Road Safety: Stika za Nenda kwa Usalama ni wizi, tuungane kuupinga

1952

Senior Member
Mar 29, 2014
109
37
Ninaandika barua ya wazi kwa Afande MPINGA Mkuu wa Usalama Barabarani kwa wizi na uonevu unaofanywa na Maaskari wa Usalama Barabarani kituo cha Mpakani mwa Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Mara.

Nilikuwa naenda kuhudhuria mazishi ya Ndugu yangu tarehe 28.2.2015 kule Tarime na nilikuwa na gari dogo la RAVA4. Nilipofika mpakani mwa Simiyu na Mara nikakaguliwa na askari namba G.9368 wa Usalama Barabarani.

Baada ya ukaguzi akanieleza kuwa sina STIKA na mimi nikakubali. Nikamweleza kagua gari na nilipie stika. Nikamuuliza kuwa stika ni shillingi ngapi?.

Akanieleza kuwa stika ni tshs.10,000 mimi nikamueleza kuwa mbona stika ni shs.2,000 na ukichelewa kama mimi inaweza kuwa tshs.5,000.

Yeye akanieleza kuwa nitoe tshs.10,000 ndipo anipe stika. Mimi nikagoma na baadaye akasema sasa ninakulipisha faini ya tshs.30,000 kwa kukosa stika.

Nikakubali sawa lakini nipe risiti. Yeye akanieleza kuwa hana risiti ila nitoe tshs.30,000. Nikamuuliza je faini si fedha za Serikali?. Akashindwa la kusema.

Baadaye nikaandikiwa kosa kwa ahadi ya kuchukua risiti kesho yake. Kesho yake nikafuatilia risiti kwa binde ndipo nikaipata.

Maaskari wa Usalama Barabarani wa kituo cha NASA na mpaka wa Simiyu na Mara wanaiibia Serikali sana kwa sababu hawatoi risiti pindi mwenye gari anapopatikana na kosa na fedha wanaweka mfukoni.

Nakushauri Afande MPINGA maaskari wote kwenye vituo nilivyovitaja wavuliwe vyeo mara moja na kuwa Maaskari wa kawaida.

Kwanza wanatesa sana wasafiri na siyo waaminifu mbele ya umma. Hasa Askari namba G.9368 wa kituo cha Wilaya ya Busega afukuzwe kazi mara moja.
 
Habari wana JF.

Mimi nashindwa kuelewa hii kitu wiki nenda mea usalama ni mradi wa serikali au? Na kama ni mradi hizo pesa zinakwenda wapi?

Na kwanini isibadilishwe jina outset ni kodi Flani ya barabarani...nasema hivi kwakuwa mimi mea ifahamu wangu nilijuwa kuwa swala la wiki nenda kwa usalama ni program ya

Kila mwaka ya ukaguzi wa magari yanayotumika barabarani kuhakiki ubora na unalopewa stika maana yake ni kuwa gari lako limekaguliwa na kupitishwa kuwa Lina ubora unaokubalika kisheria....sasa hili linaliendelea sijui kama ni lengo la jeshi la polisi au ni nini.... Vishoka hupita katika maofisi mbalimbali na kukusanya namba zao magari huku wakichangisha 20,000 eti stika ya wiki na fire extinguisher.
 
Naomba msaada wenu, nikiwa sina stika za wiki ya twende kwa usalama na fire extinguisher kwenye gari yangu ninakuwa nimevunja sheria?
 
Ni kwa kujazia budget deficit iliyosababishwa na kutumia mabilioni igunga
 
jamani wanajf,mimi gari yangu haina stika ya fire sasa polisi wanansumbua sana,fire extinguisher ninayo lakini kila siku nakamatwa eti sina stika ya fire,nauliza hivi hili gari ni la kwangu sasa hata likiungua wao linawahusu nini je ni halali kukamatwa na polisi kisa sita stika ya fire?
 
halafu utashangaa hawatoi matangazo kuwa stika zinapatikana wapi?mpe rushwa buku 5 uachane nae!daladala ina stika 7 zote ni pesa tuu.hapa nilipo naitafuta ya wiki ya nenda kwa usalama
 
Stika maana yake ulilipia fire extinguisher, ukapata induction ya kutumia fire extinguisher , na ukapewa fire extinguisher.
Kua na fire extinguisher bila stika kuna leta mashaka kuhusu namna uliipata na kama unajua kutumia.
Ni mtazamo wangu
 
halafu utashangaa hawatoi matangazo kuwa stika zinapatikana wapi?mpe rushwa buku 5 uachane nae!daladala ina stika 7 zote ni pesa tuu.hapa nilipo naitafuta ya wiki ya nenda kwa usalama

hawa jamaa ni noma,buku buku wanachukua sana kisa fire,wananiudhi sana iko siku ntawatolea uvivu
 
Stika maana yake ulilipia fire extinguisher, ukapata induction ya kutumia fire extinguisher , na ukapewa fire extinguisher.
Kua na fire extinguisher bila stika kuna leta mashaka kuhusu namna uliipata na kama unajua kutumia.
Ni mtazamo wangu

unajua stika ilitoka kwa kuloa na maji so sina stika tena,kutumia worry not najua
 
jamani wanajf,mimi gari yangu haina stika ya fire sasa polisi wanansumbua sana,fire extinguisher ninayo lakini kila siku nakamatwa eti sina stika ya fire,nauliza hivi hili gari ni la kwangu sasa hata likiungua wao linawahusu nini je ni halali kukamatwa na polisi kisa sita stika ya fire?

Kuepuka usumbufu nenda pale Fire na 5000 utapata hiyo stika bila zengwe.

Hata hivyo kuwa navyo vyote haikupi garantii ya kutokamatwa, maana wakiona una kila kitu atakwambia mtungi wa fire extinguisher ni mdogo unatakiwa kuwa na wa 2kgs.
 
jamani wanajf,mimi gari yangu haina stika ya fire sasa polisi wanansumbua sana,fire extinguisher ninayo lakini kila siku nakamatwa eti sina stika ya fire,nauliza hivi hili gari ni la kwangu sasa hata likiungua wao linawahusu nini je ni halali kukamatwa na polisi kisa sita stika ya fire?

Mkuu kila gari inatumia barabara na miundo mbinu mingine ya umma....
Kwa hiyo gari lako kuungua ni public concern....
Ila pia usisahau hasara ya moto kwa mtu mmoja ni hasara kwa umma....uchumi wa mtu mmoja mmoja ni muhimu sana kwa uchumi wa taifa!


 
jamani wanajf,mimi gari yangu haina stika ya fire sasa polisi wanansumbua sana,fire extinguisher ninayo lakini kila siku nakamatwa eti sina stika ya fire,nauliza hivi hili gari ni la kwangu sasa hata likiungua wao linawahusu nini je ni halali kukamatwa na polisi kisa sita stika ya fire?

Pole sana mshirika, hawa jamaa walinipiga sana bao kwa ajili ya hiyo sticker ya fire hadi nikaamua kulipia kukwepa usumbufu. Mie naona trafic kabla hajapeleka mboga nyumbani atatfuta kisingizio hadi akutoe upepo, ni kiashirio cha matatizo makubwa zaidi ndani ya mfumo wetu wa utawala.
 
ok thanks people kwa ushauri wenu,ngoja nkakate stika nyngne although ni dili ya watu wachache tu
 
sasa hv wanakomalia week ya nenda kwa usalama!mm walinikamata,sticker ninayo ila ipo kwenye droo,jamaa nkamwambia nimeichukua mda s mrefu kwa trafic mwenzio hapo moroko,alistuka!akasema ubandike basi,akaniachia!wazush kweli/hawa jamaa
 
jamani wanajf,mimi gari yangu haina stika ya fire sasa polisi wanansumbua sana,fire extinguisher ninayo lakini kila siku nakamatwa eti sina stika ya fire,nauliza hivi hili gari ni la kwangu sasa hata likiungua wao linawahusu nini je ni halali kukamatwa na polisi kisa sita stika ya fire?

mkuu hapo penye nyekundu nakupa mfano wa mtu anashtakiwa kwa kutaka kujiua mwenyewe sasa unashangaa kwa nini ashtakiwe wakati ana maisha yake na maamuzi juu ya mwili wake.?sasa ndo ww unayeshangaa watu wako concend na gari yako ingawa hata hawajui bei yake na umelipataje kiufupi hakukuchangia.ndugu that is the law.
sasa suala la stika ya fire kama uliivyo iita naomba tujiulize whether kuna sheria inayosema hivyo kuwa na stika ya fire?la kujua ni kwamba no one can be charged with non existing offence.kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa huwezi kushtakiwa kwa kosa ambalo sheria haijatamka kua ni kosa.mfano kama sheria haijatamka kua kutofunga mkanda wa gari ni kosa basi hata kama usipofunga usiogope kukamatwa na kua charged kwa kosa hilo kwa sababu si kosa
hivyo hivyo kwa issue ya stika ya fire nadhani hao jamaa wanajua kua watanzania ni waelewa hivyo kutokua na stika ya fire itakua ni kosa.
zinapatikana vip hapo ndo patamu kwani Tanzania ni zaidi uijuavyo.
Kwa kutaka kujiridhisha soma Traffic road act uone inasemaje ktk hilo.au any by law to that effect.
 
Wiki ya nenda kwa usalama. kumekuwepo ukaguzi wa nguvu toka kwa matrafik, wenye magari wanalazimika kukata stika na kuibandika ktk gari yako, hata kama gari yako ni mpya huna budi kulanguliwa stika kwa gharama kuanzia tsh 5000/= na kuendelea ili hali bei halisi ni tsh 3000/=. kuna tetesi kuwa umetokea wizi huko wa vitabu vya stika hizo na vehicle inspector 6 wako ndani kwa tuhuma hiyo , zoezi la kupata stika limesimama hadi wiki ijayo, hivi kumbe hata polisi kuna wezi.....? mwenye taarifa jamani atudadavulie hawa jamaa (trafic) NI WATU AMBAO SIWAPENDI KIUPITA MAELEZO.
 
Wiki ya nenda kwa usalama. kumekuwepo ukaguzi wa nguvu toka kwa matrafik, wenye magari wanalazimika kukata stika na kuibandika ktk gari yako, hata kama gari yako ni mpya huna budi kulanguliwa stika kwa gharama kuanzia tsh 5000/= na kuendelea ili hali bei halisi ni tsh 3000/=. kuna tetesi kuwa umetokea wizi huko wa vitabu vya stika hizo na vehicle inspector 6 wako ndani kwa tuhuma hiyo , zoezi la kupata stika limesimama hadi wiki ijayo, hivi kumbe hata polisi kuna wezi.....? mwenye taarifa jamani atudadavulie hawa jamaa (trafic) NI WATU AMBAO SIWAPENDI KIUPITA MAELEZO.
Ebwana hata mimi nimeipata hii. inasemekana zimeibwa sticka za M20. Kwa hiyo chukua tahadhari sna na ununuzi wa sticka maana inaweza ikaangukia kwenye range ya zilizoibiwa na ukatakiwa kuwasaidia ili apatikane aliye kuuzia, japo naamini hata ukimpata talindwa na system baadaye itagundulika wewe ndiye uliyeiba...kumbuka msemo wa aliyekamatwa na ngozi............
 
Wengi wamebandika hizo stika kwa magari yao lakini hawajui ni kwa ajili gani hata ungemuuliza huyo trafiki aliyekukamata ni sheria gani umevunja kwa kutokuwa na hiyo stika ya fire asingeweza kujibu.
Mi nakumbuka last year hapa A town police wala sio trafic walikuwa wanakamata magari yasiyo na stika, wakanipiga mkono nikasimama ooh mbona huna stika ya fire nikawambia lakini fire extinguisher ninayo, akajibu basi hujakaguliwa unatakiwa ikaguliwe lafu upewe stika, basi nikampa efu 10 akaniandikia hiyo stika wala hajaikagua hiyo fire extinguisha wala nini.
Basi badae nikuiza tu hivi nini hii kitu ya stiker za fire extinguisher ndio nikaeleweshwa kwamba inatakiwa upeleke gari lako ukiwa na fire extinguisher ikaguliwe ikionekana ipo OK hiyo extinguisher ndio unapewa hiyo stika.

kwa ufupi sio kosa kutokuwa na stika kwa gari ila ni kosa kutokuwa na fire extinguisher kwa gari. kama vile ambavyo sio kosa kutokuwa na stika ya usalama barabarani, kwani wengi wanazo lakini magari yao sio roadworthy ambayo ndo maana hasa ya hiyo stika kwamba gari imefanyiwa ukaguzi na imeonekana ni roadworthy.
 
Back
Top Bottom