Je, ni Muhimu Kiasi gani?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,138
Je, ni Muhimu Kiasi gani?



Je, sex ni muhimu katika ndoa kiasi gani?
Wanandoa wengi wana struggle sana ili kuhakikisha ndoa yao inakuwa ya kuridhisha ingawa ni kweli ndoa yoyote imara huhitaji efforts kwa mke na mume ili mambo kila siku yawe mazuri na vicheko vya hapa na pale.

Swali la leo ni kwamba Je, baada ya ndoa kutokuwa na sex ni kitu gani kingine kinaweza kuwafanya wanandoa kushikana au kubaki na bond strong?
Je, ni familia yaani watoto na kule kujisikia ni mke na mume au ni urafiki wa kubaki kuishi kama dada na kaka walioamua kuishi pamoja?

Je, unaweza kuishi kwa kuridhika katika ndoa ambayo hakuna sex kwa hiari yaani si ugonjwa au tatizo ambalo daktari amethibitisha bali wanandoa wameamua tu?

Kila mmoja ana majibu yake ambayo anayo kichwani, mwingine atasema ndiyo na mwingine atasema hapana haiwezekani kuishi bila hiyo huduma.

Hata hivyo ni kweli sex ni muhimu sana katika ndoa, na ukishaingia kwenye ndoa ina maana kwamba umeingia mahali sahihi ambapo sex ni kitu cha bure na si dhambi, kwani sex ni mali ya ndoa, nje ya ndoa ni uchafu na laana kama si dhambi na kuwa na hatia.
Hii ina maana kama ni mwanandoa usipopata sex ndani ya ndoa huna sehemu nyingine ambayo unaweza kupata hiyo huduma.

Hii ina maana kwamba unayokazi ya kuhakikisha ndoa inakupa ridhiko na kuridhika huanza kwa kupata huduma muhimu kama sex.

Ni kweli siku hazifanani na hukuna ndoa ambayo kila siku na masaa yote 24 katika siku 365 na robo wanakuwa na hamu na sex, zipo siku kunakuwa na ukame na kuna siku kuna kuwa na mvua ya libido kwa wawili kuwa mwili mmoja.

Kuna njia nyingi za kuwa connected na kurudi kwenye mstari na kuruhusu mapenzi upya (intimacy), tatizo kubwa ni pale mmoja wa wanandoa anapojisahau na kukosa kuwa caring, gentle, tender na maneno mengine mengi tu ya kimapenzi kwa mwenzake.

Kitu kilicho muhimu kwetu ambao tumeoa na kuolewa ni kwamba sex ni haki yetu na tunahitaji kuwa wazi kueleza matarajio yetu, mahitaji yetu, interest zetu na vile tunajisikia au tunapenda wapenzi watu watufanyie.

Kwa wazazi wetu tulipata kila kitu ila kimoja tu ambacho ni sex na tumekubaliana kuishi pamoja kwanza ili kuondoa upweke na pili ili kuufurahia uumbaji kwa njia ya sex kwa mke na mume.
Ndoa yenye furaha na bora ni ile ambayo ina balance mizani katika vitu vitatu yaani
Kwanza ni mwili,
Pili ni nafsi na
Tatu ni roho.
Kimoja kikikosekana tu basi kasheshe huanza na tofauti huendelea kutafuna ndoa kisirisiri kama mchwa.

Ni ukweli usiopingika kwamba sex ni muhimu sana kwenye ndoa kwani ni kipimo cha wanandoa wapo karibu kiasi gani na zaidi jinsi gap la hitaji la mmoja kuhitaji huduma linavyozidi kuwa kubwa ndivyo na mambo mengine yatakavyoweza kuharibika na hatimaye migogoro mingine huzaliwa.

Inawezekana mume wako au mke wako ana hasira, ukali, majibu ya mkato, kuwa mbali na wewe, kutumia muda na rafiki zake au kufanya vitu vingine badala ya kukaa na wewe si kwa sababu ya makosa unafanya bali kutopenda kwako sex.

Sex si hitaji la mwili tu katika ndoa bali ni kuonesha (approval) kwamba mume au mke wangu ananipenda, ananihitaji, ananijali, ninamvutia na napendeza na zaidi kuwa connected.
Frustrations nyingi za wanandoa huanza kwa masuala ya kitandani kuwa baridi.
 
Back
Top Bottom