Je, ni sahihi kwa wapinga Christmas ya 25 December kuchangamkia na kupokea Christmas bonus, promo, zawadi na n.k

EP cosmetics

JF-Expert Member
Oct 18, 2015
2,466
3,834
Wapendwa hongereni na poleni kwa majukumu ya hapa na pale. MERRY CHRISTMAS.

wakuu kawaida tunapoelekea mwisho wa mwaka wakristo huwa tunasikukuu moja kubwa ya kuzaliwa(kufanyika mwili) mkombozi wetu yaani Kristo Yesu, chistmas ambayo huwa ni tarehe 25 dec ya kila mwaka. na imekuwa ikifanyika tangu mwaka 336AD mpaka leo

Bahati mbaya sana kuna baadhi ya ndugu, marafiki, jamaa, wakristo wenzetu na hata wasio wakristo kwa sababu zao fulani fulani kila mmoja na yake hawaitambui, hawaikubali na kuipokea sikukuu hii ya Mungu kufanyika mwili (umwilisho) kwa ajili ya ukombozi wetu. kifupi kabisa kwao kufanya hivyo ni kosa, ni dhambi, ni kuungana na upagani, ni unbiblical au kinyume cha quran nk nk. binafsi ninaheshimu mawazo na sababu zao.

baada ya maelezo hayo hapo juu hoja yangu ya msingi ni hii.

JE, ni sahihi kwa hao ndugu zetu kutoa au kupokea zawadi zozote za christmas "christmas gifts" ?

JE, ni sahihi kwa hao ndugu zetu kushadidia na kupokea "christmas bonus" toka kwenye vituo vya kazi nk ?

JE, ni sahihi kwa hao ndugu zetu kuchangamkia na kununua products zozote zilizoko kwenye "christmas promo" ?

JE, ofa zozote zile ambazo ni matokeo ya christmas kuanzia "free bundles" nk zinawahusu ?

ninawatakia krismasi njema na maandalizi mema ya mwaka mpya.

KARIBUNI
 
FB_IMG_15458164326616894.jpg
 
Ukiwa Popoma ukasoma ukajibu bila kufikiri kwa Uyakinifu unaweza jiona mwamba, ila ukitafakari ipasavyo, umeuliza swali Fikirishi sana. Nafuatilia michango ya wadau hapo
 
Ukiwa Popoma ukasoma ukajibu bila kufikiri kwa Uyakinifu unaweza jiona mwamba, ila ukitafakari ipasavyo, umeuliza swali Fikirishi sana. Nafuatilia michango ya wadau hapo
ahsante kwa kunielewa vema
KARIBU SANA
 
Haina shida kabisa.
Kwa mfano mimi siamini katika Iddi yoyote ile(Am a christian)
Lakini mwislam akinitakia heri ya Iddi siwezi kukataa.
Nikipewa zawadi ya Iddi siwezi kukataa.
Nikienda kununua kitu nikakuta kina ofa ya sikukuu ya Iddi siwezi kukataa ofa hiyo.
Nimeishi na waislam kipindi cha Iddi walikuwa wanatuzawadiwa msosi yaani kiufupi tulikuwa tunasherekea nao.
Mambo mengine tumejifunga wenyewe na dini zetu ila hayana uzito mbele za Muumba.
Ni ajabu unaletewa zawadi ya christmas unaikataa kisa wewe ni Msabato au Mwislam(japo sio lazima kupokea)
Kumbuka imeandikwa
"Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku,mwingine aona siku zote kuwa sawasawa.Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku,huiadhimisha kwa Bwana;
-warumi14:5-6
Pia imeandikwa
"furahi nao wafurahiao lia pamoja nao waliao"
NOTE:kusherekea sikukuu kwa utukufu wa Mungu sio dhambi na kutosherekea sio dhambi.Ila kama unasherekea kwa utukufu wa shetani ni dhambi mf: sherehe za matambiko ya mizimu.
Kesi nyingine?
 
Haina shida kabisa.
Kwa mfano mimi siamini katika Iddi yoyote ile(Am a christian)
Lakini mwislam akinitakia heri ya Iddi siwezi kukataa.
Nikipewa zawadi ya Iddi siwezi kukataa.
Nikienda kununua kitu nikakuta kina ofa ya sikukuu ya Iddi siwezi kukataa ofa hiyo.
Nimeishi na waislam kipindi cha Iddi walikuwa wanatuzawadiwa msosi yaani kiufupi tulikuwa tunasherekea nao.
Mambo mengine tumejifunga wenyewe na dini zetu ila hayana uzito mbele za Muumba.
Ni ajabu unaletewa zawadi ya christmas unaikataa kisa wewe ni Msabato au Mwislam(japo sio lazima kupokea)
Kumbuka imeandikwa
"Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku,mwingine aona siku zote kuwa sawasawa.Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku,huiadhimisha kwa Bwana;
-warumi14:5-6
Pia imeandikwa
"furahi nao wafurahiao lia pamoja nao waliao"
NOTE:kusherekea sikukuu kwa utukufu wa Mungu sio dhambi na kutosherekea sio dhambi.Ila kama unasherekea kwa utukufu wa shetani ni dhambi mf: sherehe za matambiko ya mizimu.
Kesi nyingine?
mkuu ahsante kwa maelezo mazuri, nimekuelewa vizuri sana kwani ulichoelezea ni uhalisia na kielelezo cha upendo na umoja katika vitendo bila kujali tofauti zetu japo sizungumzii habari za "idd" ila "christmas" na yote yanayotufikia kwa jina la "christmas"

point na hoja yangu ipo kwenye mistari mitatu ya mwisho ya post yako.
 
mkuu ahsante kwa maelezo mazuri, nimekuelewa vizuri sana kwani ulichoelezea ni uhalisia na kielelezo cha upendo na umoja katika vitendo bila kujali tofauti zetu japo sizungumzii habari za "idd" ila "christmas" na yote yanayotufikia kwa jina la "christmas"

point na hoja yangu ipo kwenye mistari mitatu ya mwisho ya post yako.
Haujanielewa!
Nimetumia sikukuu ya Iddi kama mfano kwasababu mimi imani yangu haiitambui Iddi kama sikukuu kama ilivyo kwa wengine ambao imani yao haiitambui christmas kama sikukuu.
Nimetumia sikukuu ya Iddi kuonyesha kipi huwa nafanya kwenye sikukuu nisizoziami,ninsigeweza kutumia christmas kama mfano kwasababu mimi naisherehekea.
Umeelewa sasa?
Kesi nyingine?
 
Haujanielewa!
Nimetumia sikukuu ya Iddi kama mfano kwasababu mimi imani yangu haiitambui Iddi kama sikukuu kama ilivyo kwa wengine ambao imani yao haiitambui christmas kama sikukuu.
Nimetumia sikukuu ya Iddi kuonyesha kipi huwa nafanya kwenye sikukuu nisizoziami,ninsigeweza kutumia christmas kama mfano kwasababu mimi naisherehekea.
Umeelewa sasa?
Kesi nyingine?
Nimekuelewa kitambo mkuu. Sababu hata Mimi nafanana na wewe kimtazamo juu ya sikukuu njema kwa madhehebu mengine mathalani IDD nk

Uzi wangu na hoja yangu hasa kama umeosoma kwa umakini unawahusu wale wakejeli na wapinga Christmas kwa lugha kwamba ni ushetani, ni upagani, ni ushetani, lengo ni ibada za Mungu jua Wa kirumi na sio Yesu tunaemfahamu wewe na mimi. Sasa ndio ninahoji kuhusu Christmas bonus, offer, gifts nk waje watueleze kama ni halali au ni haramu ?
 
Haina shida kabisa.
Kwa mfano mimi siamini katika Iddi yoyote ile(Am a christian)
Lakini mwislam akinitakia heri ya Iddi siwezi kukataa.
Nikipewa zawadi ya Iddi siwezi kukataa.
Nikienda kununua kitu nikakuta kina ofa ya sikukuu ya Iddi siwezi kukataa ofa hiyo.
Nimeishi na waislam kipindi cha Iddi walikuwa wanatuzawadiwa msosi yaani kiufupi tulikuwa tunasherekea nao.
Mambo mengine tumejifunga wenyewe na dini zetu ila hayana uzito mbele za Muumba.
Ni ajabu unaletewa zawadi ya christmas unaikataa kisa wewe ni Msabato au Mwislam(japo sio lazima kupokea)
Kumbuka imeandikwa
"Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku,mwingine aona siku zote kuwa sawasawa.Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku,huiadhimisha kwa Bwana;
-warumi14:5-6
Pia imeandikwa
"furahi nao wafurahiao lia pamoja nao waliao"
NOTE:kusherekea sikukuu kwa utukufu wa Mungu sio dhambi na kutosherekea sio dhambi.Ila kama unasherekea kwa utukufu wa shetani ni dhambi mf: sherehe za matambiko ya mizimu.
Kesi nyingine?
Mkuu umemjibu vizuri sana, mleta mada, na na wengine wenye mtizamo kama wake.

Kutoa amini anachoamini mwingine, akunifanyi nishirikiane nae maeneo mengine.
Eti nisile nao, nisinunue vitu vilivyoshushwa bei, wakati huo, nisinywe nae, Watanzania hatuishi hivyo.

Kwa faida ya mleta mada, Sisi Waislam, hatupingi Crismas, bali sio waumini wa Kristo, Na wala waislam hawapingi ukristo, bali siyo waumini wa imani hiyo.

Ndiyo maana tunashiriana maeneo mengine tena yanayohusu Dini zetu, mfano sherehe za ndoa, sherehe za dini.

Usitumie neno kupinga, tumia wasioamini, Ndiyo maneno ya kiungwana.
 
mkuu ahsante kwa maelezo mazuri, nimekuelewa vizuri sana kwani ulichoelezea ni uhalisia na kielelezo cha upendo na umoja katika vitendo bila kujali tofauti zetu japo sizungumzii habari za "idd" ila "christmas" na yote yanayotufikia kwa jina la "christmas"

point na hoja yangu ipo kwenye mistari mitatu ya mwisho ya post yako.
Jamaa kakujibu vizuri tu sijui unataka nini, kwanye Dini hakuna Wapinzani, hili neno ni la shari.

Kwenye Dini wasio wa umini, (Wasiamini). Lakini kwenye mazishi, Sherehe tunashirikana bila kujali unazikwa kwa imani gani, ama sherehe ya imani gani.

Hata ndani ya Nyie wakristo, huwezi kumwita mnaetofautiana nae kanisa mpizani, bali huitwa thehebu lingine.
 
Mkuu umemjibu vizuri sana, mleta mada, na na wengine wenye mtizamo kama wake.

Kutoa amini anachoamini mwingine, akunifanyi nishirikiane nae maeneo mengine.
Eti nisile nao, nisinunue vitu vilivyoshushwa bei, wakati huo, nisinywe nae, Watanzania hatuishi hivyo.

Kwa faida ya mleta mada, Sisi Waislam, hatupingi Crismas, bali sio waumini wa Kristo, Na wala waislam hawapingi ukristo, bali siyo waumini wa imani hiyo.

Ndiyo maana tunashiriana maeneo mengine tena yanayohusu Dini zetu, mfano sherehe za ndoa, sherehe za dini.

Usitumie neno kupinga, tumia wasioamini, Ndiyo maneno ya kiungwana.
Nimekuelewa Mkuu.
 
Jamaa kakujibu vizuri tu sijui unataka nini, kwanye Dini hakuna Wapinzani, hili neno ni la shari.

Kwenye Dini wasio wa umini, (Wasiamini). Lakini kwenye mazishi, Sherehe tunashirikana bila kujali unazikwa kwa imani gani, ama sherehe ya imani gani.

Hata ndani ya Nyie wakristo, huwezi kumwita mnaetofautiana nae kanisa mpizani, bali huitwa thehebu lingine.
Mkuu Asante kwa maoni
Kama neno "kupinga" limekuwa sio zuri samahani kwa hilo. Sababu hata Mimi mwenyewe ni moja ya wafaidi katika shrerehe za IDD hivyo sina ugomvi na IDD wala imani zetu.

Lengo la Uzi kama umeusoma kwa umakini ni "Christmas" na sio "IDD" au imani zetu. Hivyo jaribu kumakinika na nilichoeleza kwenye uzi husika na sio nje ya hapo.

KARIBU
 
Back
Top Bottom