Je, ni sahihi Steven Mbazi kusimamia mali za Bilionea? Tumpe ushauri DC Jerry Muro katika utatuzi wa sakata hili la mali

Nimekusoma mkuu ila hii kesi imekaa kama ila ya sharifu ngoja tuone mahakama itatoa hukumu gani
hapana labda Kesi (Miriam) imekaa km ya Chusa kule Hospitalini Baraa alipowekwa akiwa ana kesi ya Mada alipanga na Sharif aliyekuwa na hasira za kuzidiwa utajiri
post: 7129510 said:
Huyo lazima atakuwa Chusa, manake yeye ndiye aliyemwua yule kijana wa Erasto aliyekuwa anamwibia madini pale tanzaniteone. Baadaye Chusa na Erasto wakawa na bifu sana mpaka Chusa akawekwa ndani kwa ajili ya mauaji ya yule kijana.
Inasemekana pikipiki zilizoenda kwenye mauaji ya Erasto zilinunuliwa mpya kwa kazi maalum, simu mpya mbili kwa kazi maalum.
Tusubiri mengi........................
Jua Kesi ya Mauaji ya Dada wa Bilionea iimekosa muuaji(muuaji atatoka km Chusa hata kwa chonee)
nambie hapo Kesi imesimama
Hakimu kesi ya mke wa bilionea Msuya ataka muda zaidi kusikiliza mashahidi

  • Mtanzania
  • 20 Jul 2019
  • Na KULWA MZEE -DAR ES SALAAM
img
-PICHA: IMANI NATHANIELMAHAKAMANI: Aliyekuwa mke wa bilionea Msuya ambaye ni marehemu, Miriam Mlita, akielekea Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam jana kusikiliza kesi ya mauaji inayomkabili.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imesema ili kuwepo usikilizaji wa haki katika kesi ya mauaji inayomkabili Miriam Mrita, mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya na mwenzake, inahitaji muda wa kutosha ili mashahidi 45 wa Jamhuri na wale wa utetezi wote wasikilizwe.
Hayo yalisemwa jana na Jaji Sekela Moshi, wakati akiahirisha kesi hiyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo siku mbili zilizopangwa kusikiliza shauri hilo kuwa hazitoshi.
Akiiwakilisha Jamhuri, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mkunde Mshanga, alidai shauri lilikuja kusikikizwa, lakini wazee wa baraza ambao kisheria wanatakiwa kuwepo hawapo.
Alidai pia Jamhuri inasikitika mashahidi wao hawajapewa hati ya wito wafike mahakamani kutoa ushahidi, hivyo aliomba mahakama itoe wito wafike.
Jaji Moshi alisema kesi hii isingeweza kuendelea, ilipangwa siku mbili ambayo ni jana na Jumatatu, lakini kuna mashahidi 45 wa Jamhuri, bado mashahidi wa upande wa utetezi.
“Tumeona ili tuwe na usikilizaji wa haki, mashahidi wote wasikilizwe, hii kesi inahitaji muda zaidi, tutaiahirisha hii kesi ili tuipangie muda wa kutosha.
“Kesi itaendelea wakati mwingine kwa tarehe itakayopangwa na Naibu Msajili, washtakiwa wataendelea kukaa rumande,” alisema.
Mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Revocatus Muyella.
Wanadaiwa Mei 25 mwaka 2016 katika eneo la Kibada Kigamboni, walimuua kwa makusudi Aneth Msuya ambaye ni dada wa Bilionea Msuya.
 
Hotel inabiashara kubwa sana msimu wa utalii kuna kampuni nyingi za utalii zinalaza wageni pale,kuna kampuni ya climbkili inalaza wageni hapo wa kutosha mana ni kampuni kubwa
Sawa kwa kodi za anko Magu ni nyingi sana
 
hapana labda Kesi (Miriam) imekaa km ya Chusa kule Hospitalini Baraa alipowekwa akiwa ana kesi ya Mada alipanga na Sharif aliyekuwa na hasira za kuzidiwa utajiri

Jua Kesi ya Mauaji ya Dada wa Bilionea iimekosa muuaji(muuaji atatoka km Chusa hata kwa chonee)
nambie hapo Kesi imesimama
Hakimu kesi ya mke wa bilionea Msuya ataka muda zaidi kusikiliza mashahidi

  • Mtanzania
  • 20 Jul 2019
  • Na KULWA MZEE -DAR ES SALAAM
img
-PICHA: IMANI NATHANIELMAHAKAMANI: Aliyekuwa mke wa bilionea Msuya ambaye ni marehemu, Miriam Mlita, akielekea Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam jana kusikiliza kesi ya mauaji inayomkabili.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imesema ili kuwepo usikilizaji wa haki katika kesi ya mauaji inayomkabili Miriam Mrita, mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya na mwenzake, inahitaji muda wa kutosha ili mashahidi 45 wa Jamhuri na wale wa utetezi wote wasikilizwe.
Hayo yalisemwa jana na Jaji Sekela Moshi, wakati akiahirisha kesi hiyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo siku mbili zilizopangwa kusikiliza shauri hilo kuwa hazitoshi.
Akiiwakilisha Jamhuri, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mkunde Mshanga, alidai shauri lilikuja kusikikizwa, lakini wazee wa baraza ambao kisheria wanatakiwa kuwepo hawapo.
Alidai pia Jamhuri inasikitika mashahidi wao hawajapewa hati ya wito wafike mahakamani kutoa ushahidi, hivyo aliomba mahakama itoe wito wafike.
Jaji Moshi alisema kesi hii isingeweza kuendelea, ilipangwa siku mbili ambayo ni jana na Jumatatu, lakini kuna mashahidi 45 wa Jamhuri, bado mashahidi wa upande wa utetezi.
“Tumeona ili tuwe na usikilizaji wa haki, mashahidi wote wasikilizwe, hii kesi inahitaji muda zaidi, tutaiahirisha hii kesi ili tuipangie muda wa kutosha.
“Kesi itaendelea wakati mwingine kwa tarehe itakayopangwa na Naibu Msajili, washtakiwa wataendelea kukaa rumande,” alisema.
Mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Revocatus Muyella.
Wanadaiwa Mei 25 mwaka 2016 katika eneo la Kibada Kigamboni, walimuua kwa makusudi Aneth Msuya ambaye ni dada wa Bilionea Msuya.
Ukwaju hii kesi hatoki mtu hukumu inampeleka,aliehusika na huyo mama ni mshkaji na alikua na maisha yake ila alipopoteza kazi ndio akawa mishentwn.ndio kukutana na huyo maza na kupanga unyama wao.
Kuna jamaa mwingine alishikwa pamoja nao anaitwa magoma yeye aliachiwa mana hakua anajua chochote na ndio anatupa story kua maza mhusika mwanzo mwisho
 
hukumu inampeleka,aliehusika na huyo mama ni mshkaji na alikua na maisha yake ila alipopoteza kazi ndio akawa mishentwn.ndio kukutana na huyo maza na kupanga unyama wao.
Kuna jamaa mwingine alishikwa pamoja nao anaitwa magoma yeye aliachiwa
sawa Mkuu lkn ukizungumzia Hukumu kabla ya upelelezi mnakosea, huyu Mama kapanga mipangilio ya mauaji ndio maana kuna MANSLAUGHTER na MURDER upelelezi kwa DPP bado, mara ya mwisho ilikuwa Julai mwaka huu leo November
kwenye RED km huyu mshikaji kawataja waliokamata kisu na kuua au aiwashuhudia pale chumbani wameshakamatwa basi hukumu ipo na jamaa yako na Mke wa Bilionea hawahusiki wao wataambulia kifungo na wakitoka watarejea Uraiani na Mama akaendelee na usimamizi wa mirathi. Nionavyo mm il revenge itakuwepo tu kwa watu hawa mpaka akosekane mshindi
 
sawa Mkuu lkn ukizungumzia Hukumu kabla ya upelelezi mnakosea, huyu Mama kapanga mipangilio ya mauaji ndio maana kuna MANSLAUGHTER na MURDER upelelezi kwa DPP bado, mara ya mwisho ilikuwa Julai mwaka huu leo November
kwenye RED km huyu mshikaji kawataja waliokamata kisu na kuua au aiwashuhudia pale chumbani wameshakamatwa basi hukumu ipo na jamaa yako na Mke wa Bilionea hawahusiki wao wataambulia kifungo na wakitoka watarejea Uraiani na Mama akaendelee na usimamizi wa mirathi. Nionavyo mm il revenge itakuwepo tu kwa watu hawa mpaka akosekane mshindi
Murder is defined as killing somebody with “malice aforethought,” which is malice. The two types of malice is “express malice” and “implied malice.” Express malice is when a person intended to kill another person or persons. Implied malice is when a person intentionally commits an act they knew was dangerous to other people and human life resulting in death. In other words, the murder was committed with a conscious disregard for human life.
If a crime involves expressed or implied malice its defined as “murder.”
 
Murder is defined as killing somebody with “malice aforethought,” which is malice. The two types of malice is “express malice” and “implied malice.” Express malice is when a person intended to kill another person or persons. Implied malice is when a person intentionally commits an act they knew was dangerous to other people and human life resulting in death. In other words, the murder was committed with a conscious disregard for human life.
If a crime involves expressed or implied malice its defined as “murder.”
TANMOJA Nimekubali ila hukumu yake ni ipi? maana hizi Sheria nyingi za lugha za kigeni
Lakini Mueder kwetu naona wengi wanapangua nikirifaa Kesi ya Asha Mkwizu na Zombe na kwa wenzetu USA wanazaidi ya aina 52 na Murder
How do you prove malice in defamation?
To prove prima facie defamation, a plaintiff must show four things: 1) a false statement purporting to be fact; 2) publication or communication of that statement to a third person; 3) fault amounting to at least negligence; and 4) damages, or some harm caused to the person or entity who is the subject of the statement.
Mm nasubiri km unayo Hukumu ya hii Kesi ya Mke wa Bilionea kwa faida ya wote ingawa hatuingilii upelelezi
 
Kisasi huwa kinatambaa...

toka erasto hajafa huyo aneth alikuwa haelewani na wifi yake...
Erasto na mdogo wake inazungumzwa kuwa walikuwa
" wakipendana sana yaani!"
 
Ukwaju hii kesi hatoki mtu hukumu inampeleka,aliehusika na huyo mama ni mshkaji na alikua na maisha yake ila alipopoteza kazi ndio akawa mishentwn.ndio kukutana na huyo maza na kupanga unyama wao.
Kuna jamaa mwingine alishikwa pamoja nao anaitwa magoma yeye aliachiwa mana hakua anajua chochote na ndio anatupa story kua maza mhusika mwanzo mwisho


Maza yupi muhusika kwenye yapi ya mwanzo mwisho?
 
Kimsingi upande wa baba ndiyo ndugu halisi na chimbuko la watoto.
Ndugu wa mama siku zote huwa tatizo na ndugu wa baba pia huwa nao ni matatizo pia,wamama huwavuta watoto nakuwapandikiza chuki zidi ya upande wababa nakuwaambia watakuzurumuni mali zenu,na upande wababa mala nyingi wao ndio hujiona wenye haki zaidi na marehemu kuliko wengine.kama wangelilikuwa waislamu basi milathi yao ingelikuwa nyepesi kabisa baba wa marehemu ana haki yake ambayo imetajwa wazi mama nae anafungu lake kisha mke naye ana lake nawatoto nao wanahaki zaidi kuliko hao niliowataja huko nyuma tena kipimo kinachotumika ni chaasilimia.kiisilamu hapo kumbukeni warithi wahuyo marehemu ni mafungu 3 tu, 1 wazazi 2 mke 3 watoto.nashangaa sana munafeli wapi wakristo? Kama hamna sheria ktk kitabu chenu! musione aibu kuazima hii sheria alafu muone kama kutakuwa naugomvi tena
 
Mara nyingi upande wa baba huwa wapo busy na mambo yao. Ila familia ya Erasto inaonekana kuwa ya kueleweka zaidi kuliko ya Mrita.
Ukiifatilia vizuri hii kesi unagundua kuwa huyo kijana kama alikuwa anasoma kweli nje ya nchi.Basi iko chuo au shule sio ya kupeleka mtoto wako kabsa maana anasikiliza zaidi maneno ya kuambiwa kulko kuangalia uhalisia wa tukio.Mama yako amekiri kamuua shangazi yako unawachukiaje upande wa baba yako wakati wamepoteza wapendwa wao wawili.Huyo dogo akituliza kichwa ana nafas kubwa ya kumaliza hyo kesi maana kiumri anauwezo wa kusimamia mali za baba yake.Kwa upande wangu naona FAMILIA YA BABA iko sawa zaidi japo wanaweza kuwa na mapungufu kama binadamu,Kuliko upande wa mama yake.Wamshaur kijana atulize akili yake ili asimamie mali zao na amlee mama yake huko gerezani alipo.Akae karibu na familia zote mbili upande wa Baba na Mama maana wote wanamuhusu.
 
Uku Tanganyika atufati sheria za dini , Tunafata sheria za jamuhuri ya muungano wa Tanzania, ata ndoa za kiislam wakigombana au kutallikiana kama mmoja wapo ajalizika ukimbilia mahakani ya hakim mkazi, nasiyo mahakama za kadhi.
Kaulize vizuri mahakamani.sheria ya dini inatumika,ninyinyi tu ndio munachagua mugawe mali zenu kwa sheria ipi.kuna ya dini na ya serikali na yakimila.mimi ni shahidi ktk hili tumegawana milathi yetu kwa sheria ya kiislamu ktk mahakama ya magomeni hapo drs
 
Maelezo ya mashahidi
Baada ya kumaliza kutaja idadi na
majina ya mashahidi pamoja na
vielelezo, mawakili hao wa
upande wa mashitaka walianza
kuwasomea washtakiwa maelezo
ya mashahidi wote
wanaotarajiwa kutoa ushahidi
katika kesi hiyo.
Mawakili hao waliwasomea
washtakiwa maelezo ya
mashahidi hatua kwa hatua, kwa
kupokezana kila baada ya kusoma
maelezo ya mashahidi kadhaa,
kazi ambayo ilitumia takribani saa
tano, kuanzia saa 5.15 asubuhi
mpaka saa 9.55 alasiri, Alhamisi
iliyopita
Pamoja na mambo mengine
yaliyomo katika maelezo ya
mashahidi hao, mawakili hao
walidai mshitakiwa wa kwanza,
Miriam alikiri kuhusika katika
mauaji hayo na kueleza sababu na
mpango wa namna
walivyotekeleza mauaji
Mipango ya mauaji
Wakili Mwita alidai washtakiwa
katika kutekeleza mauaji hayo
walimtafuta mfanyakazi wa ndani
wa Aneth.
Alidai Mei 5, 2016 , Miriam na
mwenzake walienda Kibada
alikokuwa akiishi Aneth na
kwamba kabla ya kufika katika
nyumba ya Aneth, alikutana na
mfanyakazi huyo wa ndani wa
Aneth, aitwaye Getrude Mafuru
ambaye alikuwa anaenda dukani
kununua karatasi za chooni (toilet
paper).
Wakili Mwita alidai mshtakiwa
Miriam alishusha kioo cha gari la
kifahari lenye rangi ya bluu
alimokuwamo na kumuita
Getrude ambaye aliitikia wito na
akamuuliza mahali Aneth
alikokuwa akiishi. Alidai kuwa
Getrude alimueleza kuwa Aneth
anakaa nyumba iliyokuwa
inafuata, kutoka walikokuwa
wamesimama na kisha Miriam
alimuahidi msichana huyo kuwa
angepita kesho, kisha alipandisha
kioo cha gari yake na kuondoka.
Siku iliyofuata, Wakili Mwita alidai
Miriam alienda tena hadi karibu
na nyumba aliyokuwa akiishi
Aneth, ambapo alimuona Getrude
akichota maji nyumba ya jirani na
akamuita na msichana huyo
alipomfikia, Miriam alimtaka
apande katika gari hilo. Kwa
mujibu wa maelezo hayo, Wakili
Mwita alidai msichana huyo
aliingia ndani ya gari hilo na
Miriam akampatia simu ndogo
yenye rangi nyeusi.
Mwita alidai kuwa wakati Getrude
anapewa simu na Miriam,
mshitakiwa wa pili yeye alikuwa
amekaa nyuma huku akiwa
amemuwekea Getrude bastola
begani na kwamba Miriam
alimwambia msichana huyo
asimwangalie Muyella bali
amwangalie yeye.
Wakili Mwita alidai Miriam
alimweleza Getrude kuwa simu
hiyo ni ya mawasiliano baina yao
wawili huku akimweleza sio kwa
ajili ya kumpigia mtu mwingine
yeyote.
Alidai Getrude ambaye alikuwa
analipwa mshahara wa Sh 60,000
alieleza kuwa sura ya Miriam
alishawahi kuiona Moshi, kwa bibi
yake yaani kwa mama yake
marehemu Aneth, alikokuwa
kabla ya kwenda kwa Aneth, na
kwamba Miriam alikwenda
nyumbani hapo na mumewe
Erasto Msuya enzi za uhai wake.
Wakili Mwita aliendelea kudai
kuwa Mei 23, 2016 saa tisa
mchana, Miriam alimpigia Getrude
na kumwambia anataka kuonana
naye, huku akimwelekeza mahali
alikokuwa.
Alidai kuwa Getrude alikwenda
hadi mahali lilipokuwa
limeegeshwa gari la washitakiwa
hao, karibu na nyumba ya Aneth
na kisha binti huyo aliingia katika
gari hilo.
Wakili Mwita alidai Getrude akiwa
ndani ya gari hilo aliiona pochi ya
Miriam ikiwa imejaa hela zikiwa
zimefungwa na mpira
mwembamba, na Miriam akampa
Sh 20,000.
Alidai baada ya kumpa fedha hizo,
Miriam alimsisitiza Getrude
aondoke nyumbani kwa Aneth
kabla ya Mei 25, 2016 na kwamba
simu hiyo aliyompa aitupe
sehemu ambayo mtu mwingine
hawezi kuiona.
Wakili Mwita alidai Mei 25, 2016
Getrude aliondoka nyumbani kwa
Aneth na ufunguo wa geti
aliupeleka kwa jirani yao, kisha
akampigia simu Aneth kuwa
ufunguo wa ndani upo chini ya
kapeti la kufutia vumbi lililopo
mlangoni na kwamba ufunguo wa
getini upo kwa jirani yao.
Alidai Getrude aliondoka na
kwenda Chanika kwa mchumba
wake aitwaye Sabri Kombo, na
kwamba wakati akiwa kwenye
pantoni, aliitupa simu hiyo
baharini na alipofika kwa mpenzi
wake alimwelezea mambo
aliyoambiwa na Miriam. Akiwa
Chanika, Wakili Mwita alidai kuwa
Getrude alipigiwa simu na bibi
yake, yaani mama wa Aneth na
kumweleza kuwa Aneth ameuawa
kwa kukatwa koromeo.
Kwa upande wake Wakili Nguka
alidai baada ya tukio, hilo timu ya
askari wa upelelezi wakiongozwa
na Mkuu wa Upelelezi Kinondoni,
Mrakibu wa Polisi (SP) Richard
Mwaisamba ilifika eneo la tukio na
kukuta mlango wa nje ukiwa
haujafungwa.
Alidai timu hiyo ilikuta mlango wa
chumbani ukiwa umevunjwa kwa
kutumia tofali na kwamba chini
ya mlango kulikuwa na vumbi la
matofali. Ndani ya chumba cha
Aneth, Wakili Nguka alidai kuwa
wapelelezi hao walikuta mwili wa
Aneth ukiwa umekatwa koromeo
ukiwa sakafuni, huku ukiwa uchi
wa mnyama na mdomoni alikuwa
amewekewa kitambaa.
Alidai pembeni mwa mwili wa
Aneth, wapelelezi hao walikuta
nguo ya ndani yenye rangi ya
zambarau, kisu chenye damu na
filimbi iliyokuwa karibu na
kitanda. Kwenye kabati lililokutwa
wazi walikuta hereni, cheni za
dhahabu na simu.
Mshitakiwa adaiwa kukiri
Wakili Mwita alidai kuwa
wakaguzi wa Polisi, Latifa
Mohamed, ASP Jumanne
Malangehe na Koplo Mwaka
walienda Arusha kwa ajili ya
kufanya mahojiano na upekuzi
nyumbani kwa mshitakiwa
Miriam.
Alidai Agosti 7, 2016 akihojiwa na
wakaguzi hao, mshitakiwa huyo
alikiri kuhusika kupanga mpango
wa mauaji na aliwaelekeza
maeneo walikokuwa wanapangia
mpango huo. Alidai mbali na
kukiri kosa hilo mbele ya askari
hao ambao waliandika maelezo
yake, pia mshitakiwa alikiri
kutenda kosa hilo mbele ya Mlinzi
wa Amani (Hakimu wa Mahakama
ya Mwanzo). Alidai wakaguzi hao
wa polisi walirudi Dar es Salaam
na Miriam, wakiongozana na
wachunguzi wa picha za kawaida
na za video kutoka makao makuu
ya polisi na Miriam aliwapeleka
sehemu ambayo walikuwa
wanakutana na Getrude kwa ajili
ya kufanikisha mauaji hayo.
Wakili Mwita alidai katika
maelezo hayo ambayo
mshitakiwa wa kwanza aliyatoa
kwa askari na mbele ya Mlinzi wa
Amani, alieleza kuwa aliamua
kutenda kosa hilo kutokana na
mgogoro wa mali za mumewe
yaani Bilionea Msuya.
Pia, walidai kuwa mshtakiwa
huyo aliamua kutenda kosa hilo
kwa hasira kutokana na Aneth
kumtumia picha za kukashfu
umbile lake. Wakili Mwita alidai
mshitakiwa alieleza kuwa Aneth
alikuwa akimtumia picha za
wanawake wenye maumbile
makubwa mabaya, wenye
matumbo makubwa, jambo
ambalo lilimfanya apate hasira.
Alidai kwa mujibu wa maelezo
yake, mshitakiwa Miriam baada ya
kuchukizwa na kitendo cha wifi
yake kumtumia picha hizo
alizoziona kama za kumkashfu,
aliamua kutafuta ushauri kwa
mshitakiwa wa pili Muyella,
ambaye alimshauri kuwa huyo
dawa yake ni kumuua tu.
Wakili Mwita alidai baada ya
ushauri huo wa mshitakiwa wa
pili walikubaliana mshtakiwa wa
kwanza amlipe mshitakiwa wa
pili Sh20 milioni kwa ajili ya kazi
hiyo.
Alidai washitakiwa hao baada ya
makubaliano hayo ndipo
walipopanga na kutekeleza
mauaji hayo, na kwamba
mshtakiwa wa kwanza alimlipa
mshtakiwa wa pili Sh10 milioni
kwanza wakiwa jijini Dar es
Salaam na baada ya kutekeleza
mauaji hayo, alimmalizia Sh10
milioni jijini Arusha.
Soma zaidi: Jalada la Mke wa
Bilionea Msuya latua kwa DPP
Wakili Mwita aliieleza mahakama
kuwa mshitakiwa wa pili baada
ya kukamatwa na kuhojiwa
alikubali kumfahamu mshitakiwa
wa kwanza kuwa ni
mfanyabiashara mwenzake na
alikuwa akifahamiana na
marehemu mumewe, lakini
alikana kuhusika na mauaji hayo.
Soma zaidi: Upelelezi kesi ya mke
wa Bilionea Msuya wakamilika
Licha ya kukana kuhusika katika
mauaji hayo, Wakili Mwita
aliieleza mahakama kuwa
mshitakiwa huyo alitambuliwa na
shahidi mmoja (ambaye ni shahidi
muhimu kwenye kesi hiyo)
kwenye gwaride la utambuzi. Kwa
upande wake Wakili Nguka alidai
Agosti 4, 2016 timu ya upelelezi
kutoka Dar es Salama ilisafiri hadi
Arusha kwa ajili ya kumkamata
Miriam na walimkamata.
Wakili Nguka alidai Miriam
alikamatwa akiwa katika klabu ya
Tembo iliyopo Arusha kisha askari
hao waliongozana na mshitakiwa
huyo hadi nyumbani kwa
mshtakiwa na kuanza upekuzi.
Alidai katika upekuzi huo ulioanza
saa saba mchana hadi saa 10 jioni,
timu hiyo ya upekuzi ilichukua
suti mbili ikiwemo ya rangi ya
bluu na nyekundu, cheni za
dhahabu na viatu jozi mbili.
Alidai Miriam alikiri kuhusika
katika mauaji ya wifi yake
kutokana na mgogoro wa
kifamilia. Hata hivyo, kwa mujibu
wa maelezo ya mashahidi hao,
Miriam alipendekezwa na familia
ya mumewe, Bilionea Msuya, na
akateuliwa na mahakama kuwa
msimamizi wa mirathi ya
mumewe. Baadaye mshitakiwa
huyo alilalamikiwa na ndugu wa
marehemu kwa ufujaji wa mali na
kwamba kutokana na kushindwa
kuwasilisha mahakamani
mrejesho wa usimamizi na
mgawanyo wa mali hizo,
mahakama iliamua kumuondoa
katika usimamizi wa mirathi hiyo.
Kutokana na hali hiyo, mshtakiwa
huyo aliomba ushauri wa
mfanyabaishara aitwaye Muyella
kuhusiana na mgogoro huo na
kumueleza kuwa Aneth amekuwa
akimuingilia katika mirathi na
mali alizoachiwa na mume wake.
Kwa mujibu wa maelezo ya
mashahidi hao, baada ya
mahakama kumuondoa katika
usimamizi wa mirathi, kikao cha
familia kilimpendekeza dada
mwingine wa marehemu Msuya
pamoja na baba wa marehemu
kuwa wasimamizi wa mirathi hiyo
lakini mshtakiwa Miriam aliweka
pingamizi.
View attachment 1243634
Aisee! Mali hizi!
 
sawa Mkuu lkn ukizungumzia Hukumu kabla ya upelelezi mnakosea, huyu Mama kapanga mipangilio ya mauaji ndio maana kuna MANSLAUGHTER na MURDER upelelezi kwa DPP bado, mara ya mwisho ilikuwa Julai mwaka huu leo November
kwenye RED km huyu mshikaji kawataja waliokamata kisu na kuua au aiwashuhudia pale chumbani wameshakamatwa basi hukumu ipo na jamaa yako na Mke wa Bilionea hawahusiki wao wataambulia kifungo na wakitoka watarejea Uraiani na Mama akaendelee na usimamizi wa mirathi. Nionavyo mm il revenge itakuwepo tu kwa watu hawa mpaka akosekane mshindi
Hii kesi mama atahukumiwa kwa kupanga mauaji,hata aliemuua erasto alihukumiwa kwa kupanga mauaji yani kudhamini watu waue na kuwalipa
 
Main character wa sakata lote hilo ni mtoto wa kiume wa
marehemu.
Huyo kijana atafutiwe councelor au lawyer ili amshauri aache ulevi na kutegemea hao wajomba na wafilisi wengine.
Ajitahidi kumsomesha dada yake na ndg zake ili wawe na msingi mzuri.
Ajiepushe na magomvi na beef za kifamilia.
Ajiunge chuo asomee BManagement ili awe nguzo ya familia hiyo, ajitambue asibebwe kama kiwete.
Asimwamini saana huyo mama yake na mjomba, kama alimchinja shangazi yake hashindwi lolote.
Arudi kwa Babu Msuya apate ushauri mzuri
 
Back
Top Bottom