Je, ni kweli watu weusi tuna akili ndogo?

Kwa maana hiyo basi hatuna universally accepted definition ya "mtu mweusi" na badala yake kila mtu ana definition yake kulingana na muono binafsi.

Lakini mkanganyiko huu wa kutokuwepo kwa tafsiri sahihi ya mtu mweusi uko kwa watu waliochanganya race pekee(biracial people) na wala sio kwa mtu asiyechanganya race kama mimi hivi au wewe.

Kwa hiyo kumbe mimi au wewe ni mfano sahihi wa mtu mweusi.

Tukisema twende ndani zaidi kwa minajili ya kibailojia basi tutarudi kule kule kwenye mkanganyiko mfano ni hapo kwa huyo mwana mama Sigrid Johnson.

Sent using Jamii Forums mobile app
Suala zima la race si ndilo hilo hilo la weusi na weupe?

Na lenyewe ni la utunzi wa watu.

Kuna watu wengi sana wa pwani, wanajiita weusi, tunawaona weusi, lakini ukiwapima ki DNA wana viasili vingi tu vinavyohusishwa na waarabu.

Watu wamechanganyikana, wamechanganyikana sana, wamechanganyikana sana kwa maelfu na maelfu ya miaka kiasi kwamba kwa sasa tunajiwekea hadithi tu za "mtu mweusi".

Katika hao wanaoitwa weusi wenyewe kuna jamii kibao tofauti, Hottentonts, Nilotic, Bantu etc.

Haya mambo ukiyafuatilia kwa undani, utaona dhana nzima ya "watu weusi" inakuwa simplified kuliko facts zilivyo. Ni dhana ya kisiasa na kisosholojia zaidi ya kibaiolojia.
 
Dini/ imani uliyokuwa nayo awali, bado haielezi ni Dini au imani ipi hiyo ambayo kwayo ni tofauti na ya weupe.

Hiyo (dini au imani) yako (weusi) ilifanyikaje au ilitekelezwaje na hii ya weupe inatekelezwaje.

Aidha, kwa upande wa traditional belief ni zipi zinaweza kubainishwa kama ni za weusi (Afrika) na weupe hawakuwa nazo.

Hailezei kivipi wakati hapo tu tayari nimeileza japo ni kwa ufupi sana.?

Kwamba ilifanyika vipi, hapo nitakujibu ilifanyika kimila na desturi za kikwetu tena kimatambiko zaidi.

Traditional beliefs za muafrika ambazo mzungu hakuwa nazo zipo nyingi tu moja wapo ni kumteua kiongozi/mwinyi/chief kwa kuangalia superficial power aliyonayo kama vile kuleta mvua hasa nyakati za njaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye hii hoja yako.

Unaweza kusema kwa uchache kabla ya ukoloni kipi tulichokuwa nacho, kwa hicho tunaweza kusema wakoloni hawakutusaidia chochote?
Wakoloni wametusaidia sana ila baada ya kujitambua tulitakiwa kusimama wenyewe kwa misingi yetu binafsi.
 
Suala zima la race si ndilo hilo hilo la weusi na weupe?

Na lenyewe ni la utunzi wa watu.

Kuna watu wengi sana wa pwani, wanajiita weusi, tunawaona weusi, lakini ukiwapima ki DNA wana viasili vingi tu vinavyohusishwa na waarabu.

Watu wamechanganyikana, wamechanganyikana sana, wamechanganyikana sana kwa maelfu na maelfu ya miaka kiasi kwamba kwa sasa tunajiwekea hadithi tu za "mtu mweusi".

Katika hao wanaoitwa weusi wenyewe kuna jamii kibao tofauti, Hottentonts, Nilotic, Bantu etc.

Haya mambo ukiyafuatilia kwa undani, utaona dhana nzima ya "watu weusi" inakuwa simplified kuliko facts zilivyo. Ni dhana ya kisiasa na kisosholojia zaidi ya kibaiolojia.

Kwa mantiki hii kumbe basi trans-generational inherent traits cause inavunja kabisa hii dhana nzima ya mtu mweusi, mana hata ukisoma ethnography itaturudisha kule kule tu kwenye tafsiri za kisiasa.

Sasa basi kumtambua huyu mtu ni mweusi au mweupe kinachofanyika ni assumptions tu ambazo msingi wake uko kwenye skin pigmentation ya mtu huyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamba ilifanyika vipi, hapo nitakujibu ilifanyika kimila na desturi za kikwetu tena kimatambiko zaidi.
Sio sahihi kufikiri kwamba "mila" ni jambo la jamii ya Waafrika.

Ukiwa makini ukayatazama mambo haya utaona ni "universal" ya watu wote na popote.

Tambiko kwa mfano, ambayo Waafrika wengi wanayashikilia kwamba ni yao ukitafiti mapokeo, acha matambiko haya ya nyakati zetu ni udanganyifu mkubwa, huoni yakitofautiana na Kanisa Katoliki linavyofanya.

Ukisoma historia kwa mfano, utaona kwamba dini/imani hii ambayo Waafrika tunaikataa na kusema ni ya wazungu imeanzia eneo linalofahamika hii leo kama Mashariki ya kati.

Eneo hili la Mashariki ya kati kama lilivyo mbali na eneo linalofahamika hii leo kama Afrika ni mbali pia na eneo linalofahamika hii leo kama Ulaya.

Hii yote haijakuwezesha kutambua kipi ni kipi.
 
Umeandika vizuri sana.

Tatizo ni "utambuzi".

Utambuzi ni nguvu ya akili. Bila utambuzi akili inapungukiwa.

Inawezekana kabisa " utambuzi" hatuna. Hii inatosha kuelezea tulivyo.
Angalia ma professor wetu wamekosa utambuzi ila wana elimu kubwa isiyo na msaada kwa jamii na tatizo ni misingi inayotukuza kielimu haishabihiani na mazingira yetu halisi wengi huishia kuwa kama vituko na vichekesho katika jamii.
Bila kujitambua hatuwezi kuendelea
 
Angalia ma professor wetu wamekosa utambuzi ila wana elimu kubwa isiyo na msaada kwa jamii na tatizo ni misingi inayotukuza kielimu haishabihiani na mazingira yetu halisi wengi huishia kuwa kama vituko na vichekesho katika jamii.
Bila kujitambua hatuwezi kuendelea
Kuwanyoshea vidole watu fulani kwa sababu ya nafasi zao kijamii au kitaaluma hakuna uhalali kisayansi, kisaikolojia na kidini au kimaadili.

Watu hawa kama ulivyo wewe wanatoka kwenye jamii.

Ingawa tunataraji kwa sababu ya elimu walionayo wangetenda vema.

Lakini inawezekanaje kwa mtu ambaye akili na mwili wake vimeachana akatenda kwa manufaa?

Watu wengi tuna majeraha ya akili hivi kwamba mwili pekee ndio unaonekana kufanya kazi. Lakini akili, ambayo ndio manufaa yenyewe, na kazi yenyewe haiko na mwili.

Waafrika wengi mwili u peke yake na akili i peke yake.

Tazama watu wa kawaida kabisa, wasomi, na wenye nafasi za mamlaka utaona malengo ya mwili mengine na malengo ya akili mengine.

Waafrika wengi Akili na mwili haviko pamoja. Mtu yoyote akiwa katika hali ya namna hii haiwezekani, kwa kweli haiwezekani mtu huyo au jamii hiyo kupata maendeleo.

Watu wanaopata maendeleo au wanaogundua vitu au mambo ni wale ambao Akili na mwili viko pamoja.

Fikiri kwa mfano, mtoto anaanza darasa la kwanza mpaka darasa la saba hajui kusoma na kuandika. Huyu unaweza kusema Akili na Mwili viko pamoja?

Mfano mwingine, mtu anaye oa mke, badae akaoa mke mwingine; au mke aliye na mume, lakini ana uhusiano wa kingono na mume mwingine, au mume mwenye mke, lakini ana uhusiano wa kingono na mke mwingine, huyu akili na mwili haviko pamoja.

Mtu asiye weza tambua "Niko Wapi", "Nasikia Nini", huyu, Mwili na Akili yake haviko pamoja.
 
Tatizo sio akili, tatizo ni kitu gani kinaingia kwenye akili ya mtu. Tatizo ni mifumo yetu ya elimu.
 
Kwa mantiki hii kumbe basi trans-generational inherent traits cause inavunja kabisa hii dhana nzima ya mtu mweusi, mana hata ukisoma ethnography itaturudisha kule kule tu kwenye tafsiri za kisiasa.

Sasa basi kumtambua huyu mtu ni mweusi au mweupe kinachofanyika ni assumptions tu ambazo msingi wake uko kwenye skin pigmentation ya mtu huyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
The whole thing is a superficial, arbitrary, skin deep social construct.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
James Watson,mwanasayansi maarufu duniani na mshindi wa nishani ya noble katika tiba mwaka 1962, ameleta mjadala mkubwa kwa madai kwamba inaelekea mtu mweusi ana akili ndogo kuliko mtu mweupe. Kauli hiyo imeshikiliwa bango na wapinzani wa ubaguzi wa rangi kwa madai kwamba inamdhalilisha mtu mweusi.

Hata hivyo Watson si mtu wa kwanza kusema hivyo isipokuwa yeye kaisema kisayansi zaidi. Siku za nyuma Waziri Mkuu mmoja wa Japan alipata kusema maneno kama hayo kwamba anatilia mashaka uwezo wa mtu mweusi. Waziri mwingine pia alishanukuliwa anasema hivyo. Wote baadaye waliomba radhi ila ujumbe ulifika.

Chika Onyeani katika kitabu chake cha The Capitalist Nigger naye anashangaa ni kwanini Mwafrika atukanwe namna hiyo na mawaziri wa Japan, lakini bado waendelee kununua bidhaa kutoka japan. Pia anasema jamii nyingi za watu Weusi zinafanana kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano ukikutana na Muamerika mweusi aliyezaliwa marekani au carribean au afrika kwenyewe bado wanatabia zilezile ambazo zinatia shaka kama kweli akili za mtu mweusi si ndogo kwa kiasi fulani.

Ukianza kuangalia matokeo mbalimbali yaliyotokea Afrika enzi za miaka ya nyuma utaanza kuwa na wasiwasi kuhusu hali ya uelewa wa mtu mweusi.Historia inaonyesha kwamba ,hadi karne ya 16 kiwango cha maendeleo kati ya nchi za Afrika na ulaya kilikuwa sawa

Tunaambiwa pia kwamba miaka ya 1960 baadhi ya nchi za Afrika zilikuwa zimeendelea kimaendeleo au sawa na nchi za Asia ambazo leo ziko mbali kimaendeleo.Bado unajiuliza ni wapi kwenye matatizo? Kwanini waafrika tuachwe kila leo?

Ripoti za umaskini duniani zinaonesha kwamba umaskini umepungua kwa kiasi kikubwa lakini kwa Afrika unaonyesha kuongezeka.Mbaya zaidi maskini wa Afrika wapo kwenye dimbwi zito ambalo si rahisi kujinasua.Utafiti huu unafanywa kulinganisha na nchi za India na China ambazo zina idadi kubwa sana ya watu

Ukipima baadhi ya kauli za hawa tunaowaita wabaguzi utagundua kuna ujumbe wanawasilisha.Ukichukua Tanzania kama mwakilishi wa Afrika utaweza kugundua haya.Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi lakini si nufaishi kwa mwananchi wake isipokuwa wawekezaji wanakuwa na mamlaka makubwa juu ya rasilimali hizi.Kuna mito,Madini na misimu lakini bado tunaagizia dawa kutoka nje.SHAME!!

Watu wanajilundikia mabilioni ya Fedha kwenye akaunti zao za benki zilizopo nchini au hata nje ulaya wakati shule ya AZANIA iliyoko katikati ya jiji kuu la nchi ina wastani wa tundu moja la choo kwa wanafunzi 300

Bado tunazipa likizo ya kodi kampuni kubwa huku tukifuatilia vikodi vidogo vidogo.Kampuni kubwa zinaruhusiwa kubeba hasara na kuipeleka kwenye mahesabu ya mwaka ujao kwa miaka KADHAA lakini hiyo hiyo kampuni inaendelea kufanya biashara.Hapa sisi ni wakusanyaji wazuri wa kodi au wakwepaji wazuri wa makampuni makubwa?

Inafaa tujiulize kunani kwenye akili zetu?Tunasema tuna mafuta lakini tukitaka kuyachimba tunamwita mzungu japokuwa tumekuwa tukizalisha wakandarasi na wanajiorojia kila mwaka.Lazima tujiulize kama elimu yetu ina mushikeli au la!Sasa hivi tunajigamba kuwa na vyuo vikuu 30 lakini bado tunaagizia vijiti vya kuchokonolea meno toka Malaysia. Kweli??

Kabla ya kushika mabango na kuwalaani wabaguzi wa rangi lazima tujiulize kwanza ni wapi tumekosea na sababu za kukwama kwetu.Tusikimbilie kulaumu wazungu kwa kuleta ukoloni na ukoloni mambo leo.Malaysia na Ghana zote zilikuwa koloni za muingereza na zilipata uhuru mwaka 1957 kwa pamoja lakini leo hali ni tofauti.

Wamalaysia walikuwa wanakwenda Ghana kujifunza kilimo cha mawese. Leo hii Ghana wanajifunza kila kitu toka Malaysia kikiwemo kilimo cha mawese.Wazungu wanaopinga kauli za WATSON sio kwamba wanasikitika sana bali wanaonesha kukasirika usoni lakini moyoni wanasema ni kweli hawa wanaujinga wao mkubwa.Wanatutetea ili waendelee kutuvuna.Hawataki tukaechini na kujitathmini tulipoenda mrama.

Nachukia kuitwa kiumbe dhaifu hasa kiakili.Nachukia kwa sababu naupenda uafrika na WEUSI wangu.Nawapenda waafrika wenzangu.Nachukia wanapoambiwa kwamba wanaubongo dhaifu. Lakini nahisi kuna mahali kama watu WEUSI tumekosea

Kama mtu anaiba mabilioni ya fedha za umma kwenye nchi maskini na kuyaweka ulaya au kewekeza mahali popote,huku kukiwa na wananchi wanakufa kwa kukosa madawa hospitalini basi kuna ulazima wa kujiuliza tuliko na kasoro.Kama viongozi wanawaibia wananchi wao waliowachagua kuwawakilisha bila aibu yoyote inabidi tuhoji akili zetu.Kama wananchi wanaridhika na hila za viongozi wao bila ya kuchukua hatua madhubuti basi tuhoji akili zetu

JE? Watson aombe radhi

Hata kama Watson ataomba radhi kama mawaziri wa Japan atakuwa amepeleka ujumbe mzito kwa watu WEUSI kujichunguza.Huu ni ujumbe mzito kwa taifa letu la Tanzania.Mimi ni miongoni mwa wasioamini upuuzi wa James Watson, kwamba waafrika tuna akili ndogo.

Historia inaonyesha kwamba chuo kikuu cha kwanza duniani kilikuwa Afrika,kule Mali.Uvumbuzi wa hisabati ulitoka Afrika,hata mtu wa kwanza duniani anaaminika kuishi Afrika.Pia MAAJABU mengi yapo kule misri (pyramids)

Wapo waliokwenda mbali na kusema kwamba hata YESU KRISTO alikuwa mtu mweusi wa misri na kwamba ndiyo sababu SIMON WA KRENE,ambaye alikuwa mtu mweusi alimsaidia YESU kubeba msalaba.Ilikuwa ni huruma ya kuona mtu mweusi mwezake anateswa.

Jamani ni wapi tumekosea??

Sasa je,ni kweli watu WEUSI tuna akili ndogo??View attachment 1314061

Sent using Jamii Forums mobile app
pale tu unapoacha KUJIAMINI na KUJITAMBUA unakuwa hauna akili kabisa, hakuna cha akili ndogo wala kubwa, na hili halina mchina mzungu mwarabu au makonde
 
So realistically i'm neither black nor white and no one can tell me otherwise.

Thank you kiranga.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nobody is black or white.

I have never seen a black or a white person in my life.

Black being HTML code #000000 and White being HTML code #111111


 
Kuwanyoshea vidole watu fulani kwa sababu ya nafasi zao kijamii au kitaaluma hakuna uhalali kisayansi, kisaikolojia na kidini au kimaadili.

Watu hawa kama ulivyo wewe wanatoka kwenye jamii.

Ingawa tunataraji kwa sababu ya elimu walionayo wangetenda vema.

Lakini inawezekanaje kwa mtu ambaye akili na mwili wake vimeachana akatenda kwa manufaa?

Watu wengi tuna majeraha ya akili hivi kwamba mwili pekee ndio unaonekana kufanya kazi. Lakini akili, ambayo ndio manufaa yenyewe, na kazi yenyewe haiko na mwili.

Waafrika wengi mwili u peke yake na akili i peke yake.

Tazama watu wa kawaida kabisa, wasomi, na wenye nafasi za mamlaka utaona malengo ya mwili mengine na malengo ya akili mengine.

Waafrika wengi Akili na mwili haviko pamoja. Mtu yoyote akiwa katika hali ya namna hii haiwezekani, kwa kweli haiwezekani mtu huyo au jamii hiyo kupata maendeleo.

Watu wanaopata maendeleo au wanaogundua vitu au mambo ni wale ambao Akili na mwili viko pamoja.

Fikiri kwa mfano, mtoto anaanza darasa la kwanza mpaka darasa la saba hajui kusoma na kuandika. Huyu unaweza kusema Akili na Mwili viko pamoja?

Mfano mwingine, mtu anaye oa mke, badae akaoa mke mwingine; au mke aliye na mume, lakini ana uhusiano wa kingono na mume mwingine, au mume mwenye mke, lakini ana uhusiano wa kingono na mke mwingine, huyu akili na mwili haviko pamoja.

Mtu asiye weza tambua "Niko Wapi", "Nasikia Nini", huyu, Mwili na Akili yake haviko pamoja.
Binafsi nawalaumu hawa wasomi wa kada za profesa na dokta kwa sababu wao kwa namna kubwa hushiriki katika maamuzi mengi ya mitaala ya ufundishaji na Marengo ya maendeleo ya kisayansi na kiuchumi lakini huishia kutengeneza sera mbovu zisizo kuwa na tija.
Elimu yetu haina tija tuna sera mbovu ya elimu isiyo leta tija kwa jamii.

Mwili na akili haviwezi kufanya kazi pamoja kama mtu hajitambui nina bahati nzuri au mbaya kutembelea inchi nyingi za Afrika inauma mno haiwezekani mataifa yenye lasirimali nyingi madini, misitu,ardhi yenye rutuba, mito, bahari, maziwa na mabwawa yanakuwa na umasikini uliotopea.
Bila elimu yenye tija kwa maendeleo ya watu na jamii hatuwezi kupiga hatua hata moja.
Bila elimu ya kufanya kwa vitendo na kukifanya kizazi cha wa Afrika kujitambua na kujikwamua kwa juhudi binafsi hatuwezi kuendelea asilani.

Afrika isipojitambua viongozi kuwa na sera madhubuti kwa maendeleo ya uchumi wa watu na vitu hatuwezi kupiga hatua.

Mfano Tanzania viongozi wetu wanadhani maendeleo ni vitu bila watu jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa uchumi kwa taifa letu.
 
Tuangalie kwa makini ! Chukua kipengele kidogo cha "mda" katika brain ya mwafrika kale kasehemu kanakohusika na mda huenda Mungu aliongeza maji kidogo kwa mwafrika . Hatuendi na mda ! Tuangalie mambo makubwa ! Formula za kisayansi mwafrika ameshirikije ?

Sent using Jamii Forums mobile app
afrika wanashiriki sana,mfano IBM kuna mkono was mtu mweusi katika uvumbuzi wake,Ila ni wachache katika hayo mambo wengi hawataki hard sayansi wanakimbilia art na michezo ndio maana wamarekani weusi wanadominate sports ,mabondia wakubwa duniani ni weusi,wacheza kikapu wakubwa in weusi hata wachezaji wa mpira in weusi kutoka brazili na Afrika.Tunatakiwa tubadili mtazamo.Brain drain inaua Afrika,wazungu wanatoa scholarship waafrika wanadhani ni zali la mentalii kumbe ni mpngo wa wazungu Ku drain geneus kutoka Afrika na Asia,wachina wamestuka wanasayansi wao wakubwa wanarudi china ndio maana America inaweweseka, nasi wasomi wetu wakiamua kurudi Afrika itabadirika kqa kasi nasikia teknolojia ya gari LA umeme Tesla mweusi ndio aliefanya mapinduzi ntatafiti ukweli huu.Interior design was Benz ni mweusi, na kuna mnaijeria moja nae ni bingwa wa interior design.Vilevile kuna mnaijeria alizaini injini za kisasa za Honda yupo you tube.Wasomi wspo wengi sana huko ulaya na America Ila wazungu amewateka akili,wanawaoza au kuolewa na wazungu wasahau kwao na kutumia DNA ya bright people from Afrika kuendeleza kizazi chao.
 
Back
Top Bottom