Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,557
- 19,435
Imekuwa ni tabia ya Kawaida sana kwa magazeti ya Tanzania, hasa yale ya global Publishers kuonyesha waziwazi picha za watu waliokufa ama kwa ajali au kwa kupigwa risasi. Hiyo ni tabia ambayo nimeiona kwa muda mrefu sana sasa tangia zile za wakenya waliouwawa na polisi huko Arusha miaka kadhaa iliyopita. Je ni ustaarabu kweli kuonyesha picha za namna hiyo? Ninadhani kufanya hivyo kunasababisha watu wengine hasa vijana wale ambao akili zao hazijakomaa vya kutosha kushindwa kuona thamani ya uhai, na kuona kuwa kuuana ni jambo la kawaida.