scramble
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 1,593
- 256
kwanza nianze kwa kusema kuwa mimi siyo mwanasheria. haya ni mawazo yangu ya kawaida. nitashukuru wanaoifahamu sheria wakiniweka wazi kwa faida ya watanzania wenzangu. kwanza nampongeza jaji warioba na timu yake kwa kazi nzuri waliyofanya! rasimu ipo mbele yetu. tuisome watanzania ili tupendekeze marekebisho katika maeneo ambayo tunaona hayajakaa sawa. kuna maswali najiuliza. 1. JE NI SAHIHI KATIBA YA MUUNGANO KUITANGULIA KATIBA YA TANGANYIKA? mmmmhhh! mimi bado nashangaa rasimu ya katiba ya muungano kutangulia kabla ya ile ya Tanganyika au Tanzania bara kupatikana. Zanzibar wana katiba yao. Tanganyika haina katiba yake. hamuoni kuwa kutanguliza ya muungano ni kumfanya MTOTO AZALIWE KABLA YA WAZAZI WAKE? NAULIZA SWALI: Ina maana ikitungwa ya bara baadaye na baadhi ya maoni yakakinzana na hii ya muungano, ya muungano itaguswa tena! hamdhani kuwa ya muungano lazima itaiburuza ya bara iandikwe kwa kufuata vipengele vya hii ya muungano. hamdhani kuwa ikitungwa ya Tanganyika kutakua na tafrani kubwa. hivi kazi yetu kwa miaka miwili au mitatu ijayo itakua malumbano ya katiba? mmmmmhhhh! ka nchi haka kana mambo. 2. JE SIYO KWAMBA HALI ITAKUA ILEILE YA SERIKALI MBILI KUTOKANA NA KATIBA YA BARA KUBURUZWA NA ILE YA MUUNGANO? KAMA NI HIVYO TUNAHARIBU PESA ZA NINI? sikatai katiba mpya lkn ilikua ipatikane katiba ya bara kwanza kisha tuandike katiba ndogo isiyozidi kurasa 15 inayozungumzia mambo ya muungano ambayo kwa maoni ya sasa hayazidi 7. hii rasimu, nionavyo ni katiba ya bara iliyochanganywa na mambo ya muungano! ka nchi haka kana mambo!!!!!!! naomba kusaidiwa kuhusu maswali yangu wadau!