Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
Siku hizi toilet paper zinatumika kupapasi makalioHahahaha,
Dah?! Kweli umekumbuka mbali mazee.
Siku hizi toilet paper zinatumika kupapasi makalioHahahaha,
Dah?! Kweli umekumbuka mbali mazee.
Nimesoma na nimeelewa vizuri hii alama - inamaana kubwa sana
80-90
Duh nilikuwa chali wa miaka mitano ..sisi watoto wa mkapa tunatoka kapa hapa1999 ulikuwa wapi weye
Tufafanulie sisi vijana wa sasaVijana wa sasa hawajui kitu kinaitwa
- Reverse call
- TMO
- Pass book
Hah!!! Hatari sanaNa usisahau kipindi hicho kuangalia ni saa ngapi ilikuwa shughuli pevu. Nazungumzia kabla ya kuja zile saa zisizo na mishale (electronic). Watu wenye saa za uhakika walikuwa ni wachache tena wengi zilikuwa zinapoteza majira kishenzi. Vijijini watu walikuwa wanaamka kwa kutumia majogoo na mchana sehemu zenye makanisa walikuwa wanajua saa kwa kutumia kengele za kanisani.
Na ndiye aliyeleta mtihani wa form two. Tulikuwa tunauita MAKWETAMuwe na adabu sasa. Watu tumesoma WAZIRI WA ELIMU AKIWA JACKSOM MAKWETA.
Tufafanulie sisi vijana wa sasa
umenikumbusha kawimbo fulani hiviKuna Bus Ziliitwa Luxuary zilikuwa zikienda Pugu Kariakoo. Toyota Coaster kidungu mbele.View attachment 1634740
Namshangaa mwambie atupishe huu uzi sio wake ila nisimkatishe tamaa hiki chumba kimejaa angalie vyumba vya 1995 hadi sasa.Ila kila mtu na zamani yake hata nzi anaishi mwezi mmoja wiki jana anaona ni miaka mingiSasa clouds fm si redio ya juzi tu
Nakumbuka enzi hizo ilikuwa kawaida kabisa kusibiria kipindi cha muziki mida ya usiku huku ukiwa na kaseti yako, unasuburia wimbo unaoupenda ukifika unaurekodi, Tulikuwa tunasubiria usiku kwa sababu mchana Dj alikiwa anaongea akijisikia wakati mziki unacheza na wimbo anaweza kuukata mapema,
Enzi hizo hakukuwa na chanzo cha taarifa cha haraka kukujibia maswali, mfano unaweza kunywa coca cola ila ukitaka kujua nani alie itengeneza ilikuwa ni shughuli pevu kweli kweli, siku hizi ni mwendo wa google, wikipedia, n.k
Kuwasiliana kwa njia ya barua na watu wa mbali, Nakumbuka barua zikifika kama ni ya mpenzi wako ilikuwa unaoga kabisa na kula kabisa kabla hujaisoma, sikwambie mtu, watu walijua kuongea kupitia maandishi.
Kulikuwa na vijiwe vya kupeana habari na kukutana na washkaji, ukibaki nyumbani utaboreka sana kwanza inakubidi tu utoke nje maana wenzako wote wapo nje, hakukuwa na kubaki ndani unachati, upo instagram, netflix, n.k