha heshima kubwa kwangu. Je, nimuombe msamaha au nifanye nini kuonesha nilimkosea, au nisiombe msamaha maana nilikuwa natimiza wajibu wangu wa kumlinda mke? Tatu yule alonipa habari ni wa sehemu fulani amelewa sijui nimwambie
Hapo shida ni kua na mke mlevi tu mkuu na si kingine
 
Back
Top Bottom