Je, ni Mambo gani yalikuwa ya kawaida sana miaka ya 1980s - 1990s ambayo Vijana wa sasa hawawezi kuyajua?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,014
Nakumbuka enzi hizo ilikuwa kawaida kabisa kusibiria kipindi cha muziki mida ya usiku huku ukiwa na kaseti yako, unasuburia wimbo unaoupenda ukifika unaurekodi, Tulikuwa tunasubiria usiku kwa sababu mchana Dj alikiwa anaongea akijisikia wakati mziki unacheza na wimbo anaweza kuukata mapema,

Enzi hizo hakukuwa na chanzo cha taarifa cha haraka kukujibia maswali, mfano unaweza kunywa coca cola ila ukitaka kujua nani alie itengeneza ilikuwa ni shughuli pevu kweli kweli, siku hizi ni mwendo wa google, wikipedia, n.k

Kuwasiliana kwa njia ya barua na watu wa mbali, Nakumbuka barua zikifika kama ni ya mpenzi wako ilikuwa unaoga kabisa na kula kabisa kabla hujaisoma, sikwambie mtu, watu walijua kuongea kupitia maandishi.

Kulikuwa na vijiwe vya kupeana habari na kukutana na washkaji, ukibaki nyumbani utaboreka sana kwanza inakubidi tu utoke nje maana wenzako wote wapo nje, hakukuwa na kubaki ndani unachati, upo instagram, netflix, n.k
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom