Je, ni nini kinacholitesa a taifa hili kwa sasa?

Shida kubwa inayolikumba taifa letu ni kukosa priorities. Shida zetu, matatizo yetu yanafahamika vizuri sana. Mfano, kuna idadi kubwa sana ya watu wanaishi kando kando ya vyanzo vya maji lakini mpaka leo hawana maji safi na salama. Utashangaa kuona wanatumia maji hayohayo wao na mifugo wao. Tatizo lingine ni kuwaamini sana wanasiasa kwamba ndio watatuletea kila hitaji letu la maisha. Tatu ni kuwaza matukio ya kisiasa na kuyapa kipaumbele kuliko maisha yetu ya sasa na yajayo. Mtu anachaguliwa leo baada ya mwaka au miezi anaanza kujupanga kwamba atarudi au hatarudi kwenye uchaguzi ujao. Nne bado tuna viongozi wanaojisahau kuwatumikia watu. Kiongozi anachaguliwa anaacha eneo lake la kiutawala anahamia sehemu nyingine hasa mijini ili kukidhi matakwa yake binafsi. Tano bado wananchi hatuna nguvu za kuwawajibisha viongozi wetu. Mfano kiongozi anapiga kampeni anatoa ahadi kibao. Akishindwa kuzitekeleza hatuna namna ya kumuwajibisha. Sita bado chaguzi zetu zimejaa makandokando. Saba bado sheria zetu ni butu sana. Nane bado elimu yetu haijamuwezesha mtu kuwa critical thinker. Tisa ubinafsi. Unakuta mwananchi ana kipato kizuri tu. Lakini mtaani anapoishi hata barabara anayopita kwenda na kutoka nyumbani kwake haipitiki au hakuna maji. Akishajitengenezea mazingira mazuri yake yeye na familia yake, wwngine muisubiri serikali. Mengine ongezeni.
Solution is the new Constitution that's ALL.
 
Viongozi wa Tanzania na Afrika nzima Wana ubinafsi wa Hali ya juu, siku zote wanajali na kupambana katika kufanikisha ya kwao kwani hata hao Ccm au Chadema Kuna ambao wanatumia tu kama kandambili na mwisho wa siku watakufa maskini kama Bado wapo hai mpaka sasa. Na shida nyingine ni wananchi wa nchi nyingi za Afrika ni waoga kupita maelezo., Wana akili ndogo kama punje ya ubuyu. Awake Africans from the darkness.
 
Upandaji wa bei kwa bidhaa mbalimbali unaoendelea ndani ya nchi yetu kwa sasa haujawahi kushuhudiwa kwa miongo kadhaa,watanzania wanaendelea kukomolewa na chama kilekile na serikali ileile toka uhuru wa nchi hii.na serikali iko kimya kabisa.watanzania wanaweza kudhani kuna serikali kumbe serikali ilishatoweka zamani sana.na ikishatokea hivyo kila kitu kinabaki ni uholela mtup.
 
tatizo ni kizazi fulani Cha viongozi fulani,hiki kingefutika kabisa ktk ardhi hii au kingepigwa ban kujihusisha na siasa nadhani Mambo yangekuwa sawa!!
 
Hivi WATU,SIASA SAFI NA UONGOZI BORA Vimeenda wapi na kwa nn tunaendelea kushuudia ulevi wa nadaraka ktk TAIFA HILI.
 
Back
Top Bottom