Elections 2010 Je ni sahihi waandishi wa habari kutumika kupiga kampeni za chama fulani?

Ngolinda

Senior Member
Apr 12, 2010
125
25

Kuna habari kwamba waandishi wa habari hasa kutoka habari corporation wanatumika katika kampeni za kumnadi Rais Kikwete, na wale wote wanaokwenda kinjume na maslahi ya CCM wanafukuzwa katika msafara wa kampeni za Kikwete kama ilivyotokea kwa mwandishi wa gazeti la mwananchi. Na juzi wanahabari hao katika msafara wa Kikwete walionekana wamevalia vijikoti vyenye picha na maneno ya kumnadi mgombea huyo. Maswali ni: Je, ni sahihi kwa wanahabari kutumika kupiga kampeni na kuandika habari kwa maslahi ya kundi fulani linalosaka madaraka?. Je, haya ndio maadili ya wanahabari? Na kama media ikikubali kutumika kwa maslahi ya kundi fulani, hii si kuhatarisha maslahi na mustakabali wa nchi yetu?
 
Ndio siasa hiyo. Kwani mnadhani Obama wenu alichaguliwaje kama si waandishi wa habari na vyombo vyao kumpamba na kumlamba makalio. Angalieni PMS-NBC muone jinsi walivyo kwenye tank kwa Obama. Inakera!!!
 
sioni tatizo kwani hata wa freemedia wanaweza kuipamba chadema na annur kupamba kafu... cha maana tu ni kwamba wasiwanyime haki waandishi wengine kupata coverage ili tupate habari zisizochakachuliwa
 
Waandishi weengi wa kibongo ni wa bahasha tu kwani hujui? Wao uandika habari za mtu aliyetoa bahasha.

Sisi M wao ni mbingwa wa kutoa hongo hivyo usishangae kuona waandishi wakicheza ngoma yao.
 
hamna tatizo waandishi kulalia upande fulani, labda ulalamikie vyombo vya umma, kama TBC na Daily News, hivyo ndivyo vinavyotakiwa kuwa fair, maana ni mali ya walipa kodi wote, ila ITV, Mananchi, Tz Daima na Mtanzania wana haki ya kuwa upande wowote wautakao, na wala hawavunji maadili yeyote.
tena kama nchi za wenzetu kama uingereza inajulikana kabisa chombo fulani kinamu-endorse mgombea fulani au chama fulani, wala hamna shida hapo!
 
Back
Top Bottom