Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu jamiiforums.
Ndugu zangu watanzania;
Je, ni sahihi kwa baba wa kambo na baba mzazi (biological father) kwa pamoja kuhudhuria katika sherehe ya harusi ya binti yao? Ni busara ipi itumike?
HIKI KISA NI KIREFU SANA ILA NINAOMBA KUANDIKA KWA UFUPI
==========
Kuna siku moja nilihudhuria katika mazishi ya binti mmoja wa miaka kama 21 alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha CBE. Huyu binti baba yake mzazi ni kutoka katika kabila la Wahehe ila mama yake ni mkurya. Huyu mama alizaa tu na Muhehe ila hakuolewa naye bali akaja kuolewa na Mkurya mwezie.
Huyu mama hakuwahi kumwambia baba mzazi (Mhehe) kuhusiana na mila za watu wa mkoa wa Mara kuwa kama mwanamke akizaa bila kuolewa, ikija ikatokea akaolewa basi yule aliyelipa mahari anamchukua mpaka na mtoto anakuwa wa ukoo wake. Siku ya mazishi baba yake mzazi alikuwepo ila baba yake wa kambo (Mkurya) hakuwepo kwa maana alikuwa Ulaya kwa masomo.
Baba yake mzazi ndio ikabidi aende kuweka shahada katika kaburi ingawa msalaha ulikuwa unasoma jina la yule baba wa kambo. Baba mzazi alikasirika sana siku hiyo kwa maana alitaka jina la katika msalaba lisomeke la ukoo wake.
(mfano; ELIZABETH MARWA BADALA YA ELIZABETH MSIGWA) kwa maana kwa mila za watu wa mkoa wa Mara, kama ambavyo nimeeleza hapo juu ni kwamba kama mwanamke akizaa bila kuolewa, ikija ikatokea akaolewa basi yule aliyelipa mahari anamchukua mpaka na mtoto anakuwa wa ukoo wake.
Nimejaribu kuvuta picha vp endapo kama huyu binti asingekufa mapema hivi? Vp kama angefanikiwa kufika umri wa kuolewa miaka labda 26 ingekuwaje katika siku ya sherehe?
Je, ni sahihi kwa baba wa kambo na baba mzazi (biological father) kwa pamoja kuhudhuria katika sherehe ya harusi ya binti yao? Ni busara ipi itumike? Ukifika muda wa bibi harushi kutambulisha wazazi wake atamtambulisha nani kama baba?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ndugu zangu watanzania;
Je, ni sahihi kwa baba wa kambo na baba mzazi (biological father) kwa pamoja kuhudhuria katika sherehe ya harusi ya binti yao? Ni busara ipi itumike?
HIKI KISA NI KIREFU SANA ILA NINAOMBA KUANDIKA KWA UFUPI
==========
Kuna siku moja nilihudhuria katika mazishi ya binti mmoja wa miaka kama 21 alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha CBE. Huyu binti baba yake mzazi ni kutoka katika kabila la Wahehe ila mama yake ni mkurya. Huyu mama alizaa tu na Muhehe ila hakuolewa naye bali akaja kuolewa na Mkurya mwezie.
Huyu mama hakuwahi kumwambia baba mzazi (Mhehe) kuhusiana na mila za watu wa mkoa wa Mara kuwa kama mwanamke akizaa bila kuolewa, ikija ikatokea akaolewa basi yule aliyelipa mahari anamchukua mpaka na mtoto anakuwa wa ukoo wake. Siku ya mazishi baba yake mzazi alikuwepo ila baba yake wa kambo (Mkurya) hakuwepo kwa maana alikuwa Ulaya kwa masomo.
Baba yake mzazi ndio ikabidi aende kuweka shahada katika kaburi ingawa msalaha ulikuwa unasoma jina la yule baba wa kambo. Baba mzazi alikasirika sana siku hiyo kwa maana alitaka jina la katika msalaba lisomeke la ukoo wake.
(mfano; ELIZABETH MARWA BADALA YA ELIZABETH MSIGWA) kwa maana kwa mila za watu wa mkoa wa Mara, kama ambavyo nimeeleza hapo juu ni kwamba kama mwanamke akizaa bila kuolewa, ikija ikatokea akaolewa basi yule aliyelipa mahari anamchukua mpaka na mtoto anakuwa wa ukoo wake.
Nimejaribu kuvuta picha vp endapo kama huyu binti asingekufa mapema hivi? Vp kama angefanikiwa kufika umri wa kuolewa miaka labda 26 ingekuwaje katika siku ya sherehe?
Je, ni sahihi kwa baba wa kambo na baba mzazi (biological father) kwa pamoja kuhudhuria katika sherehe ya harusi ya binti yao? Ni busara ipi itumike? Ukifika muda wa bibi harushi kutambulisha wazazi wake atamtambulisha nani kama baba?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.