Inakuwaje watu wenye akili zao wafikirie kila unapomkuta mwanamke na mwanamume faragha eti wanazungumzia mambo ya kuzaa tu,au eti ukiweka miadi na mwanamke mkutane sehemu fulani ni kwa ajili ya mambo ya kuzaa tu,kwani wanawake hawako kwenye mipango ya kiuchumi?hatuwezi kuzungumza na wanawake masuala ya biashara? masuala ya kuanzisha miradi? ushauri katika masuala ya maisha?.masuala ya uadilifu,masuala ya utu wema?.Yaani ukikutwa na mwanamke wapo wanaofikiria ni uzinzi tu,uchafu tu,.Watu tubadilike tuwape Wanawake ,mama zetu Heshima zao na wanaume tuwe na staha,tujiheshimu ,tutoe maboriti kwenye macho yetu, na tuzipe raha na ujasiri nafsi zetu.Aliye msafi na awe wa kwanza kurusha jiwe.