adriel
Member
- Jul 31, 2015
- 50
- 32
Katika kile ambacho Rais Magufuli huwa anakisema mara nyingi kuwa yeye ni Rais wa wanyonge na masikini ndicho kimenipa kipaumbele cha kuandika uzi huu.
Ni kweli yeye ni Rais wa wanyonge na masikini, lakini hayuko kuwasaidia hao wanyonge na masikini anaowaongoza kwanini??
Kwasababu ameshindwa kutegua kitendawili cha kuwasaidia na kuwafuta machozi hao wanyonge na masikini. Hawa wanyonge na masikini wamesomesha watoto wao kwa kuuza nyanya na pombe, na serikali ikawashika mkono kwa kuwakopesha vijana kwa ajili ya masomo ya elimu ya juuu.
Na vijana hawa hawa, walipomaliza elimu zao za juu ambazo zinawafundisha kutegemea ajira, wanasubiri ajira na Mheshimiwa Rais wa wanyonge na masikini amefunga kabisa zoezi la kuajiri.
Hapa ndipo ninaposema Mheshimiwa Magufuli amefeli pakubwa kwa 100%, na kibaya zaidi anawaongezea deni lao la mikopo kila mwaka kama fee ya kuchelewa kulipa mkopo wao na bodi ya mikopo Tanzania.
Na hilo halitoshi, anapokuja na kauli ya "MAENDELEO HAYANA CHAMA" Na hapa anafeli tena, anatoka kusema hapa Maendeleo hayana chama, hapo hapo anakuambia nichagulieni Diwani na Mbunge wa CCM, anaenda mbali zaidi na kutoa vitisho kwamba MSIPONICHAGULIA HAWA MTAPATA TABU KWELI KWELI, HAMTAPATA MAENDELEO HAPA.
Hapa ndipo ninasema anafeli pakubwa, analeta siasa za ubinafsi na ubabe, ilihali anatuaminisha kuwa MAENDELEO HAYANA CHAMA.
Naomba kuwasilisha
Kutoka Jangwani
Adriel Joseph
Ni kweli yeye ni Rais wa wanyonge na masikini, lakini hayuko kuwasaidia hao wanyonge na masikini anaowaongoza kwanini??
Kwasababu ameshindwa kutegua kitendawili cha kuwasaidia na kuwafuta machozi hao wanyonge na masikini. Hawa wanyonge na masikini wamesomesha watoto wao kwa kuuza nyanya na pombe, na serikali ikawashika mkono kwa kuwakopesha vijana kwa ajili ya masomo ya elimu ya juuu.
Na vijana hawa hawa, walipomaliza elimu zao za juu ambazo zinawafundisha kutegemea ajira, wanasubiri ajira na Mheshimiwa Rais wa wanyonge na masikini amefunga kabisa zoezi la kuajiri.
Hapa ndipo ninaposema Mheshimiwa Magufuli amefeli pakubwa kwa 100%, na kibaya zaidi anawaongezea deni lao la mikopo kila mwaka kama fee ya kuchelewa kulipa mkopo wao na bodi ya mikopo Tanzania.
Na hilo halitoshi, anapokuja na kauli ya "MAENDELEO HAYANA CHAMA" Na hapa anafeli tena, anatoka kusema hapa Maendeleo hayana chama, hapo hapo anakuambia nichagulieni Diwani na Mbunge wa CCM, anaenda mbali zaidi na kutoa vitisho kwamba MSIPONICHAGULIA HAWA MTAPATA TABU KWELI KWELI, HAMTAPATA MAENDELEO HAPA.
Hapa ndipo ninasema anafeli pakubwa, analeta siasa za ubinafsi na ubabe, ilihali anatuaminisha kuwa MAENDELEO HAYANA CHAMA.
Naomba kuwasilisha
Kutoka Jangwani
Adriel Joseph