Je ni kweli wanawake wa tanzania wapo tayari kupewa?

Mambo vipi wadau?

nimesikiliza hotuba ya mgombea wa c.c.m kiti cha uraisi huko kirumba mwanza leo.................katika hotuba yake amesema amejitahidi kutoa nafasi mbalimbali za maamuzi kwa wanawake wengi kuliko kiongozi yeyote aliyepita...akatoa mifano kama vile mahakimu,mawaziri,manaibu waziri,majaji,wakuu wa wilaya na mikoa.....................
akaongeza kwamba hawa wanafanya vizuri kuliko wanaume....kwani ni waaminifu na baadhi ya wanaume ni wadokozi...............akaongeza kwamba wanawake hawa ni kidogo na wanastahili kupewa nafasi zaidi kuongezwa idadi........................

wadau tuondoe ushabiki wa kisiasa...tijadili ili kujenga nchi yetu...je ni kweli wanawake waliopo kwenye uongozi kwa sasa wanaweza???

kwa zile wilaya ambazo viongozi wa ngazi za juu ni wanawake kwa asilimia kubwa vipi kuna mafanikio?
kwa zile wizara ambazo waziri,naibu waziri au katibu mkuu ni mwanamke je ni kweli wanatosha?


Faithful,
Unaweza kuweka hiyo heading vizuri please; tujue, 'kupewa' nini; favor, vyeo, madaraka, au?
 
kwani hao wanawake aliwapa cheo kwa kuwa ni wamezaliwa wanawake tu au kwa kuwa wanaweza?

au anataka kutuambia aliwachagua lakini hakuwa na uhakika wa utendaji wao na wamem SUPRISE kuwa wanaweza!

ingelikuwa mimi ni mmoja wa majaji waliochaguliwa kisha mkuu wa nchi akawa suprised kuwa naweza ningelijiskia ovyo sana.

asirudie hii kitu!

Aache kabisa kwani inaonyesha hana hoja ya msingi kwa wa-tz.

Binafsi nilitegemea pale Mwanza aseme yafuatayo:
  • Alikusanya kodi kiasi gani toka jiji la Mwanza na,
  • Alizifanyia nini hizo fedha,
  • Je, kwenye matumizi ya fedha hizo zimebaki kiasi gani na ziko wapi?
Asifikiri wa-tz wanapenda ngonjera na mashairi yake. Tunajua kuwa maendeleo yanaletwa na kodi za wananchi na si-Chama fulani!!

Onyo kwetu wa-tz ni kuwa Uongozi mbovu unapochaguliwa shida hazichagui pa kwenda, uwe CUF, CCM, CHADEMA shida zitakukuta huko huko. Tafadhali tuache ushabiki ili JK, alijue hili na aanze sasa kutuambia atafanya nini miaka 5 ijayo na siyo hadithi za eti wanaume ni wadokozi. Hivi huo u-DR wake hiyo ndo reflection yake?
 
Hapa kifupi tu ni kwamba zinatafutwa kura za wanawake .......walio wachache waliopewa ulaji, ndo wameshakuwa chambo tena...
 
Mkuu inawezekana MS kakubwaga kwenye kura za maoni kila post hata iwe haihusiani unamtaja..anyway, mi nadhani JK kasema "wanaweza" nyinyi mnataka takwimu za "kwanini" ama "kwa vipi"wanaweza wakati nyinyi hamna hata hizo za kwanini hawawezi?
Mnajuwa nyie wasomi wa vitabuni msioweza kuvumbua hata sindano mnatabu kidogo, ndiyo mliotufikisha hapa tulipo, nchi masikini mnatuletea takwimu za kwenye makaratasi tu wakati ukitazama kwa macho tu unakuta njaa kali bado.

Mkuu anasema "wanaweza" mimi nakubalinana naye kuwa baadhi ya sekta wanawake wameweza sana tu, kama mahakama, nimewaona kwa macho yangu akina mama Mjasiri, Kimaro, Munuo etc wakifanya vizuri tu kuliko hata wanaume, wakuu wa mikoa na wilaya kama Hajjat Amina Said Mrisho, Christine Ishengoma, Betty Mkwasa wanaongoza vizuri tu kwa kadiri ya uwezo wao...kweli wanaweza wala haihitaji takwimu hiiiiizo kujuwa kuwa wanaweza, wakuu give the devil his due...tuweni wapinzani lakini penye ukweli tusemeni.

Sawa Bwana, hata Ishengoma? Na Chiku wa Temeke!!! haya bwana....lakini wapo wanawake wenye uwezo lakini hawapewi nafasi, wanaopewa ni wale !!!!!???? au
 
Wewe bana ustake ncheke..hivi una akili timamu kweli wewe?

Rais wako kipenzi chako Dr.Mkwere anasema wanawake wanaweza na wanaume ati ni wadokozi, sasa huoni hiyo statement ni self-defeating?? yeye yupo kundi gani? Kwanini basi asianze yeye kuachia ngazi pale magogoni?

Pili nimemtolea mfano Malaria Sugu, maana yeye ni kama buu , anakula chochote chenye lebo ya CCM bila kutafuna, pengine yupo kama wewe, ndio maana hamchekani.

BTW, sijaongelea hata takwimu, vita yangu mimi ni ya kimantiki zaidi sio matukio wala kauli fyongo za Dr.Mkwere which u find faultless..I bet hujui wala huelewi post unayoijibu. Typical STUPIDITY by choice.

Siezi hata kujadili hayo majina uliyoaweka, maana principally sikubaliani na kupeana vyeo kwene ofisi za umma kwa njia ya kuteuana. Mnateuana mpaka nafasi za ubunge, typical wabongo halafu mnaketi kitako kujadili kwanini hamuendelei.

Pheeew
Kwani sikaanza Kikwete tu! wengine waliopita walikuwa hawateui or kama walikuwa wanateua mbona ulikuwa husemi? JITU ZIMA HOVYO.
 
Natamani bongo tungekuwa na kitu kama factcheck.org maana hawa wanasiasa wanaweza wakaropoka tu bila kauli zao kuwa checked na mijitu ikaamini.

Kuna sehemu humu nimeona kuna mtu kaandika kuwa Kikwete katengeneza ajira milioni moja na ushee. Really? Kwenye sekta gani? Unemplyoment rate wakati anaingia madarakani ukilinganisha na sasa ni kiasi gani? Au hata ku track unemployment rate hatufanyi?

Na Prof. Jumanne Maghembe je? Joseph Mungai je? Sitta na Voda fasta je? Hapa tuongelee watu na si jinsi zao.
 
Mkuu inawezekana MS kakubwaga kwenye kura za maoni kila post hata iwe haihusiani unamtaja..anyway, mi nadhani JK kasema "wanaweza" nyinyi mnataka takwimu za "kwanini" ama "kwa vipi"wanaweza wakati nyinyi hamna hata hizo za kwanini hawawezi?
Mnajuwa nyie wasomi wa vitabuni msioweza kuvumbua hata sindano mnatabu kidogo, ndiyo mliotufikisha hapa tulipo, nchi masikini mnatuletea takwimu za kwenye makaratasi tu wakati ukitazama kwa macho tu unakuta njaa kali bado.

Mkuu anasema "wanaweza" mimi nakubalinana naye kuwa baadhi ya sekta wanawake wameweza sana tu, kama mahakama, nimewaona kwa macho yangu akina mama Mjasiri, Kimaro, Munuo etc wakifanya vizuri tu kuliko hata wanaume, wakuu wa mikoa na wilaya kama Hajjat Amina Said Mrisho, Christine Ishengoma, Betty Mkwasa wanaongoza vizuri tu kwa kadiri ya uwezo wao...kweli wanaweza wala haihitaji takwimu hiiiiizo kujuwa kuwa wanaweza, wakuu give the devil his due...tuweni wapinzani lakini penye ukweli tusemeni.

BILA KUMSAHAU HALIMA OMARY DENDEGO DC WA KILOSA......aliyeacha historia makini ya uchapakazi mpwawa na kukabiliana na mafuriko kilosa....big up halima
mix with yours
 
Tuchukulie mfano wa waziri Sofia Simba je anaweza?
tuchukulie mfano wa tibaijuka, asha-rose migiro, stela manyanya anna kilango na halima mdee..je wameweza? sijui nimemweke chiku abwao hapa na mary chipungahelo? anyway list ya mwanzo inatosha
mix with yours
 
Kama rais anawachagua wafanyakazi wanaotokea kuwa wanawake "on the merit" na wanaenda kufanya kazi vizuri, kuwa identify kama "wanawake" ni discrimination.

Wafanyakazi wazuri ni wazuri tu, na wabaya ni wabaya tu, wawe wanawake au wanaume. Sasa atataka kuangalia nini zaidi, kati ya waislamu na wakristo nani wanafanya kazi vizuri zaidi? Kati ya Wakwere na Waha nani wanafanya kazi vizuri zaidi?

Hivi ingekuwaje kama rais angesema "Nimeongeza idadi ya wamasai serikalini, wanafanya kazi vizuri tu, tena kushinda makabila mengine" ? Si watu wangemsema mkabila.

Cheap populism and divisive politics.

Huyu jamaa mie najuta ni kwa nini ni raisi wangu.. nikijaribu kumfikiria sana naona nitatukana ukweli ni kwamba IQ ya mshkaji ni = ...?
wapo mawaziri wanaofaa na wapo ambao hawafai kabisaaa hata kuwa class monitor mfano ni sophia Fisi hafikirii kitu chochote zaidi ya ngono tu! huyo naye ni wakusifia? i support you kiranga 100%
 
Kama rais anawachagua wafanyakazi wanaotokea kuwa wanawake "on the merit" na wanaenda kufanya kazi vizuri, kuwa identify kama "wanawake" ni discrimination.

Wafanyakazi wazuri ni wazuri tu, na wabaya ni wabaya tu, wawe wanawake au wanaume.
Anahangaika kwa kauli zake ambazo ni weightless,si angemwachia Migiro au Tibaijuka au hata Getu wagombee urais, hasa wakati huu ambao afya yake inasumbua ndo tungejua kuwa anaikubali kazi yao!!
 
Back
Top Bottom