Je, ni kweli p2 inazuia mimba?

MissRaya

Member
Sep 23, 2021
22
24
Habari za mda huu, naamini ni wazima wa afya na kama yupo anaeumwa Mungu atampa nafuu.

Niende kwenye point, iko ivi nilisex na mme wangu siku 2 baada ya KUMALIZA hedhi, yaani zile siku ambazo ni salama ila alimwagia ndani😥

Ikabidi nitumie p2 mapema kabla ya masaa 24 kuisha. Yote ni kuhofia nisije beba mimba nyingine maana nina mtoto wa miezi 7 now.

So naomba kwa wenye uzoefu wa hizo p2 mnijuze, kuwa ni kweli zinazuia ujauzito?
 
Cha kwanza Ni lazima ujue siku za kushika mimba Ni zipi ndio utakua na uhakika wa kuizuia hiyo mimba;

kimsingi kwa walio wengi siku za kushika mimba Ni KUANZIA siku ya 10 Hadi 17 tangu siku ya kwanza kuona hedhi.

Kwa mantiki hii wewe hapo hukua ktk hatari yoyote vya kubeba mimba.
Kwa maelezo Zaid karibu Dm
 
Siku 2 baada ya hedhi huwezi kupata ujauzito.

Hizi P2 kuweni nazo makini zitawaleteeni matatizo huko mbeleni, maana watu wamekuwa wakizitafuna kama peremende vile.

Inashauriwa kuzitumia si zaidi ya mara 2 kwa mwaka. Ila sasa imekuwa kama fashion wakimwagiwa ndani tu P2.
 
Hizo P2 haziaminiki sana, kuna cases za waliotumia kwa usahihi na hazikuwasaidia.
 
P2..inachofanya ni kufanya ute wa mwanamke kuwa mzito kuliko kawaida hivyo sperm za mwanamme zinashindwa kusafiri kupitia ute huo kwenda kurutubisha mayai..

Ndio maana zinatumiwa ndani ya masaa 72 baada ya sex hii ni kwa sababu kipindi hiki mayai yanaweza kuwa hayajachavushwa na sperm..japo hushauriwa zaidi kutumia ndani ya masaa 24 kwa uhakika zaidi..

Nimesikitika sana mleta mada unasema una watoto saba na bado haujajua siku za hatari kubeba mimba..
 
Hautapata ujauzito, kuwa na amani; miaka ya nyuma mchepuko alikuwa anatumia sana hizo na zilimsaidia.
 
Hivi ukiwa na irregular cycles siku ya pili baada ya hedhi unaweza kupata mimba?😳
Hauwezi kupata mimba, irregular cycles ni mabadiliko tu ya tarehe za kuuona mwezi, kama Ilikuwa inaanza tarh 5 basi utaona tu haieleweki, mwezi huu tarh 5 ujao trh 8 ama tarh zinarudi nyuma.

Hapa ndo mimba zisizotarajiwa zinaweza kutokea. (Lakini si kwa siku 2 baada ya hedhi).
 
Alikuwa na hamu ya kunywa dawa tu.
Cha kwanza Ni lazima ujue siku za kushika mimba Ni zipi ndio utakua na uhakika wa kuizuia hiyo mimba; kimsingi kwa walio wengi siku za kushika mimba Ni KUANZIA siku ya 10 Hadi 17 tangu siku ya kwanza kuona hedhi... Kwa mantiki hii wewe hapo hukua ktk hatari yoyote vya kubeba mimba.
Kwa maelezo Zaid karibu Dm
 
Siku 2 baada ya hedhi huwezi kupata ujauzito.

Hizi P2 kuweni nazo makini zitawaleteeni matatizo huko mbeleni, maana watu wamekuwa wakizitafuna kama peremende vile.
Inashauriwa kuzitumia si zaidi ya mara 2 kwa mwaka. Ila sasa imekuwa kama fashion wakimwagiwa ndani tu P2.
sawa nimekuelewa😍👍👍
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom