Je ni Sahihi Serikali Kubagua Umri katika Elimu ya Sekondari?

mambomengi

JF-Expert Member
May 16, 2009
829
242
Nimetatizwa na Serikali kutokuwachagua vijana 29 kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita eti kwasababu wanaumri unazidi miaka 25!
Je serikali inakumbatia ujinga? Nafikiri ingekuwa bora wale waliochelewa kusoma wasaidiwe (wasipendelewe) ili walau waweze kuelimika--sasa hawa 29 wamefaulu kwanini wasiendelee na masomo. Au Kauli mbiu ya serikali ni "Elimu ina mwisho"

Dk Kawambwa alisema mwaka 2010 wanafunzi waliochaguliwa walikuwa asilimia 83.52 ya wenye sifa, hivyo mwaka huu kuna ongezeko la asilimia 12.63, kwa awamu ya kwanza.Alisema wavulana 624 sawa na asilimia 2.42, hawakuchaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kutokana na sababu mbalimbali.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni kutokuwa na uwiano wa alama za masomo (credits), alama kutotimia na baadhi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 25.
Alisema wanafunzi 29 walikuwa na umri uliozidi miaka 25 ambao kisheria hauwaruhusu kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano kwa shule za Serikali
Source: Mwananchi.co.tz
 
Mmmmmh sijaipenda kwa kweli, maisha yenyewe haya ya kuunga unga hivi.
 
Sasa waliwaruhusu kufanya mitihani ya kidato cha nne ili iweje? Nadhani kuna kitu kina miss katika maelezo yao!
 
Hawa jamaa waliobaguliwa wanapaswa kumburuza Waziri Kawambwa Kortini. It is unfair, at least to me.
 
ndiyo matatizo ya viongozi wetu kila kitu kuongozwa kisiasa badala ya kitaaluma,,tangu lini elimu ikawa na mipaka ya umri??. Lisipotatuliwa hili ipo siku waziri atasema wale wote wenye miaka zaidi ya 30 hawaruhusiwi kujiunga na elimu ya juu bali ni wale wenye umri chin ya 30 tu ndiyo wanaruhusiwa.......wadau wa elimu , wadau wa haki za binadamu hili lazima lipatiwe ufumbuzi la sivyo nchi hii kielimu itaishia pabaya......kwa vile wao walipata nafasi ya kusoma basi hawataki wengine wapate nafasi hiyo....unamruhusu mtu kufanya mtihani wa o level lakin haumruhusu kuendelea na a level,mbona inaumiza sana.wangejua kusoma huku ukiwa na familia,majukumu kulivyo kugumu wala wasingeleta porojo hii.....tangu lini elimu ikawa na mwisho??? Hawajui kuwa elimu ndiyo mkombozi wa kila kitu iwe hata kiuchumi bila elimu utapata wapi ufahamu wa kujikomboa kiuchumi???......hii tanzania sasa tunakokwenda na maamuzi ya hawa viongozi wetu sijui wapi...hivi na sisi wananchi tukiamua tutakavyo je tutaelewana kweli???.....wasituamshe tuliolala kwani kitakachofuata ni kulala wao.....au wanaona kuelimika kwetu kunatusaidia kujitambua na kuzijua haki zetu???, kunapunguza wigo wa wao kuendelea kutunyanyasa na kutukandamiza pamoja na kutuibia....wadau wote mkilikemea hili kwa nguvu zenu zote naamini hawatafanikiwa na huu mpango wao mbovu unaotaka kuendeleza ujinga na umasikini wa akili badala ya kumtokomeza adui ujinga.
 
Hawa jamaa waliobaguliwa wanapaswa kumburuza Waziri Kawambwa Kortini. It is unfair, at least to me.

Ukweli wakipata wakili mzuri wanaweza kukomesha hii descrimination ya watawala wenu, wao wameshasahau kuwa hata Nyerere alianzisha elimu ya ngumbaru na Tz ikapanda chati kwa elimu, WAO KAZI KUUWA UWA KILA LILILOJEMA, AZIMIO LA ARUSHA NDIO KABISAA
 
Back
Top Bottom