Je, Tanzania kuna amani ya kweli?

sindano butu

JF-Expert Member
Aug 20, 2012
503
157
Mtu anakuwa na amani kama ametulia kwenye akili. Ni mtulizo wa akili mtu hapo tunasema ana amani.HUMU tanzania hamna amani kwasababu nyingi. mifano:  1)ela yetu haina thamani 2)polisi kuwakandamiza wananchi pale wanapotaka kupata haki zao 3)wananchi kunyimwa haki zao na MAHAKAMA YA KISUTU  4)matokeo ya form four ni mabovu sijawahi kuona 5) watawala wanachukulia liwalo na liwe hata kama uhai wa watu huko hatarini 6) kufungiwa kwa magazeti yanayotoboa siri. KWA HIYO JAMANI TANZAN HAMNA AMANI bali kunaamani ya kichina. Mi nashangaa polisi wanadiriki kusema eti maandamo yenu yatahatarisha amani wakati WALIOHATARISHA AMANI NI WATAWALA na kifikra wanatakiwa wawatumie FFU WATAWALA!
 
Mtu anakuwa na amani kama ametulia kwenye akili. Ni mtulizo wa akili mtu hapo tunasema ana amani.HUMU tanzania hamna amani kwasababu nyingi. mifano:  1)ela yetu haina thamani 2)polisi kuwakandamiza wananchi pale wanapotaka kupata haki zao 3)wananchi kunyimwa haki zao na MAHAKAMA YA KISUTU  4)matokeo ya form four ni mabovu sijawahi kuona 5) watawala wanachukulia liwalo na liwe hata kama uhai wa watu huko hatarini 6) kufungiwa kwa magazeti yanayotoboa siri. KWA HIYO JAMANI TANZAN HAMNA AMANI bali kunaamani ya kichina. Mi nashangaa polisi wanadiriki kusema eti maandamo yenu yatahatarisha amani wakati WALIOHATARISHA AMANI NI WATAWALA na kifikra wanatakiwa wawatumie FFU WATAWALA!
 
mtu mwenye njaa + madeni ,hawezi kuwa na amani hata siku moja .haya funga hoja yako.
 
mtu mwenye njaa + madeni ,hawezi kuwa na amani hata siku moja .haya funga hoja yako.

Acha zako wewe unazania mimi ni mwanahalisi au labda umetumwa na usalama wa IKULU! Unataka nifunge hoja yangu wewe kama nani? kama unapepo la kova au pepo la USALAMA WA IKULU hapa kwenye jamii forum atutoi maombi. UNAWRZA UKAWA NA MADENI NA NJAA bila kupoteza amani. lakini mi nazungumzia amani ya kiakili ambako mtu anakuwa na hope .KUWA NA HOPE NI MSINGI wa amani .
 
Tujiulize kwa kina kama nchi yetu ni kisiwa cha amani ama la.
Kama Tanzania ni kisiwa cha amani je ni kwa watu gani?
Kama tunaona haturidhiki na majibu yatokanayo mioyoni mwetu je tuchukue hatua gani?
 
Nguvu ya umma ndo itakayorudisha heshima kwa watanzania na democrasia ya kweli
 
Kwa hali ilivyo sasa nchni ni kujidanganya tukisema tuna amani ili hali tunaona mauaji, migomo na mambo mengine kibao yanayoashiria kukosekana kwa amani.!
Kwa ilivyo sasa nchini amani imetoweka na kilichobaki ni utulivu tu na kama tusipochukua hatua hata huo utulivu tutaupoteza.
 
Amani ipo midomoni mwa viongozi wa ccm na watoto zao ambao ndio wengi hapa jf kwaajili ya kuwatetea Kama zomba, Ritz, Rejao, Chama na Majebere
 
mtu mwenye njaa + madeni ,hawezi kuwa na amani hata siku moja .haya funga hoja yako.

kama vigezo vya Amani PESA KUTOKUA NA MADENI basi Eurupe America Japan huko hakuna amani milele kwani ni wadaiwa sug
 
Mtu anakuwa na amani kama ametulia kwenye akili. Ni mtulizo wa akili mtu hapo tunasema ana amani.HUMU tanzania hamna amani kwasababu nyingi. mifano:  1)ela yetu haina thamani 2)polisi kuwakandamiza wananchi pale wanapotaka kupata haki zao 3)wananchi kunyimwa haki zao na MAHAKAMA YA KISUTU  4)matokeo ya form four ni mabovu sijawahi kuona 5) watawala wanachukulia liwalo na liwe hata kama uhai wa watu huko hatarini 6) kufungiwa kwa magazeti yanayotoboa siri. KWA HIYO JAMANI TANZAN HAMNA AMANI bali kunaamani ya kichina. Mi nashangaa polisi wanadiriki kusema eti maandamo yenu yatahatarisha amani wakati WALIOHATARISHA AMANI NI WATAWALA na kifikra wanatakiwa wawatumie FFU WATAWALA!
Mkuu,
Unaulizia tende na halua kwa Mchungaji Mama Lwakatare? Au unaulizia Divai na mkate wa Roho mtakatifu kwa Sheikh Ponda?
 
Ni matumaini yangu u wazima

Kwa muda mrefu nimekua nikijiuliza lakini sijapata jibu, nawe kama huwa unajiuliza basi tuulizane.

Hivi TANZANIA ni nchi ya amani?
 
Mtoa mada sijajua ni amani ipi umelenga ila nisemee amanj kwa upande wa maisha ya ki ujumla haswa maswala ya kiutawala. Kuhusu suala la amani hapa nchini kwetu linategemeana na mtu mmoja mmoja au jamii, mfano mkulima aliyeko kijijini , amabaye maisha yake ni ya kawaida, hawazi siasa na kama anaziwaza ni za kawaida tu, hawazi kumiliki mali nyingi, yeye maisha yake ni kufanya shughuli zake za kujiingizia kipato cha wastani, kula na kunywa, watoto kwenda shule, kubadilishana mawazo na wenzeke kujumuika na familia baada ya kazi kula na kulala alafu kesho akawahi kwenye majukumu yake huyu ana kila sababu ya kusema kuna amani , na watanzania wengi wako kwenye kundi hili. Kwa upande wa pili kuna wale marahibu wa siasa, kutaka mali, vyeo, wizi, dhuluma, ukosoaji wa serikali, kutetea maslahi ya jumla au binafsi, ushindani nk na wengi wao wako mijini, hawa hakika hawawezi kusema kuna amani bali hawana amani japo ni wachache kwa ujumla. Lakini kwa Tanzania ukikosa amani mara nyingi ni hali inapotokea pale unapoitafuta mwenyewe ni mara chache mtu kukosa amani bila kutafuta ukosefu wa amani, mnf huko Congo, Syria, Burundi, Sudan, Ethiopia,Sudani K, RCA, nk hakuna cha nani wala nani, ukosefu wa amani ni mkubwa, haijalishi unahusika kwenye siasa, kukosoa serikali, mkulima, mwanafunzi, mtoto nk wote mara nyingi wanajikuta katika hali ya kukosa amani. Ukitaka kuishi kwa amani hapa kwetu basi jiunge kwenye kundi la kwanza.
 
Kila neno lina tafsirika kulingana na jamii husika na kwa viwango vyao. Milionea wetu ni rofa marekani, furaha na vilio vya walokole makanisani ni kero kwa wengine, nk. Hata amani uisemayo yaweza kuwa ni kwa std yetu.
 
Back
Top Bottom