Je ni sahihi kutolea mkopo fungu la kumi?

Lagrange

JF-Expert Member
Mar 7, 2017
2,256
2,572
Wakuu habarini za wakti huu?

Nikiwa nasikiliza mahubiri redioni kama kawaida yangu ,nimeshutushwa na mahubiri ya leo ya Mchungaji Mpachi katika kituo cha redio cha Rock fm hapa Mbeya .

Mtumishi huyu wa Mungu anasema ni sharti unapo chukua mkopo uupeleke madhabahuni ukanenewe maneno ya baraka na kutolewa fungu la kumi:

Mtumishi akaendelea kutoa shuhuda za waumini wake kadhaa walio pata maanguko kutokana na kutopeleka mikopo yao madhabahuni.

Akaendelea kuhubiri kuwa kuna siku alienda kwa mkopeshaji mmoja ,akakuta ana matunguri kwenye droo ,katika hayo matunguri majina ya wakopaji yameandikwa na kiasi walicho kopa .

Mtumishi anadai akambananisha mkopeshaji, mkopeshaji akamwambia kuwa kabla ya kumkopesha mtu wanamchunguza kwanza kwenye ulimwengu wa roho kama anaweza kuwa mteja mzuri au la, Mkopeshaji akamwambia pia Mtumishi ili mtu aweze kurejesha mkopo ni lazima aupeleke madhabahuni ,na mtumishi akaongezea kuwa hupaswi kwenda mbele za Mungu mikono mitupu na ndicho kinacho wakimbiza watu ,akanukuu

" 15 Utaiweka sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu; utakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba kama nilivyokuagiza, kwa wakati uliowekwa, mwezi wa Abibu (kwa maana ndio mwezi uliotoka Misri); wala hapana mtu atakayeonekana mbele yangu na mikono mitupu;
Kutoka 23:15"

Wakuu najua hapa jamvuni kuna watu wana uzoefu mkubwa sana kwenye maisha katika nyanja mbalimbali ,karibuni tubadilishane mawazo katika hili.

Karibuni sana tujadili hichi kitu maana nimebaki njia panda Wakuu
 
Zaka ni asilimia 10 ya mapato yako yatokanayo na kazi uliyofanya, sasa hiyo ya mkopo unapaswa utoe shukurani na siyo zaka.

Pindi utakapoanza uzalishaji wowote kupitia huo mkopo ile faida/mapato ndipo unatoa 10percent ya Mungu na kuipeleka madhabahuni.

Hao wengine ni watumishi vibaka tu.
 
Zaka ni asilimia 10 ya mapato yako yatokanayo na kazi uliyofanya, sasa hiyo ya mkopo unapaswa utoe shukurani na siyo zaka.
Pindi utakapoanza uzalishaji wowote kupitia huo mkopo ile faida/mapato ndipo unatoa 10percent ya Mungu na kuipeleka madhabahuni.
Hao wengine ni watumishi vibaka tu.

Sasa mkuu ukitoa hizo 10% za zaka bado kodi ,bado riba utarejesha hela yaa watu kweli.

Ulokole ni kazi sana Mkuu ,,
 
Utoaji wa zaka siyo takwa la mtu fulani.
Sasa mkuu ukitoa hizo 10% za zaka bado kodi ,bado riba utarejesha hela yaa watu kweli. Ulokole ni kazi sana Mkuu ,.
Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Mtazamo wako ubadilishe baada ya kusoma hapo 👆. Jifunze kwa muanzilishi wa dawa ya meno ya colgeti sasa hivi anatoa zaka mara kumi kuliko inayoamliwa na maandiko.

Uzuri wa Mungu ameahidi makubwa sana kupitia kumtolea kidogo sana kulingana na mapato yako ndiyo maana ukipata faida as 1000/- unampa Mungu 100/- wewe unabaki na 900/-
 
kwani umeelewa vizuri alichokiandika?


Ndio ,,namaanisha kutoa 10% ya mkopo ukisha chukua kabla ya kufanya chochote.

Je hapo mtu utaweza kurejesha hela ya bank kweli ,mfano mtu umekopa 30,000,000 unatakiwa utoe 3,000,000 madhabahuni kabla hujaanza kufanyia biashara na huwo mkopo. Katika mazingira hayo inaweza kumiwiya mtu ngumu sana kurejesha mkopo.
 
Wakuu habarini za wakti huu?

Nikiwa nasikiliza mahubiri redioni kama kawaida yangu ,nimeshutushwa na mahubiri ya leo ya Mchungaji Mpachi katika kituo cha redio cha Rock fm hapa Mbeya .

Mtumishi huyu wa Mungu anasema ni sharti unapo chukua mkopo uupeleke madhabahuni ukanenewe maneno ya baraka na kutolewa fungu la kumi:

Mtumishi akaendelea kutoa shuhuda za waumini wake kadhaa walio pata maanguko kutokana na kutopeleka mikopo yao madhabahuni.

Akaendelea kuhubiri kuwa kuna siku alienda kwa mkopeshaji mmoja ,akakuta ana matunguri kwenye droo ,katika hayo matunguri majina ya wakopaji yameandikwa na kiasi walicho kopa .

Mtumishi anadai akambananisha mkopeshaji, mkopeshaji akamwambia kuwa kabla ya kumkopesha mtu wanamchunguza kwanza kwenye ulimwengu wa roho kama anaweza kuwa mteja mzuri au la, Mkopeshaji akamwambia pia Mtumishi ili mtu aweze kurejesha mkopo ni lazima aupeleke madhabahuni ,na mtumishi akaongezea kuwa hupaswi kwenda mbele za Mungu mikono mitupu na ndicho kinacho wakimbiza watu ,akanukuu

" 15 Utaiweka sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu; utakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba kama nilivyokuagiza, kwa wakati uliowekwa, mwezi wa Abibu (kwa maana ndio mwezi uliotoka Misri); wala hapana mtu atakayeonekana mbele yangu na mikono mitupu;
Kutoka 23:15"

Wakuu najua hapa jamvuni kuna watu wana uzoefu mkubwa sana kwenye maisha katika nyanja mbalimbali ,karibuni tubadilishane mawazo katika hili.

Karibuni sana tujadili hichi kitu maana nimebaki njia panda Wakuu
Peleka shukrani ambayo haitakuathiri kufanya kazi na huo mkopo wako kadri ya malengo yako

Zako Ni sehemu ya mapato yako...mkopo sio mapato...fanya kazi na mkopo faida utaipiga 10 percent umtolee Bwana Mungu wetu

Angalizo usiende kuomba ushauri huu kwa mchungaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zaka ni asilimia 10 ya mapato yako yatokanayo na kazi uliyofanya, sasa hiyo ya mkopo unapaswa utoe shukurani na siyo zaka.

Pindi utakapoanza uzalishaji wowote kupitia huo mkopo ile faida/mapato ndipo unatoa 10percent ya Mungu na kuipeleka madhabahuni.

Hao wengine ni watumishi vibaka tu.
Nmekuelewa vzur

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ,,namaanisha kutoa 10% ya mkopo ukisha chukua kabla ya kufanya chochote.

Je hapo mtu utaweza kurejesha hela ya bank kweli ,mfano mtu umekopa 30,000,000 unatakiwa utoe 3,000,000 madhabahuni kabla hujaanza kufanyia biashara na huwo mkopo. Katika mazingira hayo inaweza kumiwiya mtu ngumu sana kurejesha mkopo.
Mkopp hautoi fungu la kumi kaFanye ulichopanga faida ya hyo biashara ndio toa fungu la kumi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Peleka shukrani ambayo haitakuathiri kufanya kazi na huo mkopo wako kadri ya malengo yako

Zako Ni sehemu ya mapato yako...mkopo sio mapato...fanya kazi na mkopo faida utaipiga 10 percent umtolee Bwana Mungu wetu

Angalizo usiende kuomba ushauri huu kwa mchungaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Iko sahihi Mkuu 100%
Anapaswa afuate ushauri huu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pale panapotoka ile kodi ya mapato ndo panapotoka fungu la kumi. Sasa uje uniambie kodi inatokaga kwenye mtaji .Na kama ukifanikiwa kuulipa huo mkopo hautaitaji kuutolea fungu la kumi kwa umeulipa kutokana na mapato ambayo tayari ulikuwa unayalipia zaka au kodi. Ni jambo rahisi tuu wewe ukikopa haulipi kodi yeyote kwenye mkopo kwa hiyo hata zaka hailipwi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ,,namaanisha kutoa 10% ya mkopo ukisha chukua kabla ya kufanya chochote.

Je hapo mtu utaweza kurejesha hela ya bank kweli ,mfano mtu umekopa 30,000,000 unatakiwa utoe 3,000,000 madhabahuni kabla hujaanza kufanyia biashara na huwo mkopo. Katika mazingira hayo inaweza kumiwiya mtu ngumu sana kurejesha mkopo.
Mambo yakiyumba mchungaji atakuombea Benki Wasahau deni lako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utoaji wa zaka siyo takwa la mtu fulani.

Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Mtazamo wako ubadilishe baada ya kusoma hapo . Jifunze kwa muanzilishi wa dawa ya meno ya colgeti sasa hivi anatoa zaka mara kumi kuliko inayoamliwa na maandiko.

Uzuri wa Mungu ameahidi makubwa sana kupitia kumtolea kidogo sana kulingana na mapato yako ndiyo maana ukipata faida as 1000/- unampa Mungu 100/- wewe unabaki na 900/-
Imeariwa 10% hivyo 10×10= 100%hivyo habakiwi na kitu.Acha uongo sema vya kwa yesu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom