Uchaguzi 2020 Je, ni nani alikuwa nyuma ya biashara ya waunga juhudi? Je, imemlipa ama kala hasara kubwa?

Kwenye biashara yoyote usipokuwa makini unaangukia pua na kupata hasara kubwa, lakini si biashara tu tunakosea na kupatia mengi maishani mwetu kuanzia kwenye elimu, siasa, ajira mpaka mahusiano.

Ukikosea binafsi unaweza kujiadhibu ama kujisamehe mwenyewe lakini vipi kama ukikosea kitaasisi? Kwa hakika sheria itachukua mkondo hasa kwa mambo yale yaliyo rasmi.

Kwenye harakati hizi za siasa kama chama cha siasa kisipofuata taratibu na kanuni, mfumo huvurugika na matokeo yake kufanya mambo ambayo hata likitokea kosa ni vigumu kuwajibishana.

Mwaka 2018 ilianza biashara ya siri ya kununua viongozi wa upinzani katika kada mbalimbali, ni wazi lengo lilikuwa kuvuruga na pengine kuusambaratisha upinzani walioasisi mpango huo wakidhani upinzani ni viongozi wakatenga bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kutimiza huo mradi.

Bajeti hiyo na mradi huo havikuwa rasmi ndani ya chama na kwa hisia za wengi hilo lilikuwa jambo la wachache na pengine kwa maslahi yao binafsi bila kutafakari ya mbeleni.

Hakuna biashara inayokosa dalali ama mtu wa kati duniani, HAKUNA. Hii ni ajira inayoendesha maisha ya wengi, chochote kikishakuwa biashara ni ngumu kuepuka dalali labda tu iwe ni moja kwa moja kati ya muuzaji na mnunuzi.

Kwenye siasa pia kuna madalali hasa pale siasa inapogeuka biashara, madalali wa kisiasa ndio waliochombeza kwa karibu na kusimamia zoezi zima la biashara ya waunga juhudi.

Leo ile biashara ya siri iko upenuni peupe, badala ya faida mradi umekula hasara kubwa lakini huku madalali wakivimbiwa percent! Kwakuwa haikuwa biashara rasmi na ya wazi hivyo tunawajibishana chini kwa chini na kisirisiri.

Halisi kamwe haiwezi kuongozwa na bandia leo ule wimbo maarufu wa waunga juhudi na tafrija za mapokezi hatuvioni tena na vimeshazikwa kwenye makaburi ya sahau, waunga juhudi wale waliokuwa na tambo za kila aina sasa wamekuwa kama wendawazimu ndio sasa wanajua nini maana ya ile methali ya Waswahel. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.

Fundisho hili gumu na muhimu tunalipata katika awamu hii na uwekezaji huu ulioshindwa na kutia hasara kubwa huku mwananchi akikosa huduma muhimu. Sasa ni wakati wa kuadhibu.

Adhabu ya kwanza ni kwa wale waliorubuniwa almaarufu kama waunga juhudi.

Adhabu ya pili ni kwa warubuni, hawa kiama chao ni kwenye sanduku la kura.
Katika mambo ni ya ajabu kwenye utawala wa Magufuli ni waliokuwa wabunge wa upinzani kuhamia chama chake kinyemera halafu yeye kama mwenyekiti alikaa kimya kama vile hausiki.
 
Wamarekani wanavyopenda kuingilia cases kama hizi kwenye mataifa mengine, now wanaendelea kukusanya ushahidi tu. Siku utashangaa file linakuwa disclosed na mpaka waliokuwa wanamwagiza na kiasi cha pesa alichokuwa akikabidhiwa kitatajwa.
Hapo ndipo patakapokuwa patamu, kumbe kwa njia nyingine watu wanaichafua madhabahu unapofika muda wa kutubu wanalia haswa dhamira zikiwachoma ila madaraka yanapofusha
Sure! You are very right mkuu
 
Kutaka kwangu upinzani uchukue dola ni kwa ajili tu ya tu ya kutaka kuona hawa kunguru kijani watakavyokuwa wanatapatapa
 
Biashara imefeli na mtaji umeliwa 😂😂😂😂
Imegeuka White elephant project kwa chama ni aibu,ni fedheha kwa chama kikongwe,lakini pesa imetumika.

Yule mjumbe Halmashauri Kuu ya CCM alitaka majibu,lakini alijibiwa kuwa ndani ya CCM damu damu hawana kitu ndio sababu ya kusajiri kupitia dirisha dogo.

Pammoja na majibu hayo matokeo yake wajumbe wakaamua kuwapiga spana watia nia wa ubunge na udiwani waliopitia dirisha dogo la usajiri.
 
Kwenye biashara yoyote usipokuwa makini unaangukia pua na kupata hasara kubwa, lakini si biashara tu tunakosea na kupatia mengi maishani mwetu kuanzia kwenye elimu, siasa, ajira mpaka mahusiano.

Ukikosea binafsi unaweza kujiadhibu ama kujisamehe mwenyewe lakini vipi kama ukikosea kitaasisi? Kwa hakika sheria itachukua mkondo hasa kwa mambo yale yaliyo rasmi.

Kwenye harakati hizi za siasa kama chama cha siasa kisipofuata taratibu na kanuni, mfumo huvurugika na matokeo yake kufanya mambo ambayo hata likitokea kosa ni vigumu kuwajibishana.

Mwaka 2018 ilianza biashara ya siri ya kununua viongozi wa upinzani katika kada mbalimbali, ni wazi lengo lilikuwa kuvuruga na pengine kuusambaratisha upinzani walioasisi mpango huo wakidhani upinzani ni viongozi wakatenga bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kutimiza huo mradi.

Bajeti hiyo na mradi huo havikuwa rasmi ndani ya chama na kwa hisia za wengi hilo lilikuwa jambo la wachache na pengine kwa maslahi yao binafsi bila kutafakari ya mbeleni.

Hakuna biashara inayokosa dalali ama mtu wa kati duniani, HAKUNA. Hii ni ajira inayoendesha maisha ya wengi, chochote kikishakuwa biashara ni ngumu kuepuka dalali labda tu iwe ni moja kwa moja kati ya muuzaji na mnunuzi.

Kwenye siasa pia kuna madalali hasa pale siasa inapogeuka biashara, madalali wa kisiasa ndio waliochombeza kwa karibu na kusimamia zoezi zima la biashara ya waunga juhudi.

Leo ile biashara ya siri iko upenuni peupe, badala ya faida mradi umekula hasara kubwa lakini huku madalali wakivimbiwa percent! Kwakuwa haikuwa biashara rasmi na ya wazi hivyo tunawajibishana chini kwa chini na kisirisiri.

Halisi kamwe haiwezi kuongozwa na bandia leo ule wimbo maarufu wa waunga juhudi na tafrija za mapokezi hatuvioni tena na vimeshazikwa kwenye makaburi ya sahau, waunga juhudi wale waliokuwa na tambo za kila aina sasa wamekuwa kama wendawazimu ndio sasa wanajua nini maana ya ile methali ya Waswahel. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.

Fundisho hili gumu na muhimu tunalipata katika awamu hii na uwekezaji huu ulioshindwa na kutia hasara kubwa huku mwananchi akikosa huduma muhimu. Sasa ni wakati wa kuadhibu.

Adhabu ya kwanza ni kwa wale waliorubuniwa almaarufu kama waunga juhudi.

Adhabu ya pili ni kwa warubuni, hawa kiama chao ni kwenye sanduku la kura.
Madalali wa siasa CCM walikula huku na huku wanakula 10% pande zote kwa mnunuliwa na kwa mnunuzi
 
ukikosea binafsi unaweza kujiadhibu ama kujisamehe lakini vipi kama ukikosea Kitaasisi.?
 
Mkuu,

Mshana Jr,

Kumbe ndo maana deni la Taifa limekuwa kwa kasi.

Kumbe kulikuwa na biashara ya kununua wapinzaniBashiru na Polepole wanapashwa kulejeaha pesa ili tupungeze nadeni kwa mabebelu.
 
Mkuu,

Mshana Jr,

Kumbe ndo maana deni la Taifa limekuwa kwa kasi.

Kumbe kulikuwa na biashara ya kununua wapinzaniBashiru na Polepole wanapashwa kulejeaha pesa ili tupungeze nadeni kwa mabebelu.
Matumizi ya hovyo kwa kutumia pesa zetu yalikuwa mengi mno...kuna siku tukiyajua yote ...tutaweka msiba wa kitaifa
 
Back
Top Bottom