Je, ni virusi vya Corona au ni watu wenye ubaguzi wa rangi?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,006
1,026
VCG41N853932092.jpg

Maambukizi ya virusi vya Corona yamefichua unafiki kuwa nchi zile zinazopinga vikali ubaguzi wa rangi ndio zenye vitendo vibaya zaidi vya ubaguzi wa rangi.

Wakati virusi vya Corona vilipogunduliwa kwa mara ya kwanza mjini Wuhan, China, wao walitoa kauli ya ubaguzi kama “virusi vya China” kuwacheka, kuwanyooshea vidole na kuwashambulia Wachina na watu wenye asili ya Asia; na ambapo siku hizi India inakabiliwa na hali mbaya ya maambukizi ya virusi, Marekani na nchi nyingine kadhaa zilikuwa za kwanza kukatisha safari za ndege na kusita kutoa misaada, na hata Australia nayo ilitangaza kuwazuia watu waliofika India ndani ya siku 14 kurudi nchini humo, ikisema watu wanaokiuka hatua hiyo watafungwa jela kwa miaka hadi mitano na kulipa fidia ya kiasi kikubwa. Juu ya hili, serikali ya Australia inaeleza kuwa imefanya uamuzi huo ikizingatia maslahi ya nchi na afya ya wananchi wake. Basi hebu tujiulize, je, wakati Marekani na Uingereza zilipokuwa na hali inayofanana na ya sasa ya India kwa maambukizi ya virusi vya Corona, kwa nini Australia haikukatisha safari za ndege kutoka kwenye nchi hizo, sembuse kutoa uamuzi wa kufanya kurudi nchini kwa raia wake kama kitendo cha uhalifu. Wakati ule, maslahi ya Australia yalikuwa ni yepi? Vilevile hatuoni ripoti kwenye vyombo vya habari kuwa kuna watu wanapiga kelele kuwataka watu hao “warudi Marekani” au “warudi Uingereza”.

Kama waasia, waafrika nao pia wanakabiliwa na ubaguzi wa rangi mbele ya janga hili la virusi vya Corona. Aliyekuwa naibu waziri mkuu wa Italia Matteo Salvini aliwahi kuwatupia lawama watu waliotafuta hifadhi nchini humo kutoka Afrika kwa kupeleka virusi hivyo katika kipindi cha mwanzo, lakini ukweli ni kuwa wanasayansi wamegundua mapema kuwa mwishoni mwa mwaka 2019, kabla ya virusi kugunduliwa Wuhan, virusi vilikuwa tayari vipo nchini Italia. Wanayansi wawili wa Ufaransa nao walitoa kauli ya ajabu ya “kufanya Afrika kuwa uwanja wa majaribio ya chanjo dhidi ya virusi vya Corona”. Na takwimu mpya zilizotolewa na Chuo Kikuu cha Harvard Marekani zimeonesha kuwa kiwango cha wanaume waliofariki dunia kwa virusi vya Corona ni cha juu kuliko cha wanawake, lakini kiwango cha vifo vya wanawake wenye asili ya Afrika ni mara tatu zaidi ya kiwango cha wanaume wazungu.

Lakini vyombo vya habari vya kimagharibi havikosoi na kuzihoji serikali za nchi hizo juu ya hayo, badala yake vilizusha jambo kwa nia mbaya kati ya waasia na waafrika ambao ni makundi yanayokabiliwa zaidi na ubaguzi wa rangi na kuchochea chuki kati yao. Kuna habari zinazosema kuwa kutokana na ubaguzi wa rangi na “unyanyasaji” unaofanywa na wachina dhidi ya wakenya na waafrika wa nchi nyingine, mvutano kati ya wachina waishio nchini Kenya na wenyeji unaongezeka sana. Hakuna jamii ya utumwa katika historia ya China, na suala la “ubaguzi wa rangi” ni jambo geni na ni nadharia tu kwa wachina. Na hata kuna mgongano kati ya wachina na waafrika waishio China, ni kutokana na kuelewana vibaya au vitendo vya mtu mmoja mmoja, na kutaja wachina kuwadhalilisha waafrika basi ni jambo la kichekesho tu. Lakini matumizi ya nguvu ya polisi dhidi ya watu wa rangi na matukio ya kuwapiga watu risasi ovyo yanayosababishwa na ubaguzi wa rangi wa kimfumo kweli yapo na pia yanaongezeka katika nchi za magharibi zilizowahi kufanya utumwa kama Marekani.

Kwa mujibu wa shirika lililotafuta faida la Marekani “Gun Violence Archive”, mwaka jana matukio ya kuwafyatulia watu risasi ovyo yaliongezeka kwa asilimia 50, haswa katika nchi wanazoishi kwa wingi watu wenye asili ya Afrika na Latin Amerika; na Shirika la kupinga chuki dhidi ya watu wa Asia na Pasifiki AAPI, katika mwaka mmoja uliopita baada ya kutokea kwa janga la virusi vya Corona, liliripoti matukio 3,800 ya chuki dhidi ya watu wenye asili ya Asia, na matukio hayo yameongezeka kwa kasi zaidi katika miezi mitano iliyopita.

Hakuna wanasayansi wanaohusisha virusi vya Corona na rangi, taifa, kabila au dini, lakini inaonekana kuwa tangu ugunduliwe, umekuwa ugonjwa wa ubaguzi wa rangi, au tuseme virusi hivyo vimetusaidia kufichua unafiki wa nchi za magharibi katika suala la ubaguzi wa rangi, na kuanika juani mchezo mbaya kati ya serikali za nchi za magharibi na vyombo vya habari.
 
Hawa wahindi waache tu wabaguliwe maana wao ni wabaguzi wakubwa sana si kidogo kuliko hao wanaowabagua
 
Back
Top Bottom