Je, Ni sahihi mke wa mtu kuletewa chips na mpangaji mwenzio mwanaume ambaye hajaoa?

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,276
21,395
Hii ikoje wadau,

Kuna rafiki yangu mmoja anaishi nyumba za kupanga maeneo fulani jijini Dar, mwanzo alipenyezewa ubuyu na dogo mmoja mpangaji mwenzake kwamba, mkewe kila mara huletewa chips na jamaa mmoja mpangaji mwenzake bachela, anayefanya kazi katika bank moja hivi, yule jamaa anaporudi toka kazini husalimiwa kwa bashasha sana na yule mwanamke, na pengine jamaa huja na chips mbili yaani ya kwake na nyingine humgawia yule dada (mke wa mtu).

Yule jamaa mwenye mke alivyopenyezewa ubuyu huo akaamua kufanya uchunguzi, na akagundua kwamba na mkewe humpakulia chakula siku moja moja yule jamaa bachela na kumuhifadhia.

Sasa mwenye Mke kaona huu ukarimu usije mletea balaa, kamuuliza mkewe kuhusu tabia hiyo na mkewe kakubali na kumsihi mmewe kwamba aache “uchoyo” kwani anafanya hayo kwa nia njema ya ujilani mwema.

Mume kamaindi sana anatamani ahame pale, kanipigia simu kuniomba ushauri mimi kama rafiki yake, nimemwambia asihame kwa ghafla, maana kuhama ndiyo haswaa kutawafanya wapigiane simu ili wakutane; Je wewe unamshauri nini jamaa huyu?

Maana mkewe ni mashalaah kajaaliwa haswa,na amekuwa gumzo kwa wapangaji wenzake hususani mabachela, siku za wikend washikaji wakiwa nje wakipiga story “huyu mwanamke anapokuwa anatoka bafuni kuoga akiwa na kanga,huwa akifika mlangoni kwake hukung’uta miguu yake kwa kuipigapiga chini kwenye kapeti kwa zaidi ya sekunde 15 akiwa kama anafuta michanga miguuni.

Hiyo tabia wale vijana wanaitafsiri kuwa ni mbinu tu ya huyu dada kuwaumiza roho kwa ile vibration ya makalio yake yalivyo, sasa kwa kisa hiki huyu jamaa atakuwa salama kweli? Nimeipost humu kwakuwa wanaume wenye wake katika nyumba za kupanga wamekuwa wanaishi kwa presha sana na mabachela boy.

KARIBUNI
 
Hata nyumba ninayoishi pia yupo polisi mmoja ana tabia kama hiyo anamtafuna mke wa mpangaji mwenzetu. Hapo jamaa awe mkali tu amwambie achague ndoa au aendeleze uhusiano na jamaa na ndoa imshinde. Hizo ni dharau za wazi kabisa kumla mke wako ndani humohumo alafu unajua.
 
sasa yeye nae alijua kuwa akioa ndio atagegeda mwenyewe tuu??!! cha msingi yeye asihame ila amwambie tuu mke wake kuwa siku nikujua umegegedwa na mabachela, ujue siku hiyo huyo bachela na mie kwa pamoja tutakugegeda maana unapenda mb..ooo nyingi kwa wakati mmoja
 
Hata nyumba ninayoishi pia yupo polisi mmoja ana tabia kama hiyo anamtafuna mke wa mpangaji mwenzetu. Hapo jamaa awe mkali tu amwambie achague ndoa au aendeleze uhusiano na jamaa na ndoa imshinde. Hizo ni dharau za wazi kabisa kumla mke wako ndani humohumo alafu unajua.
Chanzo hivi huwa ni nini?
 
Ina maana mke alianza kuhifadhi food ya bachelor bila kumshirikisha mumewe? Hapo kuna tatizo. Why mwanamke aiweke rehani ndoa yake kiasi hicho kwa lengo tu la ujirani mwema? Ajiulize tu na yeye angejisikiaje kama mumewe angemnunulia chips mdada bachelor na huyo mdada bachelor akarudisha fadhila ya chakula. Mengine kwenye uhusiano wa wawili hayafai, Hata kama una huruma kiasi gani
 
Makubwa, unatafuta ushauri na kumsifia haswa shemeji yako eeeeh.

Sasa unaona kuwa na mke sijui mzuri sijui makalio...ina nini sasa,wakati tabia yake chafu anakula na mune na mpangaji jirani. Huyo kweli na tabia ya sijui kutoka bafuni ni mke wa kuringishia mmmmh... Mwachie aamue popote ataenda atakula na wenzake kama mbeba chips.
 
Ina maana mke alianza kuhifadhi food ya bachelor bila kumshirikisha mumewe? Hapo kuna tatizo. Why mwanamke aiweke rehani ndoa yake kiasi hicho kwa lengo tu la ujirani mwema? Ajiulize tu na yeye angejisikiaje kama mumewe angemnunulia chips mdada bachelor na huyo mdada bachelor akaruwadadadisha fadhila ya chakula. Mengine kwenye uhusiano wa wawili hayafai, Hata kama una huruma kiasi gani
nimejifunza kitu,kumbe kuna madada bachelor
 
Kama tatizo ni kutokuwa wachoyo,huyo mwenye mke mkarimu nae ajifunze ukarimu wa mkewe kwa yeye nae kumtafuta dada yoyote single humo ndani au jirani na aanze kumnunulia vizawadi kila akitoka kwenye shughuli zake bila kificho. Huyo mwanamke ataelewa upuuzi anaoufanya.
 
huyo mume aanze kumletea chips mkewe labda anataman sana chips ila mume ndo bahir.
 
Sijui hao wanawake mnatoaga wapi..

Hebu na huyo mwenye mke awe anaeletewa chakula na mwanamke huko ndani..pia mwenye mke awe anapeleka zawadi NONO kwa binti anayempelekea chakula..

Ndoa za ajabu hizi..
 
haya mambo ni bora kuoa ukishajenga kwako kabisa, hizi nyumba za kupanga zina changamoto nyingi sana maana unakua umezungukwa na watu wengi sana hivyo ndoa na mahusiano yanakua rehani.

cha msingi mwambie jamaa akae chini na mkewe na amueleze kua hiyo tabia inatishia uhai wa ndoa yao, kwanza huyo mpangaji mwenzenu haina sababu ya kumletea msosi mke wake
pili na jamaa inabidi ajichunguze maana mpaka jirani anamsaidia kumletea chipsi inaonyesha ni jinsi gani jamaa hayuko vizuri kwenye swala la kumpa vizawadi mke wake (kosa kubwa hili) hvyo ajirekebishe

permanent solution jamaa ajenge kwake, nyumba za kupanga sio mpango kabisa. litaisha hilo litakuja jingine kubwa la kuumiza kichwa zaidi, ajenge tu maana hamna namna nyingine
 
haya mambo ni bora kuoa ukishajenga kwako kabisa, hizi nyumba za kupanga zina changamoto nyingi sana maana unakua umezungukwa na watu wengi sana hivyo ndoa na mahusiano yanakua rehani.

cha msingi mwambie jamaa akae chini na mkewe na amueleze kua hiyo tabia inatishia uhai wa ndoa yao, kwanza huyo mpangaji mwenzenu haina sababu ya kumletea msosi mke wake
pili na jamaa inabidi ajichunguze maana mpaka jirani anamsaidia kumletea chipsi inaonyesha ni jinsi gani jamaa hayuko vizuri kwenye swala la kumpa vizawadi mke wake (kosa kubwa hili) hvyo ajirekebishe

permanent solution jamaa ajenge kwake, nyumba za kupanga sio mpango kabisa. litaisha hilo litakuja jingine kubwa la kuumiza kichwa zaidi, ajenge tu maana hamna namna nyingine
SI MPAKA AWE NA HUO UWEZO? HIVI UNAFIKILI KUJENGA MCHEZO?
 
Back
Top Bottom