Je, ni mfumo wa JKN umetufanya kuwa watu wa ajabu namna hii?

ERoni

JF-Expert Member
Jan 9, 2013
43,528
89,643
Hello wana MMU!

Kuna mambo huwa yananitatiza, hasa katika maisha yetu ya kila siku. Binadamu lazima tuishi kwa kutegemeana, hakuna binadamu anayeweza kusema kuwa "mimi peke yangu naweza kuishi bila msaada wa ndugu/jirani/rafiki au mpita njia"

Lakini katika kuishi kwetu kwa kitegemeana, ni muhimu/lazima kujua mipaka yetu, wapi uwe karibu na mtu, wapi ujiweke pembeni, wapi unahitajika na wapi huhitajiki.

Mzee Nyerere alijitahidi sana katika ujamaa, aliamini katika ujamaa na alituaminisha(hasa sisi tuliokuwepo nyakati zake) kuwa ujamaa ndio suluhisho la maendeleo, hatuwezi kufika bila huo mfumo, sijui aliwaiga kina nani, China au Urusi? hata sijui. Lakini mfumo huu kwa maoni yangu ni mbovu na umeleta upuuzi mwingi sana kwa baadhi yetu.

Mifano midogo;
»Mtu amekuja mtaani ni mgeni, kila mtu atataka ajue ni nani, anatoka wapi.
»Mtaani kila mtu atataka ajue unaishi maisha gani, unafanya kazi gani, unatoka saa ngapi na kurudi saa ngapi
»Ukifanikiwa kidogo tu, kwa kitu kidogo ambacho hakina hata mantiki basi mtaani watu wataanza kukusema na vibaraza ili mradi tu siku ipite.
»Wanawake kukaa vibarazani toka asubuhi hadi jioni, kuongea mambo yasoyiwahusu.


Hiyo ni mifano michache tu.
Sasa najiuliza, ni mifumo ya JKN ndio inatufanya tusiwe watu wa ku-mind our business ila biznes za jirani zinakuwa zetu?

Je, nyie wenzangu mnaonaje hiyo tabia?
 
Ngoja niendelee kusoma job advertising hapa kwa muuza magazeti! Nikimaliza ntarudi.
 
Watu kutokuwa na shughuli za kufanya maana walio bize hawana muda wa kujadili mambo ya watu.
 
Mtani...

Kwani umehamia mtaa mpya ukakutana na hayo?

Mimi nadhani hilo la mgeni kuhamia mtaa fulani watau wakataka wajue ni nani na anafanya nini ni sawa. Kwa usalama wetu tusije kuishi na watu hatari bila ya sisi kujua.

Hiyo habari ya watu kujadili habari za mtu toka anatoka mpaka anaingia ni kukosa kazi. Na kama unavyosema huenda mfumo huo wa Ujamaa umechangia kutuharibu. Baadhi ya watu wakabweteka wakijua 'tutapata share'
Ila kwa namna maisha yanavyobadilika itafika wakati wale wa kukaa vibarazani kujadili ya wenzao hawatakuwa tena na huo muda,coz kila mtu atakula kwa jasho lake. Itabidi akatafute kazi au biashara. Muda wa kukaa kujadili flani kapata kapatapateje utakuwa haupo.
 
Watu kutokuwa na shughuli za kufanya maana walio bize hawana muda wa kujadili mambo ya watu.
Mkuu, unadhani kwa ubepari unaozidi kuja kwa kasi kukaa vibarazani na vijiweni kutaendelea kuwepo?
 
Mtani...

Kwani umehamia mtaa mpya ukakutana na hayo?

Mimi nadhani hilo la mgeni kuhamia mtaa fulani watau wakataka wajue ni nani na anafanya nini ni sawa. Kwa usalama wetu tusije kuishi na watu hatari bila ya sisi kujua.

Hiyo habari ya watu kujadili habari za mtu toka anatoka mpaka anaingia ni kukosa kazi. Na kama unavyosema huenda mfumo huo wa Ujamaa umechangia kutuharibu. Baadhi ya watu wakabweteka wakijua 'tutapata share'
Ila kwa namna maisha yanavyobadilika itafika wakati wale wa kukaa vibarazani kujadili ya wenzao hawatakuwa tena na huo muda,coz kila mtu atakula kwa jasho lake. Itabidi akatafute kazi au biashara. Muda wa kukaa kujadili flani kapata kapatapateje utakuwa haupo.
Mtani, nipo pale pale sijahama. Nikihama utakuwa wa kwanza kujua coz lazima unitembelee..teh teh.

Hiyo hoja yako kuwa mgeni lazima afahamike na watu wa mtaani ndipo haswa hoja yangu ilipo. Ni mfumo wa kijamaa ndio unafanya watu tudhani kuwa nikihamia mtaa A ni lazima kila mtu anijue, hata wasiostahiki kunijua. Imagine kama nakuja na documents zangu toka kwa kiongozi wa mtaa A, naleta kwa kiongozi wa mtaa B ananisajili na kujua ninapoishi, nyie wananchi mnataka kunijua kwa sababu zipi?
 
Hahaa ogopa sana nyumba ina wamama ambao ni jobless utajuta...kama unakaa nao nyumba moja au jirani nao watataka wakujue nje ndani. Unijue nje ndani we nani? Na ukiwa bize na mambo yako unaonekana unaringa
 
Back
Top Bottom