GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,874
Kuna sababu ambazo nimepewa hadi Mtu kuwa Mkimbiza Mwenge Kitaifa nchini Tanzania ( ambazo baadhi yake si za Kimaadili kabisa ) japo bado naendelea Kuzithibitisha taratibu ila kwa leo naomba tu kujua je, ni lazima ukiwa Mkimbiza Mwenge Mkuu uwe unatoka tu Chama cha Mapinduzi? Kama Jibu ni ndiyo je, Tunu ya Taifa inaweza ikawabagua Watu wa Chama fulani na kuwapendelea wa Chama fulani tu? na je, ni lazima muda wa Kukimbiza Mwenge ukimalizika huyo Mkimbiza Mwenge ateuliwe na Rais kushika Nyadhifa Serikalini?
Mkimaliza Kunipa Majibu yenu nawapeni tena Swali hili la nyongeza kwamba ni kwanini Wakimbiza Mwenge huwa wanaogopwa kuliko na kuanzia Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri na hadi kwa Mawaziri? Kuna Waziri Mmoja hivi ana ' PhD ' yake nimebahatika kumuona kupitia TBC1 akiwa na Mwenge huko Jimboni Kwake na nilichobahatika Kukiona kwa haraka haraka ni jinsi yule Mkimbiza Mwenge Mkuu akiwa anamdharau huyu Waziri ( mwenye dhamana ya Wizara ambayo inapendwa mno na wana Simba na Yanga ) na Waziri kuonekana akiwa anatetemeka, anajibalaguza na anamnyenyekea mno huyo Mkimbiza Mwenge Mkuu.
Nitashukuru nikielimishwa juu ya hili na karibuni sana Wandugu.
Mkimaliza Kunipa Majibu yenu nawapeni tena Swali hili la nyongeza kwamba ni kwanini Wakimbiza Mwenge huwa wanaogopwa kuliko na kuanzia Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri na hadi kwa Mawaziri? Kuna Waziri Mmoja hivi ana ' PhD ' yake nimebahatika kumuona kupitia TBC1 akiwa na Mwenge huko Jimboni Kwake na nilichobahatika Kukiona kwa haraka haraka ni jinsi yule Mkimbiza Mwenge Mkuu akiwa anamdharau huyu Waziri ( mwenye dhamana ya Wizara ambayo inapendwa mno na wana Simba na Yanga ) na Waziri kuonekana akiwa anatetemeka, anajibalaguza na anamnyenyekea mno huyo Mkimbiza Mwenge Mkuu.
Nitashukuru nikielimishwa juu ya hili na karibuni sana Wandugu.