Je ni lini Tanzania itaweza kurusha satellite angani?

Mataifa mengi hususani Africa yameanza kwa kasi urushaji wa Satellite angani katika karne hii kwa kurusha wenyewe au kushirikiana na mataifa kama Japan, Russia, Marekani n.k. Dunia ya sasa matumizi ya satellite ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi husika asa kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Matumzi ya satellite yanasaidia kuchukua taarifa za Duniani kwenye maswala ya uboreshaji wa kilimo, kijeshi, uchaguzi, afya, hali ya hewa na pia kupata taarifa kwa haraka zinazohusu vimbunga na matetemeko ili mamlaka zilizopo nchi hizo kutoa tahadhari za majanga kabla ya kutokea au serikali kujipanga kwa ajili ya kuchukua tahadhari.

Nchi za Africa ambazo zimeweza kurusha Satelite angani na matumizi yake ni kama ifuatavyo;_


· Misri

Misri wana satellite kama EgyptSat 1 na EgyptSat 2 ambazo wanazitumia kwa matumizi mbalimbali kwa ajili ya kuleta tija kwenye shughuli zao za uchumi. Mwaka huu 2017 wanapanga kurusha Satelite ya DesertSat kwa ajili ya ulinzi na usiamimizi wa maliasili zao ambazo zipo maeneo ya jangwani ili ziweze kuleta tija katika nchi yao.



· Africa Kusini

Afrika kusini wana satellite nyingi ambazo wamerusha toka mwaka 1999-2015. Sateliete ya Kondor-E waliirusha mwaka 2015 huwa wanaitumia kwa ajili ya matumizi ya kijeshi na Satelite nyingne nyingi kama SUNSAT, SumbandilaSat kwa ajili ya matumizi mbalimbali yanayoleta tija kwenye taifa lao n.k


· Morocco

Morocco pia wana satellite mbalimbali pia ifikapo Novemba 2017 watarusha satellite yao nyingine ambayo itatumika kwa shughuli za kijamii na kijeshi ambapo wametumia takribani Euro 500 Million kutaka kufanikisha hilo .


· Algeria

Algeria nao walianza tafiti na hatua za urushaji wa satellite toka miaka ya 2002. Algeria wana satellite zao kama Alsat-1B ambayo inatuamika kwa ajili ya uchukuaji taarifa katika maswala ya kilimo na taarifa za majanga kama vimbunga na matetemeko.

Alsat-2A wanaitumia kwa ajili ya upigaji picha za anga ambazo zinazotumika kwenye taasisi zao kama za kilimo, upimaji ardhi na mamlaka ya hali ya hewa.


· Nijeria

Wanaijeria wanazitumia sana Satellite zao kama SatX na Sat 2 ambazo zipo angani kwa ajili ya kufanya uangalizi wa vyazo vya mafuta kule Niger Delta, chaguzi mbalimbali kwa ajili ya ubainishaji wapiga kura na shughuri za kiusalama na kijeshi wakati wa kutafuta maficho ya Boko Haram pamoja na utafutaji wa watoto 273 waliotekwa kule Chibok mwaka 2014 zilitumika sana.



· Ghana

Mwaka huu 2017 Ghana wamerusha ya kwao inaitwa GhanaSat-1, ni satellite ndogo kabisa na ni satellite ya kwanza kurushwa nchini Ghana wakishirikiana na Mamalaka ya anga ya Japani JAXA (Japanese Aerospace Exploration Agency) imewaghalimu takribani Dola 50,000/=, wanaitumia kwa ajili ya upigaji wa picha za anga nchini Ghana.

MASWALI YANGU

Je Tanzania ina mikakati gani kuhusu au wazo la kurusha satellite angani kwa ajili ya matumizi kijamii na kiuchumi ili kuliletea tija Taifa letu ?

Je maproffesa wetu wanajipanga vipi kufanikisha hili?

Je Serikali inaweza kuweka bajeti ya kusomesha wadogo zetu kwenye Sayansi ya anga ili kuleta tija ya kufanikisha ndoto yetu ya kurusha hata satellite moja ndogo kama waliorusha wenzetu wa Ghana mwaka huu 2017 yenye Launch mass ya 1 Kilogramu(Kg)?

Je kuna fungu lolote huwa linatengwa kwa ajili ya tafiti za sayansi asa za anga ?


Klementos- Jamii Forum
Je,hizo satellite walirusha wenyewe au waliwalipa space agencies wawarushie?.Maana najua project za kurusha satelite wenyewe ni gharama kweli kweli.Maana kuunda yale ma space rockets ya kubebea satellite sio mchezo.Ni mapesa mengi sana yanahitajika.
 
Mataifa mengi hususani Africa yameanza kwa kasi urushaji wa Satellite angani katika karne hii kwa kurusha wenyewe au kushirikiana na mataifa kama Japan, Russia, Marekani n.k. Dunia ya sasa matumizi ya satellite ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi husika asa kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Matumzi ya satellite yanasaidia kuchukua taarifa za Duniani kwenye maswala ya uboreshaji wa kilimo, kijeshi, uchaguzi, afya, hali ya hewa na pia kupata taarifa kwa haraka zinazohusu vimbunga na matetemeko ili mamlaka zilizopo nchi hizo kutoa tahadhari za majanga kabla ya kutokea au serikali kujipanga kwa ajili ya kuchukua tahadhari.

Nchi za Africa ambazo zimeweza kurusha Satelite angani na matumizi yake ni kama ifuatavyo;_


· Misri

Misri wana satellite kama EgyptSat 1 na EgyptSat 2 ambazo wanazitumia kwa matumizi mbalimbali kwa ajili ya kuleta tija kwenye shughuli zao za uchumi. Mwaka huu 2017 wanapanga kurusha Satelite ya DesertSat kwa ajili ya ulinzi na usiamimizi wa maliasili zao ambazo zipo maeneo ya jangwani ili ziweze kuleta tija katika nchi yao.



· Africa Kusini

Afrika kusini wana satellite nyingi ambazo wamerusha toka mwaka 1999-2015. Sateliete ya Kondor-E waliirusha mwaka 2015 huwa wanaitumia kwa ajili ya matumizi ya kijeshi na Satelite nyingne nyingi kama SUNSAT, SumbandilaSat kwa ajili ya matumizi mbalimbali yanayoleta tija kwenye taifa lao n.k


· Morocco

Morocco pia wana satellite mbalimbali pia ifikapo Novemba 2017 watarusha satellite yao nyingine ambayo itatumika kwa shughuli za kijamii na kijeshi ambapo wametumia takribani Euro 500 Million kutaka kufanikisha hilo .


· Algeria

Algeria nao walianza tafiti na hatua za urushaji wa satellite toka miaka ya 2002. Algeria wana satellite zao kama Alsat-1B ambayo inatuamika kwa ajili ya uchukuaji taarifa katika maswala ya kilimo na taarifa za majanga kama vimbunga na matetemeko.

Alsat-2A wanaitumia kwa ajili ya upigaji picha za anga ambazo zinazotumika kwenye taasisi zao kama za kilimo, upimaji ardhi na mamlaka ya hali ya hewa.


· Nijeria

Wanaijeria wanazitumia sana Satellite zao kama SatX na Sat 2 ambazo zipo angani kwa ajili ya kufanya uangalizi wa vyazo vya mafuta kule Niger Delta, chaguzi mbalimbali kwa ajili ya ubainishaji wapiga kura na shughuri za kiusalama na kijeshi wakati wa kutafuta maficho ya Boko Haram pamoja na utafutaji wa watoto 273 waliotekwa kule Chibok mwaka 2014 zilitumika sana.



· Ghana

Mwaka huu 2017 Ghana wamerusha ya kwao inaitwa GhanaSat-1, ni satellite ndogo kabisa na ni satellite ya kwanza kurushwa nchini Ghana wakishirikiana na Mamalaka ya anga ya Japani JAXA (Japanese Aerospace Exploration Agency) imewaghalimu takribani Dola 50,000/=, wanaitumia kwa ajili ya upigaji wa picha za anga nchini Ghana.

MASWALI YANGU

Je Tanzania ina mikakati gani kuhusu au wazo la kurusha satellite angani kwa ajili ya matumizi kijamii na kiuchumi ili kuliletea tija Taifa letu ?

Je maproffesa wetu wanajipanga vipi kufanikisha hili?

Je Serikali inaweza kuweka bajeti ya kusomesha wadogo zetu kwenye Sayansi ya anga ili kuleta tija ya kufanikisha ndoto yetu ya kurusha hata satellite moja ndogo kama waliorusha wenzetu wa Ghana mwaka huu 2017 yenye Launch mass ya 1 Kilogramu(Kg)?

Je kuna fungu lolote huwa linatengwa kwa ajili ya tafiti za sayansi asa za anga ?


Klementos- Jamii Forum
Profesa wa Tanzania ni wa kisiasa zaidi, wangekua wasomi hasa wangehama nchi
 
Je,hizo satellite walirusha wenyewe au waliwalipa space agencies wawarushie?.Maana najua project za kurusha satelite wenyewe ni gharama kweli kweli.Maana kuunda yale ma space rockets ya kubebea satellite sio mchezo.Ni mapesa mengi sana yanahitajika.
Ni kweli kiongozi kurusha satellite ni gharama kubwa sana, hizo nchi asilimia kubwa wameshirikiana na mamalaka za anga za mataifa kama Japan, Russia, Marekani n.k. Basi tujaribu hata kama Ghana kwa bajeti ya Dola 50,000 ni msaada mkubwa kwa taifa letu.
 
Hii ni picha tosha kuwa wenzetu wana bajeti za kufanya tafiti na pia wana sponsor wananchi wao kwenda kusoma maswala ya anga kwa ajili ya kuliletea tija taifa lao.Nadhani huu ndio wakati wetu kuanza, tunaweza anza hata na mitaala kwenye vyuo vyetu kozi hizi za maswala ya anga.

Hizi ni mamlaka za maswala ya anga kwa nchi za Africa.
  • Africa kusini -The South African National Space Agency (SANSA)
  • Misri -National Authority for Remote Sensing and Space Science
  • Nigeria- National Space Research and Development Agency
  • Algeria -Algerian Space Agency
  • Tunisia -National Remote Sensing Center of Tunisia
  • Morroco- Royal Centre for Remote Sensing
 
Ni kweli kiongozi kurusha satellite ni gharama kubwa sana, hizo nchi asilimia kubwa wameshirikiana na mamalaka za anga za mataifa kama Japan, Russia, Marekani n.k. Basi tujaribu hata kama Ghana kwa bajeti ya Dola 50,000 ni msaada mkubwa kwa taifa letu.
Ni kweli mkuu,hasa communication satellite itaturahisishia sana.
 
Tutatumia hizohizo za wenzetu, kwanza huko juu yatakuwa mengi mno yatazuia mvua na yatasababisha joto na mawingu kukimbia. Hao waliorusha yanatosha. Siye hamna haja.
Mmeshindwa kuweka taa za barabarani kuongoza magari mtaweza kurusha satellite???
Kutwa matrafik wana zungusha mikono njiapanda.
 
Hata ikirushwa mtasema mbovu nati zimelegea..
wabongo mna jema...., mtauliza hata hizo pesa alikozitoa Mkuu mpaka akapata za kurusha satellite
 
Unazungumzia Tanzania hiii hiiii au
Ni Tanzania hii hii mkuu, hao walioendelea kuna mahali walianzia na sisi ndiyo tumeshaanza hatua ya kwanza, badala ya kuwa negative, hebu tuunganishe mawazo, nguvu na rasilimali kwa pamoja na tusema sasa yatosha! hatutaki kununua, kuuza na kutumia (kwa mfano) Smart phone toka ughaibuni, tunataka kutengeneza zetu wenyewe na sisi ndiyo tuwauzie majirani zetu. ili kuwezesha hili kumeanzishwa klabu maalum kwa ajiri ya kuwaunganisha watanzania wa kada mbalilmbali ili waweze kushiriki kwa kutoa maoni ya kuboresha au hata kufanya kile ambachi wanadhani kitaipeleka tanzania kwenye level ya juu kabisa ya teknolojia. kwa habari zaidi tembelea hapa
ESTA -TANZANITE CITY OF TECHNOLOGY & INNOVATION: MBEYA: FRIENDS CLUB OF THE TANZANITE CITY
 
Back
Top Bottom