Je, ni sababu gani zinazosababisha mimba za utotoni na kupelekea Wasichana wadogo kuwa Mama katika Umri mdogo

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1606209104877.png


Imeandikwa na: Jukwaa la Utu wa Mtoto - Children’s Dignity Forum (CDF)

Source: “Sikujua Nilipataje Mimba,” Utafiti Shirikishi kuhusu Mimba za Utotoni na kuwa Mama katika Umri mdogo uliofanywa Wilayani Mpwapwa, Tanzania: (2018)

Mimba za utotoni ni moja ya changamoto kubwa ya kiuchumi na kijamii nchini. Asilimia 27 ya wasichana kati ya umri wa miaka 15-19 wamepata ujauzito. Sababu kuu ya mimba za utotoni ni kipato cha chini cha kaya. Hali hii huwalazimisha wazazi kuwaozesha mabinti chini ya miaka 18 ili kupunguza majukumu ya kuwalea. Pia, husababishwa na matarajio ya familia ya binti kupata mahari inayotolewa na mume au familia ya mume.

Mambo mengine yanayochochea mimba za utotoni ni ukosefu wa miongozi ya wazazi kuhusu malezi ya watoto wao, biashara ya ngono na vishawishi kutoka kwa marafiki. Kuwepo kwa uelewa mdogo na huduma zisizo rafiki za afya ya uzazi kwenye jamii zao na pia vitendo vya ubakaji.

“Changamoto ya kuwa msichana au mwanamke kwenye jamii yetu ni kwamba wasichana hulazimishwa kuolewa katika umri mdogo ili walipiwe mahari ambayo inaweza kutumika kulipa mahari ya kaka yake anapooa. Jirani yangu aliozesha binti yake na mahari aliyopewa ilitumika kulipa mahari ya mke wa kaka yake.” (Sarah 13, Mpwapwa)

“Wavulana wana tabia ya kuwabaka wasichana, ambapo hujificha vichakani wakati wasichana wanapokuwa wanakwenda kutafuta kuni.” (Faith 16, Mpwapwa)
 
Mmomonyoko wa maadili na utanda wazi nayo ni sababu, kipindi hiki kukutana nqa msichana na kutongoza ni rahisi sana, sehemu ya kuktania ni nyingi, barabarani, shuleni,kwenye sherehe mbalimbali, pia simu za mikononi nazo zimerahisisha mahusiano.
 
Sababu kubwa ni jamii na mazingira na umasikini.

Mtoto anapokea, kuiga au kutengeneza personality itakayoendana na jamii na mazingira yaliyomzunguka
Kwa asilimia kubwa jamii zetu zimezungukwa na mawazo ya ngono na tabia nyingine chafu sababu ya umasikini.

Hivyo huyo mtoto atakayezaliwa hapo ni lazima awe part ya jamii hiyo awe msichana au mvulana.

Hivyo unavyosema wavulana hubaka sio kweli bali hao wasichana ndio wamekubali sababu na wao ni part ya hiyo jamii mbovu iliyozungukwa na mawazo ya ngono.

Sheria itungwe upya ili kuzuia mimba za utotoni.
Wavulana wana tabia ya kuwabaka wasichana, ambapo hujificha vichakani wakati wasichana wanapokuwa wanakwenda kutafuta kuni
 
Sasa hapa nani mwenye makosa, je, ni hawa watoto wa kike au huyu mtu mzima anayemtongoza mtoto. Maadili yawe kwa pande zote. Ndio mana basi, elimu ya kujitambua na afya ya uzazi, maadili vinatakiwa kutolewa kote kwa watoto wa kiume na wa kike, ili wote wajue haki na wajibu wao.
 
Mmomonyoko wa maadili na utanda wazi nayo ni sababu, kipindi hiki kukutana nqa msichana na kutongoza ni rahisi sana, sehemu ya kuktania ni nyingi, barabarani, shuleni,kwenye sherehe mbalimbali, pia simu za mikononi nazo zimerahisisha mahusiano.
Maadili, maadili ni ziro!! Hii kitu ukiitafakari saaaana huwezi ukatoa suluhisho. It is quite impossible. Every thing have changed nowadays. Every thing!!! Ndoa, elimu, kujituma, heshima, population, nk. The world has changed a lot my friends, a lot!! It is a pity!
It is hard to believe, but tuamini kwamba Mungu alituumba akiwa na kusudi zuri sana, lakini, well, tukataka kujitegemea, then akatuacha na kukaa pembeni akiangalia tamasha!! Afanye nini????????
 
Mmomonyoko wa maadili na utanda wazi nayo ni sababu, kipindi hiki kukutana nqa msichana na kutongoza ni rahisi sana, sehemu ya kuktania ni nyingi, barabarani, shuleni,kwenye sherehe mbalimbali, pia simu za mikononi nazo zimerahisisha mahusiano.
Kwanza nikurekebishe HAKUNA MIMBA ZA UTOTONI kwa maana hiyo hakuna mtoto anaye shika mimba.
 


Imeandikwa na: Jukwaa la Utu wa Mtoto - Children’s Dignity Forum (CDF)

Source: “Sikujua Nilipataje Mimba,” Utafiti Shirikishi kuhusu Mimba za Utotoni na kuwa Mama katika Umri mdogo uliofanywa Wilayani Mpwapwa, Tanzania: (2018)

Mimba za utotoni ni moja ya changamoto kubwa ya kiuchumi na kijamii nchini. Asilimia 27 ya wasichana kati ya umri wa miaka 15-19 wamepata ujauzito. Sababu kuu ya mimba za utotoni ni kipato cha chini cha kaya. Hali hii huwalazimisha wazazi kuwaozesha mabinti chini ya miaka 18 ili kupunguza majukumu ya kuwalea. Pia, husababishwa na matarajio ya familia ya binti kupata mahari inayotolewa na mume au familia ya mume.

Mambo mengine yanayochochea mimba za utotoni ni ukosefu wa miongozi ya wazazi kuhusu malezi ya watoto wao, biashara ya ngono na vishawishi kutoka kwa marafiki. Kuwepo kwa uelewa mdogo na huduma zisizo rafiki za afya ya uzazi kwenye jamii zao na pia vitendo vya ubakaji.

“Changamoto ya kuwa msichana au mwanamke kwenye jamii yetu ni kwamba wasichana hulazimishwa kuolewa katika umri mdogo ili walipiwe mahari ambayo inaweza kutumika kulipa mahari ya kaka yake anapooa. Jirani yangu aliozesha binti yake na mahari aliyopewa ilitumika kulipa mahari ya mke wa kaka yake.” (Sarah 13, Mpwapwa)

“Wavulana wana tabia ya kuwabaka wasichana, ambapo hujificha vichakani wakati wasichana wanapokuwa wanakwenda kutafuta kuni.” (Faith 16, Mpwapwa)
Kwanza nikurekebishe HAKUNA MIMBA ZA UTOTONI kwa maana hiyo hakuna mtoto anaye shika mimba.
 
Kwanza nikurekebishe HAKUNA MIMBA ZA UTOTONI kwa maana hiyo hakuna mtoto anaye shika mimba.
Mimba za utotoni zipo, wanaopata mimba hizi ni watoto. Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, inatambua kuwa mtoto ni mtu yeyote aliye chini ya miaka 18, kwa hiyo basi msichana wa miaka 17 au 11 akipata ujauzito, huyu ni mtoto aliyepewa ujauzito.
 
Kama wasichana wanaoongelewa ni walioozwa na wazazi wao kwa watu wazima, basi tatizo ni umasikini be ujinga wa hizo jamii. Ile kama wasichana wanaoongelewa ni hawa wanaozalishwa na watoto wenzao, sababu ni asili ya ubinadamu, kinachokosekana ni elimu juu ya maumbile yao na tahadhari wanazotakiwa kuchukua wanapojamiiana.
 
Mimba za utotoni zipo, wanaopata mimba hizi ni watoto. Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, inatambua kuwa mtoto ni mtu yeyote aliye chini ya miaka 18, kwa hiyo basi msichana wa miaka 17 au 11 akipata ujauzito, huyu ni mtoto aliyepewa ujauzito.
Achana na nadharia bana hakuna mtoto anaye pata mimba acheni kudanganyana huko na watu wanao tafuta ulaji ,mtoto hawezi kupata mimba kamwe.
 
Mimba za utotoni zipo, wanaopata mimba hizi ni watoto. Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, inatambua kuwa mtoto ni mtu yeyote aliye chini ya miaka 18, kwa hiyo basi msichana wa miaka 17 au 11 akipata ujauzito, huyu ni mtoto aliyepewa ujauzito.
Achana na nadharia bana hakuna mtoto anaye pata mimba acheni kudanganyana huko na watu wanao tafuta ulaji ,mtoto hawezi kupata mimba kamwe.
 
Ni kiherehere chao by jakaya mrisho kikwete
Mmomonyoko wa maadili na utanda wazi nayo ni sababu, kipindi hiki kukutana nqa msichana na kutongoza ni rahisi sana, sehemu ya kuktania ni nyingi, barabarani, shuleni,kwenye sherehe mbalimbali, pia simu za mikononi nazo zimerahisisha mahusiano.
 
Vishawishi vya marafiki,ndugu,jamaa na majirani. Kuna kijiji huwa naenda kutembea msichana/mvulana ukiwa na miaka 20 na kuendelea halafu huna mtoto unaonekana kituko. Wao hawajali ni singel mother,wa ndoa etc ujanja kwao ni kuwa na mtoto au watoto
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom